Ni nani atakaye mtikisa na kumng'oa Mh Mzindakaya jmbo la Kwela?

MovingForward

JF-Expert Member
Nov 10, 2009
489
49
Tunapozungumzia wabunge waliokaa bungeni kwa muda mrefu, hatuwezi kumsahau Mzindakaya ambaye alitimiza miaka arobaini bungeni mara baada ya uchaguzi wa 2005.

Tunapopima maendeleo ya jimbo la kwela, tukilinganisha na muda aliotumika bungeni, ingawa kwa vipindi vichache, tangu wakati ule likiwa ni sehemu ya jimbo la Sumbawanga vijijini, hatuoni jambo lolote la mfano ambalo tunaweza kuzipongeza jitihada zake.

Kwa wale waliopata kufika au kupata habari za jimbo hilo kwa kina ninawaombeni tuingine ndani ya mada hii tuichambue mada hii: Je! Ni nani atakaye mtikisa na kumng'oa Mzindakaya?
 
Huyu Mzee ni fisadi nambari wani kwani amekwapua hele benki kuu na kujifanya anaanzisha kiwanda cha nyama huko kwao hakuna lolote; aliingia ubia na wazungu kwenye biashara ya uwindaji mpaka sasa anadaiwa na serikali mamilioni ya shilingi , kinga yake kuwatisha mawaziri wa maliasili kuwa atawalipua na kashfa zao bungeni hivyo hawamdai!! Mtu anayeweza kumuondoa kule kwenye ubunge ni Didas Mfupe ingawa yeye anataka kumrithisha mwanae wa kiume kwa kupitia mgongo wa Umoja wa vijana.! Safari hii hana lake.
 
Didas Mfupe si huyu mzee aliyejiunga na NCCR- Mageuzi?

Sasa huyu mzindakaya anapotaka kumwingiza mtoto wake kugombea ubunge, jimbo la kwela, limekuwa ni jimbo la familia kama ya mfalme Mswat? Je! Huyu Mtoto wa Mzindakaya ana CV gani? Hapo Mzindakaya anataka kuendelea kutawala kwa mgogo wa mwanae au siyo?
 
Mbona mwenyewe aliwahi kunukuliwa akisema kuwa hatagombea tena,maana nionavyo keshajichumia sana.
 
Junius nami hapo ndo nazidi kushangaa, huu si u-popo wa mara myama mara ndege? Huyu mwingine D Mfupe analolipi jipya?
 
Tunapozungumzia wabunge waliokaa bungeni kwa muda mrefu, hatuwezi kumsahau Mzindakaya ambaye alitimiza miaka arobaini bungeni mara baada ya uchaguzi wa 2005.

mamamaaaaa, yani huyu yuko mjengoni hata kabla wazazi wangu hawana mpango wa kunizaa???, aaarrrggggh ANG'OLEWE.
 
Atakayemngoa ni mwanaye Violeth Mzindakaya , kwani huo ni utamaduni wa ndani ya CCM
 
Haki sawa uko ok!. Sasa hapo Vailet Mzindakaya atakuwa amechukua mikoba ya baba yake!! Amemrithi au siyo? Hapo hatuwezi kusema ameng'olewa! Check ya F Castro kule Cuba. Mzee wa watu alipochoka tu, mdogo wake kalamba post. Sasa hapo ameng'olewa au amempisha tu mdogo wake akamate nchi.

Lililopo hapo ni ufisadi. Hivi tu mwanae akimbadili, ataweza kusimama sawasawa kutetea maslahi ya jimbo lao, au ataendekeza ufisadi wa baabaye?

Na huko kwao hakuna koo nyingine ni za Mzindakaya tu? Hivi kule kwao hakuna wasomi na wanasiasa wanaoweza kujitokeza!! Au ndiyo nao wanafyata miguu kwa kile alichokisema Shapu hapo juu?

Du! yale yale ya Zanzibar. Baada ya Amani , tutarajie mdogo wake (Balozi Karume atajitokeza tena!).

Huko Rukwa hakuna wana JF watupatie newz zaidi?
 
Atakayemngoa ni mwanaye Violeth Mzindakaya , kwani huo ni utamaduni wa ndani ya CCM

Utamaduni ndiyo! lakini kwa faida ya nani? Abeid Karume = Amani Abeid Karume. Yusuph Makamba = January Makamba. Moses Nnauye = Nape Nnauye. Rashid Kawawa = Vita kawawa. Kighoma Malima = Adam Malima. Ally Hassan Mwinyi = Hussein Mwinyi. WHY not Vailet Mzindakaya??
 
Tunapozungumzia wabunge waliokaa bungeni kwa muda mrefu, hatuwezi kumsahau Mzindakaya ambaye alitimiza miaka arobaini bungeni mara baada ya uchaguzi wa 2005.

Tunapopima maendeleo ya jimbo la kwela, tukilinganisha na muda aliotumika bungeni, ingawa kwa vipindi vichache, tangu wakati ule likiwa ni sehemu ya jimbo la Sumbawanga vijijini, hatuoni jambo lolote la mfano ambalo tunaweza kuzipongeza jitihada zake.

Kwa wale waliopata kufika au kupata habari za jimbo hilo kwa kina ninawaombeni tuingine ndani ya mada hii tuichambue mada hii: Je! Ni nani atakaye mtikisa na kumng'oa Mzindakaya?


Kama amedumu muda wote huo... basi haiyumkini tunayo institutional memory ya binadamu ukiacha hansards!
Kadhalika inaonyesha imani kubwa waliyo nayo wapiga kura wake!
 
Kama amedumu muda wote huo... basi haiyumkini tunayo institutional memory ya binadamu ukiacha hansards!
Kadhalika inaonyesha imani kubwa waliyo nayo wapiga kura wake!
hakuna cha imani hapa, cristan majiyatanga mzindakaya anaogopewa kwa uchawi jimboni mwake. lisemwalo ni kwamba baba ake alikuwa mchawi aliyebobea hamna mfano na amekabidhi mikoba kwa mwanae cristan. watu wa kwela wanamlalamikia kichinichini tu hamna mwenye ubavu wa kumsema mbunge wao hadharani, awe msomi au mjinga. kwa mantiki hii kama watu wa sumbawanga hawataachana na imani za kishirikina akina mzindakaya wataendelea kuwabumbuwaza milele.
naye sista v hafai hata kidogo kuongozi lakn ndo utaukwa ubunge. mume wake ambaye ni bodigad wa makamba alimfumania laivi akila uloda akampa mkong'oto hadharani akamvunja mkono na kumpa talaka. ni mlevi kupindukia huyu kirukanjia kujiaibisha ni kila wakti.
 
Mmmmmmh Sasa Jembe Ulaya hapo umechimbua mizizi. Sasa huyo sista V kama hata nyumba yake imemshinda, jimboni ataweza?. Tena ni mlevi! Yale yale ya kulala bungeni, halafu mtu anaibuka na kusema "ninaunga mkono hoja ya mbunge aliyetangulia" wakati yeye ndiye wa kwanza!!!. Hivi sasa tuseme watu wa Rukwa hawathamini mkoa wao?

By the way, Huyo Sist Vaiolet ana elimu gani? Maana isije ikawa kama baba yake, darasa la nane, halafu ghafla kaibukia u- Dr (Phd????????)
 
Back
Top Bottom