Ni NANI aliyemuua?

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Mwalimu wa Historia anawauliza wanafunzi wake
Mwalimu: Eeenhe! Ni nani aliyemuua Chifu Mkwawa?
Mwanafunzi wa kwanza; Aka sio mimi!
Mwanafunzi wa pili:Wallahi siyo mimi ati!
Mwnafunzi wa tatu: Sio mimi,kwanza mimi jana sikuja shule
Mwalimu alipoona wanafunzi wote ni majuha akaamua kumuita Mkuu wa Shule.Mkuu wa Shule alipokwenda akawauliza lile swali kwa mikwara na vitisho vya kutosha.Mambo yakawa vilevile. Mkuu wa Shule aakamwita Mwalimu wa Historia pembeni na kumnong'oneza " Lakini una uhakika muuaji yupo darasa hili? Du,kumbe naye ni kilaza...
 
Mmenifanya nicheke hadi nimeonekana kituko ndani ya gari, siku nyingine muwe mnatoa warning!
 
Ngoja kwanza primary au o level?!!

Sent from my BlackBerry 9360 using Jamie's
 
Ha ha ha kwa elimu yetu mbovu ya siku hizi sitashangaa
haya yakitokea kweli mkuu hafahamu historia
 
Mwalimu wa Historia anawauliza wanafunzi wake
Mwalimu: Eeenhe! Ni nani aliyemuua Chifu Mkwawa?
Mwanafunzi wa kwanza; Aka sio mimi!
Mwanafunzi wa pili:Wallahi siyo mimi ati!
Mwnafunzi wa tatu: Sio mimi,kwanza mimi jana sikuja shule
Mwalimu alipoona wanafunzi wote ni majuha akaamua kumuita Mkuu wa Shule.Mkuu wa Shule alipokwenda akawauliza lile swali kwa mikwara na vitisho vya kutosha.Mambo yakawa vilevile. Mkuu wa Shule aakamwita Mwalimu wa Historia pembeni na kumnong'oneza " Lakini una uhakika muuaji yupo darasa hili? Du,kumbe naye ni kilaza...

Dunia hii vilaza hawataisha kamwe...
 
Mambo haya ndo yanayoifanya JF kuwa spesho! Asante mkuu, umenifanya nifurahi.
 
Back
Top Bottom