Kuna maswali mengi nyuma ya kiinimacho kilichotangazwa na kamanda Kova juu ya utekaji wa dr Ulimboka. kati ya mengi, Maswali yafuatayo yana wafanya Tanzania wasiamini taarifa ya jeshi la polisi juu ya utekaji na utesaji aliofanyiwa dr Ulimboka.
- Kwamba mtekaji alienda kufanya toba kanisani haiingii akilini hata kidogo.Si rahisi kiasi hicho kwanza kanisa lipo kila mahali. Toba hiyo ingeweza kufanyika Kenya, Uganda na nchi nyingine bila hatari ya mtuhumiwa kukamatwa.
- Kwamba mtekaji alitumwa na mtu asiyemfahamu tena anafanya kazi serikalini,serikali ipi ya Kenya au hii ya JK? Kwa hiyo Watanzania walikuwa sahihi kuituhumu serikali? Mbona waziri mkuu na Rais walikanusha kwa sauti kali tena ya kuapa? Haya mwajiri wa mtekaji anafanya idara ipi? Kama mwajiri na mwajiriwa hawafahamiani mshahara baada ya kazi ulilipwa vipi? Nani alishawahi kuajiriwa bila kufahamiana kwanza na mwajiri? Kujaza mkataba wa kazi?
- Mbona katika hili taarifa ya polisi haikuonyesha picha ya mtuhumiwa? Mbona watuhumiwa wengine huonyeshwa picha zao pindi wanapokamatwa?
- Kwa madhehebu mengi ya Kikristo, toba haifanywi kwa kwenda kuisema dhambi kwa mchungaji isipokuwa kanisa Katoliki,Je kanisa aliloenda mtekaji lina utaratibu huo wa toba?
- Kwamba polisi imemnasa mtuhumiwa,kwa taarifa hiyo ndo mwisho wa uchunguzi wa chaini ya kiharifu iliyo nyuma ya tukio hili?