Ni namna gani unapaswa 'kujilipa' kutokana na kipato chako?

Ncha Kali

JF-Expert Member
Sep 19, 2019
14,497
26,986
Salamu wakuu!

Imekuwa kawaida kusikia watu wakisema kuhusu kujilipa mshahara, binafsi kwa mara ya kwanza nilisoma hii nadharia kwenye moja ya vitabu hamasishi vya uhuru wa kifedha.

Kitabu hiki ni maarufu kwa jina lake, ”The Richest Man in Babylon”. Kwa mujibu wa mwandishi wa kitabu, yeye anasisitiza hakikisha 30% ya kila unachokipata inakuwa ya kujilipa wewe.

Mfano kipato chako ni LAKI MOJA kwa mwezi, basi tenga 30,000/- kwa ajili yako. Kisha kiasi kinachobaki ndo kitumike kwenye shughuli zingine mfano gharama za familia kwa kadri ya majukumu yako, ikiwemo 10% ya Mungu [hili sikumbuki kama alilitaja, lakini ni muhimu].

Binafsi nikiri kuwa sijawahi kujilipa. Huenda kwa kutokujua namna gani nijilipe, au ni visingizio tu vya kipato kutokukidhi.

Kwa maana kila shilingi ikipatikana tayari inasubiliwa kumaliza au kusogeza jukumu fulani. Hata ikitokea isitumike muda huo basi itakuwa kuna lengo mahsusi lenye kuhitaji pesa ndefu, hivyo itakaa kwa muda ili tu kusubiri hesabu itimie.

Kwa ajili yangu na familia, nikimudu mahitaji ya muhimu kwangu naona kama nipo sawa tu.

Sasa naomba tupeane mawazo na uzoefu, kwa wale wenye nia au waliofanikiwa kujilipa. Unachora wapi mstari kwamba hiki kibubu ni kwa ajili yangu tu na kile ni cha familia?

Je, kujilipa ni kujiwekea akiba ya baadae au ni kujihudumia vema kwa muda huo? Mfano kujistarehesha kwa vitu roho inapenda, na hapo iwe nje ya kile ambacho unatumia na familia yako mwenyewe?

Natamani watu wanielewe ila sidhani kama ninaweza kuandika zaidi ya hivi, pengine kupitia mawazo ya wadau wengi tutaweza kuelewa vizuri.

Ni kwa jinsi gani huwa unajilipa?
 
The richest man in Babylon by George S Clason ni moja ya kitabu bora sana. Changamoto ya kuapply ni kwamba Africa shida chungu nzima yaani hata kujilipa tu haipatikani labda kwa ambao hajaoa au kuolewa.
 
The richest man in Babylon by George S Clason ni moja ya kitabu bora sana. Changamoto ya kuapply ni kwamba Africa shida chungu nzima yaani hata kujilipa tu haipatikani labda kwa ambao hajaoa au kuolewa.

Hebu endelea kidogo, kwahiyo kipato chako (hicho kidogo) kinakuwa sio kwa ajili yako!
 
Aisee hii kujilipa uki-apply 100% kwa bongo unataitwa mbinafsi.
Na ndio theme ya kujilipa..
Lazima utakuwa unajali wa familia yako tu.
Kiyosaki yeye alienda mbali akasema WIII-FM yaani What Is In It For Me ...
Kila ukitaka kutoa pesa unajiuliza itaninufaisha vipi nikikusaidia kwa hiyo pesa itoke ili kuleta faida kwa ajili yangu ndo maana ya hiyo statement.
Kwa tafsiri ya Afrika huu ni ubinafsi
 
Na ndio theme ya kujilipa..
Lazima utakuwa unajali wa familia yako tu.
Kiyosaki yeye alienda mbali akasema WIII-FM yaani What Is In It For Me ...
Kila ukitaka kutoa pesa unajiuliza itaninufaisha vipi nikikusaidia kwa hiyo pesa itoke ili kuleta faida kwa ajili yangu ndo maana ya hiyo statement.
Kwa tafsiri ya Afrika huu ni ubinafsi

Kiyosaki kasema iv kwenye which of his book or seminar?!
 
Chief!, Kila kitu ni mipango na elimu, maana yake ni kuwa ukitaka maendeleo unatakiwa kuwa na mipango kwa ajili ya hayo maendeleo, sasa ili upange mipango vizuri inatakiwa pia upate elimu kwa ajili ya hicho unachotaka kukipanga. Sasa ikiwa mambo yatakwenda vizuri kwa hiyo mipango yako ndiyo utapata matokeo mazuri (faida) na moja ya faida hiyo ni fedha, hivyo basi fedha ni matokeo.

Kwa bahati mbaya sisi tulio wengi (nikiwemo na mimi) hatuna elimu ya kutuwezesha kupambana na hali zetu kikamilifu, ndiyo maana hata wasomi wetu walio wengi ni waoga wa maisha kwa maana wana elimu ya kukariri (siyo kosa lao) ambayo walisomeshwa ili waajiriwe hivyo wanapokosa ajira ni wachache wanaoweza kuwa na mpango namba mbili (Plan B).

Nikirudi kwenye hoja yako ni kuwa suala la kujilipa linawezekana ukiwa una nia thabiti ya kufanya hivyo, kwa kuwa nia hiyo ndiyo itakayokupelekea kupanga mipango ya kufanya hivyo, utaanza taratibu (mwanzo mgumu) kwa kuainisha mahitaji ya lazima na yale yasiyo ya lazima, namna ya kununua vitu na mahitaji mbalimbali na utaendelea kisha baadaye utazoea.

Mimi sikuwahi kusoma hicho kitabu lakini kuna mtu alikisoma na akaniambia habari hiyo, kiukweli ilinivutia nikaona nijaribu (inahitaji moyo mgumu lakini). Ikiwa kipato chako ni cha mwezi hakikisha unapokipata unanunua mahitaji muhimu kwa bei ya jumla ya kuweza kutosha mwezi mzima na pia hakikisha unajali ubora kwa kila unachonunua maana ukizingatia unafuu pekee itakugharimu mbele ya safari.

Nina mengi ya kuandika ila mkono umechoka lakini cha kuzingatia hasa ni kutoenda kinyume na nia yako thabiti uliyojiwekea na usiwe mtu wa kukata tamaa katika kujaribu. Achana na marafiki wanaopenda kukushusha kila wakati kwa kukwambia kuwa huwezi, hakikisha unajaribu jambo kwa maana hata ukishindwa tayari unakuwa umepata uzoefu.
 
Na ndio theme ya kujilipa..
Lazima utakuwa unajali wa familia yako tu.
Kiyosaki yeye alienda mbali akasema WIII-FM yaani What Is In It For Me ...
Kila ukitaka kutoa pesa unajiuliza itaninufaisha vipi nikikusaidia kwa hiyo pesa itoke ili kuleta faida kwa ajili yangu ndo maana ya hiyo statement.
Kwa tafsiri ya Afrika huu ni ubinafsi
Kitabu kipi umenukuu ndugu, samahani,...maana Kiyosaki ana vitabu vingi, naomba kukifahamu yakini ntapata mzuka wa kukipitia.
 
Back
Top Bottom