Ni namna gani barua inayotumwa kwa Kampuni ya US kwa ajili ya msaada inaandikwa?

Lawrichie

JF-Expert Member
Aug 27, 2013
753
2,044
Amani iwe nanyi nyote.

Ndugu zangu, hivi karibuni nilipata mchongo kutoka kwa rafiki yangu ambae yuko US kwamba kuna kampuni ambayo inawasaidia watu kutoka nchi mbalimbali, watu ambao wanatamani kufanya kazi US, kujiendeleza kielimu, kuhamia na kuwa na makazi ya jumla au kwa ajili ya utalii tu.

Huyu binti tuna kama miezi 8 hivi toka tufahamiane japo bado hatujaonana, ila yeye ndie aliyenishauri nijaribu kutuma barua pepe ya maombi kwenye kampuni ambayo amenitajia kuelezea shauku yangu ya kufanya kazi US.

Sasa basi ndugu zangu, nimeandika uzi huu ili nipate uzoefu kwa watu mbalimbali waliowahi kuandika ama wanafahamu jinsi gani barua ya aina hii huwa inaandikwa au jinsi gani inatakiwa iwe. Nimeshapekua Google nimepata mwanga wa angalau nini natakiwa nifanye lakini nafikiri JamiiForus ina watu makini zaidi karibu katika kila kitu.

Sijawahi kuandika barua ya aina hii kabla, hivyo nataka nikiandika kusiwe na kasoro. Barua natakiwa niitume kwenye kampuni kuwajulisha nia yangu ya kufanya kazi kwa Trump na jinsi gani nawaamini wao katika kufanikisha adhma yangu.

Naamini nitasaidiwa kupitia hili jukwaa huru.

Karibuni.
 
Wengi wetu tumeishia MEMKWA na hatujawahi kuomba kazi kwa Trump hata hapo kwa Kenyatta.
Ningekusaidia ndugu yetu ila ndio hivyo!!
Tusamehe bure!!

Ni kweli ndugu, hata mimi Elimu ya kuungaunga tu lakini fursa inapotokea inabidi uitumie tu... ndio maana nikaamua kuja kuomba ushauri humu jukwaani...
 
Ni kweli ndugu, hata mimi Elimu ya kuungaunga tu lakini fursa inapotokea inabidi uitumie tu... ndio maana nikaamua kuja kuomba ushauri humu jukwaani...
Ninacho kushauri ukituma hiyo barua na wakianza kukwambia tuma pesa kwa ajili ya application/process fee tafadhali naomba uwatukanie wazazi wao matusi ya nguoni na kama utashindwa niambie mm najua kutukana kwa kiinglish japokuwa nimeishia MEMKWA.
 
Ninacho kushauri ukituma hiyo barua na wakianza kukwambia tuma pesa kwa ajili ya application/process fee tafadhali naomba uwatukanie wazazi wao matusi ya nguoni na kama utashindwa niambie mm najua kutukana kwa kiinglish japokuwa nimeishia MEMKWA.

Nimekuelewa, asante kwa ushauri...
 
Amani iwe nanyi nyote.

Ndugu zangu, hivi karibuni nilipata mchongo kutoka kwa rafiki yangu ambae yuko US kwamba kuna kampuni ambayo inawasaidia watu kutoka nchi mbalimbali, watu ambao wanatamani kufanya kazi US, kujiendeleza kielimu, kuhamia na kuwa na makazi ya jumla au kwa ajili ya utalii tu.

Huyu binti tuna kama miezi 8 hivi toka tufahamiane japo bado hatujaonana, ila yeye ndie aliyenishauri nijaribu kutuma barua pepe ya maombi kwenye kampuni ambayo amenitajia kuelezea shauku yangu ya kufanya kazi US.

Sasa basi ndugu zangu, nimeandika uzi huu ili nipate uzoefu kwa watu mbalimbali waliowahi kuandika ama wanafahamu jinsi gani barua ya aina hii huwa inaandikwa au jinsi gani inatakiwa iwe. Nimeshapekua Google nimepata mwanga wa angalau nini natakiwa nifanye lakini nafikiri JamiiForus ina watu makini zaidi karibu katika kila kitu.

Sijawahi kuandika barua ya aina hii kabla, hivyo nataka nikiandika kusiwe na kasoro. Barua natakiwa niitume kwenye kampuni kuwajulisha nia yangu ya kufanya kazi kwa Trump na jinsi gani nawaamini wao katika kufanikisha adhma yangu.

Naamini nitasaidiwa kupitia hili jukwaa huru.

Karibuni.
Naona mtu akilizwa muda si mrefu hapa. Huyo binti ni wa wapi? Angalia sana hakuna cha binti hapo. unawasiliana na dume na linasubiri kukupiga kwa kukuambia utume ada. Tafakari: Kama hata kuandika barua simple tu hujui, ni kazi gani unategemea kufanya?
 
Naona mtu akilizwa muda si mrefu hapa. Huyo binti ni wa wapi? Angalia sana hakuna cha binti hapo. unawasiliana na dume na linasubiri kukupiga kwa kukuambia utume ada. Tafakari: Kama hata kuandika barua simple tu hujui, ni kazi gani unategemea kufanya?

Nashukuru kwa ushauri. Nina uhakika na hili hilo sina wasiwasi, kuhusu barua ni kwamba sijawahi kuandika barua ya aina hii hapo kabla, ndiyo maana nimeomba muongozo tu kwa sababu naamini kuna wengi wamewahi kuandika barua ya aina hii hapo kabla...
 
Nashukuru kwa ushauri. Nina uhakika na hili hilo sina wasiwasi, kuhusu barua ni kwamba sijawahi kuandika barua ya aina hii hapo kabla, ndiyo maana nimeomba muongozo tu kwa sababu naamini kuna wengi wamewahi kuandika barua ya aina hii hapo kabla...
Sawa kama una uhakika naye. Kuhusu barua ni kwamba unaandika na kujieleza wewe ni nani, unaishi wapi, una elimu gani, unataka wakufanyie nini (hao unaowandikia) na kwa nini!
 
Raia wanakwepa uzi wangu...

Kabla ya yote niseme kwamba mimi si mtaalamu wa masuala ya uhamiaji Marekani, na kwa msaada wa kisheria tafuta mtaalamu/ mwanasheria wa masuala ya uhamiaji Marekani, au uliza ubalozi wa Marekani ulio karibu nawe.

Sio raia wanakwepa uzi mkuu. Raia tupo tumeuheshimu uzi kwa kuupa muda sawia wa tafakari kabla ya kujibu.

Unajua ukipewa swali zito, ni heshima kulifanyia tathmini vizuri kabla ya kulijibu.

Mathalani, swali lako ningeweza kulipa majibu rahisi ambayo hayana utafiti, lakini, kwa kukupa majibu rahisi ningeweza kufanya mawili.

Ama:-

1. Kukuvunja moyo kukupa jibu la hasi sana kwa jambo ambalo lipo na linawezekana ila mimi silijui vizuri ingawa nimeishi Marekani miaka mingi.

Au

2. Kukujaza ujinga kwamba vitu hivi vinawezekana na ni rahisi bila uchunguzi wa kina, na kufanya upate matumaini yaliyotokana na uongo au uzembe wa mshauri wako.

Sasa basi.

Kwa kuwa kuna utata mwingi kwenye hizi habari - nakumbuka kijana mmoja alikwenda mpaka ubalozi wa Marekani Dar kuulizia, akaambiwa ubalozi wa Marekani Tanzania hauna "Labor Attache", swali lake litapelekwa Nairobi- ningependa kuanza kwa kusema hivi.

1. Chukulia tahadhari sana habari hizi na uzifanyie kazi kwa uchunguzi. Hususan kama umeombwa kutanguliza hela. Habari za kufanya kazi Marekani ni ndefu na zina utata mwingi.

2.Huyo binti kampuni aliyoitaja ana uhusiano nayo gani? Ni kampuni yao? Anajuana na mabosi wake? Au hana uhusiano nayo? Ni rahisi kama unajuana na mtu mwenye uhusiano wa hiyo kampuni akakusaidia.

3. Kimsingi, makampuni yana uwezo wa kumfanyia sponsorship mtu asiye Mmarekani au asiye na ukazi wa kudumu wa Marekani (Green card) ili aje kufanya kazi Marekani. Lakini, visa hizi zina vikwazo vingi na masharti mengi ya kutaka kuonesha kwamba hakuna Wamarekani/ kuna upungufu wa Wamarekani wenye uwezo wa kufanya kazi hizo.

Sasa wewe hata kama unapata kampuni inayotaka kukufadhili, una kipaji gani ambacho kina upungufu Marekani ambacho unaweza kukitumia kama kigezo?

Mfano mmoja wa visa hizi ni H1B visa. Kwa Zaidi soma hapa


Hapa zimeandikwa habari za visa nyingine kama H1B, kwa mfano kwa watu ambao hawana vipaji au usomi unaotakiwa na visa ya H1B.


Naomba upitie habari nilizoweka hapa kwanza, kabla ya kuendelea na mazungumzo Zaidi.
 
  • Thanks
Reactions: Obe
Una uwezo wa kuandika/ kusoma Kiingereza?

Nina uwezo wa kusoma na kuongea kingereza vizuri sana... Wakati mwingine ni vizuri tu kuomba ushauri kuliko kujifanya unajua kila kitu. Kuuliza si ujinga ni njia mojawapo wa kujifunza kwa ufanisi zaidi.
 
Kabla ya yote niseme kwamba mimi si mtaalamu wa masuala ya uhamiaji Marekani, na kwa msaada wa kisheria tafuta mtaalamu/ mwanasheria wa masuala ya uhamiaji Marekani, au uliza ubalozi wa Marekani ulio karibu nawe.

Sio raia wanakwepa uzi mkuu. Raia tupo tumeuheshimu uzi kwa kuupa muda sawia wa tafakari kabla ya kujibu.

Unajua ukipewa swali zito, ni heshima kulifanyia tathmini vizuri kabla ya kulijibu.

Mathalani, swali lako ningeweza kulipa majibu rahisi ambayo hayana utafiti, lakini, kwa kukupa majibu rahisi ningeweza kufanya mawili.

Ama:-

1. Kukuvunja moyo kukupa jibu la hasi sana kwa jambo ambalo lipo na linawezekana ila mimi silijui vizuri ingawa nimeishi Marekani miaka mingi.

Au

2. Kukujaza ujinga kwamba vitu hivi vinawezekana na ni rahisi bila uchunguzi wa kina, na kufanya upate matumaini yaliyotokana na uongo au uzembe wa mshauri wako.

Sasa basi.

Kwa kuwa kuna utata mwingi kwenye hizi habari - nakumbuka kijana mmoja alikwenda mpaka ubalozi wa Marekani Dar kuulizia, akaambiwa ubalozi wa Marekani Tanzania hauna "Labor Attache", swali lake litapelekwa Nairobi- ningependa kuanza kwa kusema hivi.

1. Chukulia tahadhari sana habari hizi na uzifanyie kazi kwa uchunguzi. Hususan kama umeombwa kutanguliza hela. Habari za kufanya kazi Marekani ni ndefu na zina utata mwingi.

2.Huyo binti kampuni aliyoitaja ana uhusiano nayo gani? Ni kampuni yao? Anajuana na mabosi wake? Au hana uhusiano nayo? Ni rahisi kama unajuana na mtu mwenye uhusiano wa hiyo kampuni akakusaidia.

3. Kimsingi, makampuni yana uwezo wa kumfanyia sponsorship mtu asiye Mmarekani au asiye na ukazi wa kudumu wa Marekani (Green card) ili aje kufanya kazi Marekani. Lakini, visa hizi zina vikwazo vingi na masharti mengi ya kutaka kuonesha kwamba hakuna Wamarekani/ kuna upungufu wa Wamarekani wenye uwezo wa kufanya kazi hizo.

Sasa wewe hata kama unapata kampuni inayotaka kukufadhili, una kipaji gani ambacho kina upungufu Marekani ambacho unaweza kukitumia kama kigezo?

Mfano mmoja wa visa hizi ni H1B visa. Kwa Zaidi soma hapa


Hapa zimeandikwa habari za visa nyingine kama H1B, kwa mfano kwa watu ambao hawana vipaji au usomi unaotakiwa na visa ya H1B.


Naomba upitie habari nilizoweka hapa kwanza, kabla ya kuendelea na mazungumzo Zaidi.

ASANTE KWA MUONGOZO KIONGOZI. HUYU BINTI ANAFANYA KAZI KWENYE HII KAMPUNI, HIVYO ALIFANYA KUNISHAURI TU NA KUNIPA NJIA ZA NAMNA GANI NAWEZA KUFANYA KAZI KULE...
 
Back
Top Bottom