Uchaguzi 2020 Ni Mwaka wa Uchaguzi Mkuu 2020: Kuthibitisha au Kutengua Maamuzi ya 2015?

Taja mikoa na majibu ambayo CDM ilishinda. Hii ya kila uchaguzi kuwa CDM ilishinda ni strategy za kijinga ili wakuu wa Sacco's wasichukuliwe hatua za kichama. Nyumbu wanafuata bila kuuliza maswali magumu. Long way to go
Kwa ujumla mgombea wa UKAWA alipata zaidi ya kura mil 10 , Mgombea wa ccm alipata kura mil 3 unusu tu , Kinana , January , Kapilimba na JK wanalifahamu hili , haikuwa rahisi kwa mtu mwenye akili timamu kumchagua Magufuli .

Na hii laana ya kuiba kura ndio inayowatafuna akina Kinana , January na Kapilimba , bado Kikwete naye yake yanaandaliwa mwaka huu
 
Wewe Mzee inaonekana umepata bwana mpya, babu la kizungu.

Una unafiki uliokomaa na kuvuka mipaka
 
CCM itaendelea kuendesha nchi kwa miaka yote, sababu hakuna upinzani makini na mahiri wa kuweza kushindana na chama dola kwa hivi sasa, vyama vya upinzani vimetezwa nguvu na watanzania wengi ni watu wa maslahi, kura zao zinanunuliwa kwa thamani ndogo za fedha na wengine huhadaiwa kwa lugha nzuri za ahadi zisizotekelezwa, tumeona jinsi ya wabunge na baadhi ya watu waliyo hamia CCM kwa kisingizio cha kuunga mkono juhudi za raisi Magufuli, wangeweza kumuunga mkono kwa juhudi anazozifanya raisi bila ya kuhama vyama, lakini kwa jinsi tulivyokuwa wadhaifu ndiyo maana hatuwezi kujenga upinzani madhubuti. Inavyoonyesha watanzania hawajali sana mambo ya siasa ndiyo maana ni watu wachache waliyoandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ukilinganisha na idadi ya watu wa Tanzania, elimu ya siasa na hata ya uraia ni tatizo kwa wananchi wengi, na hata hao wachache wenye ufahamu wa elimu hizo bado kuna changamoto za utekelezaji wa elimu hizo. Cha msingi watanzania waamke na wajiulize nini wanataka na wapi wanataka kwenda na nini ni vipaumbele vyao.
 
Nami namsubiri hapa
Sipingani na Kalamu1 kwenye mengi ya mabandiko yake, ila kiukweli sijawahi kupata maelezo yaliyoonyooka jinsi ya kuweza kuwafikia watu. Maelezo anayoyatoa mara zote kuhusu kufikia watu katika mazingira haya, huwa nayaita mazingaombwe. Huenda akakuambia ww, lakini mimi simwelewi kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nanye Go,
Siasa hazijazuiliwa bana; usiamini sana maneno hayo. Siasa zinafanyika na ni jambo baya kukubali kuwa siasa zimezuliwa. Sasa kama hakuna siasa uchaguzi utafanyikaje?
Makatazi ya kufanya siasa yapo na ushahidi upo. Zanzibar Maalim Seif alisababisha Naibu waziri wa mambo ya ndani , Masauni kumuagiza IGP kumchukulia hatua RPC wa mkoa wa Pemba kwa kushindwa kudhibiti mikutano ya Maalim Seif.

Kule Hai hata KUB na mwenyekiti wa CHADEMA taifa kaamriwa kuongelea mambo ya Hai tu, siyo ya Tanzania nzima.

Tumemuona Bashiru na wenzake ccm wakichanja mbuga kila kona ya Tanzania,
Kwangu Lugola waziri wa mambo ya ndani alisema washughulikiwe bila huruma wote watakao bainika kufanya siasa wakati wakifahamu mikutano ya siasa imezuiliwa lakini hatujasikia Polepole na Bashiru wakishughulikiwa.

List ni ndefu, unataka nikuamini wewe?! Vipi hawa viongozi wenye dhamana?!

Labda ulitaka kusema, siasa za ccm hazijazuiliwa, lakini tutachaguaje ikiwa ccm pekee ndiyo wanaweza kuruhusiwa kufanya siasa?!
 
Kalamu1,
Hivi, wakati wa Kikwete upinzani uliruhusiwa sana kufanya siasa bila vizingiti vyovyote? mbona siasa zilifanyika pamoja na songombingo zote za kisiasa?
Mzee Mwanakijiji, ukweli mbona uko wazi mkuu, tofauti ya kufanya siasa wakati wa Kikwete na wakati huu wa Magufuli.

Hili nalo kweli ni jambo la kupotezea muda kulijadili hapa? Hapana, tusipoteze muda.
 
Kalamu1,
..Magufuli amezuia vyama vyote vya upinzani kufanya siasa kwa miaka minne sasa. Na wakati wote huo yeye na chama chake wamekuwa wakifanya siasa bila vikwazo vyovyote vile.

..Sasa uchaguzi ukifanyika, na Magufuli akashinda, ushindi wake utakuwa halali kweli?

..Tuchukue mfano rahisi. Tuwe na timu A, timu B, na chama cha mpira.

..Halafu timu A na chama cha mpira wanashirikiana kuhujumu timu B ikiwemo kuizuia kufanya mazoezi.

..Sasa hizi timu mbili zikija kucheza, na timu A ikashinda, je ushindi huo utakubalika kuwa ni halali na wa haki?
JokaaKuu, yote hayo ya Kampeni za kudumu zilizofanywa na Magufuli huku akiwazuia wapinzani wake hata kule kuitisha tu mikutano ya hadhara ili wazungumze na wanachama wao.

Kama Magufuli anajiamini kwamba Kampeni alizofanya zimemsaidia, aachane na kuvuruga kura wakati wa uchaguzi; wananchi wachague kwa utashi wao wenyewe.

Kama kampeni zake alizofanya zimewakoga nyoyo, si watamchagua yeye? Hofu ya kuingilia na kuvuruga kura za wananchi anazitoa wapi tena.

Hilo la Kampeni sasa ni historia, hatuwezi tena kurudi nyuma. Aachie timu B nao sasa wajifue ipasavyo kabla ya kuingia uwanjani, na uwanja uwe sawa pande zote mbili.

Hili ndilo lililo mhimu, na anajua hawezi kuruhusu iwe hivyo kwa hofu kubwa aliyonayo.

Ataanguka vibaya sana!
 
85%+ inamhusu Rais Magufuli, hakamatiki na sioni wa kupambana naye,time will tell.
Hana wa kushindana nae kwanini?
1. ndani ya chama kuna watu watashindana nae
2. tume ya uchaguzi sio huru
3. sio mwanasiasa ni mbabe
 
JokaKuu, mojawapo ya mambo mabaya sana ambayo yametokea na yanaendelea kutokea ni hii imani kuwa migogoro ya kisiasa mwisho wake ni ubaya tu. Demokrasia hujengwa kwa migogoro, kupingana na wakati mwingine huokolewa kwa jasho na damu. Hakuna nchi iliyojenga demokrasia ya kweli bila mivutano, misuguano, na hata minyukano. Sasa minyukano si lazima kwa demokrasia, lakini mivutano ni lazima. Tusiogope hii mivutano vinginevyo itakuwa ni kujaribu kuahirisha kisichoepukika. Hofu yangu tunajaribu kuchelewesha kinachotakiwa kufanyika.
You earn a lot of respects when you stand in these profoundly true lines.

What makes you vacillate?
 
Mwaka 2020 ni mwaka wa kufanya uamuzi kuhusiana na utawala na mwelekeo wa taifa letu. Huu ni mwaka wa Uchaguzi Mkuu, mwaka wa Uamuzi Mkuu. Watanzania wataitwa kutoa jibu la maswali makubwa mawili. Je, tuendelee na Rais yule yule aliyechaguliwa mwaka 2015 au tufikirie mtu mwingine? Na pili, Je tuendelee na wabunge wale wale waliochaguliwa 2015 au tufikirie kundi jipya la wabunge. Katika maswali hayo mawili ndani yake kuna maswali makubwa mawili yanayoendana nayo. Kwanza, je, Rais kutoka Chama cha Mapinduzi apewe nafasi nyingine ya kuongoza taifa na pili, je Bunge linalotakana na wabunge wengi wa Chama cha Mapinduzi lirudi tena kama lilivyo au tufikirie chama kingine?

Maswali haya yote mawili yana umuhimu wa kipekee kwenye mwaka huu wa 2020. Ni nafasi kwa Watanzania kuamua kuthibitisha maamuzi yao ya 2015 au kuyatengua; kuwathibitisha tena kwenye nafasi zao viongozi wetu ama kuwatumbua. Kwa vile madaraka ya kutawala yanatoka kwa wananchi basi ni wananchi ndio wenye uamuzi wa mwisho; siyo polisi, siyo usalama wa taifa, siyo wahisani, siyo vyama vya siasa; ni wapiga kura. Hivyo, wapiga kura katika mwaka huu wanaitwa kufanya uamuzi mkubwa na kila kura itakuwa na thamani yake.

Ili wapiga kura wetu wafikie uamuzi sahihi ni lazima wawe huru kufikia uamuzi huo. Hii ina maana ya kuwa mbinu au kitu chochote kikifanywa ama na chama, vyama au dola kujaribu kuzuia wananchi kufikia uamuzi huo basi kutatia doa maana nzima ya uchaguzi. Ni kwa sababu hiyo, viongozi wote – kuanzia Rais hadi wabunge yawapasa kutambua kuwa hawana sababu ya kuwaogopa wapiga kura. Kama mwaka 2015 watu walienda na kujinadi mbele ya wapiga kura na wananchi wakawakubali basi ni wazi hakuna sababu ya kuwaogopa wananchi hao tena mwaka 2020. Ni muhimu sana kila anayechaguliwa ajijue na aonekane amechaguliwa na wananchi kweli kweli.

Kwa sababu hiyo basi mwaka huu Tume ya Taifa ya Uchaguzi na vyombo vingine vyote vinavyohusika na mchakato wa kuhakikisha uwazi, usawa na haki katika uchaguzi mkuu vinatekeleza majukumu yao kwa weledi uliopitiliza. Hii ina maana ya kutovumulia vitendo vya uvunjifu wa taratibu, upendeleo, ukandamizaji au uminyaji wa wapiga kura. Kama hili halitatokea, ni kweli tunaweza kuwapata washindi, tunaweza kupata watu watakaoitwa wamechaguliwa lakini watu watakuwa na minong’ono ya kuwa “hawakushinda bali walishindishwa”. Ni muhimu anayeshinda ajulikane ameshinda kweli kweli.

Hata hivyo, ni muhimu pia kujua kuwa demokrasia siyo kushinda tu; na si kweli kuwa demokrasia inakuwepo wakati wa kushinda tu bali pia ni kujua demokrasia ni pamoja na kushindwa. Ni lazima mifumo yetu ihakikishe kuwa mtu anaposhindwa ameshindwa kihalali na kutoa nafasi kwa watu hao au mtu huyo kukiri kushindwa (concede defeat). Swali kubwa la mwaka huu basi haliko katika kushinda tu bali pia katika kushindwa; tumekuwa na shida sana kwa watu kukubali kushindwa na wakati mwingine watu kulazimisha kushinda kana kwamba, wameumbwa kushinda! Tanzania ni ya Watanzania wote, na hata wale walioshindwa nao ni Watanzania na hata wale ambao walikuwa wameshinda 2015 lakini wakajikuta wanashindwa 2020 kujua kuwa nao ni Watanzania. Kushindwa hakumuondolei mtu Utanzania wake, na kushinda hakumfanyi mwingine kuwa Mtanzania zaidi kuliko wengine.

Hivyo, basi tunapoingia taratibu na kwa matumaini mwaka huu wa Uchaguzi Mkuu 2020 napenda kuwatakia wote kheri na fanaka na baraka kwa wale wote ambao wataitwa kulitumikia taifa letu kwa miaka mitano mingine ijayo. Wale ambao tutasimama kama wagombea, na wale ambao tutawapigia kura wagombea hao sote tutimize wajibu wetu ili kuhakikisha kuwa mwisho wa siku bado Tanzania Moja yenye hatima moja inaendelea kusonga mbele.

Kheri ya Mwaka Mpya – Tukutane Kampeni 2020.

MMM

Januari 1, 2020.
Kwenye tume huru ya Uchaguzi na vyombo vya dola vikiwa pembeni Magufuli hawezi kushinda hata akishindanishwa na Bata.
 
Kiranga, hili ni suala la strategy; what should they do? fight a losing battle, or fight a battle that they could win or even draw?
How do you define losing?

If the opposition increases its vote in parliament and the percentages of votes against Magufuli, relative to the last election, that is not losing, that is gradual winning.

Complaining about 2025 constitutional violations by "president Magufuli" when we haven't even voted him for the presidency in 2020 is sending a psychological message that the opposition considers the presidency a lost cause.

If you want to fight a battle you could win or draw, you don't start with a message that will demoralize your soldiers, proclaiming imminent defeat.

Yani kwetu ni vituko kuanzia serikalini mpaka upinzani.
 
Kiranga, hili ni suala la strategy; what should they do? fight a losing battle, or fight a battle that they could win or even draw?
Siku upinzani ukishika nchi CCM ndio ita define kwamba what it did to oposition was right or wrong.
 
Mwaka 2020 ni mwaka wa kufanya uamuzi kuhusiana na utawala na mwelekeo wa taifa letu. Huu ni mwaka wa Uchaguzi Mkuu, mwaka wa Uamuzi Mkuu. Watanzania wataitwa kutoa jibu la maswali makubwa mawili. Je, tuendelee na Rais yule yule aliyechaguliwa mwaka 2015 au tufikirie mtu mwingine? Na pili, Je tuendelee na wabunge wale wale waliochaguliwa 2015 au tufikirie kundi jipya la wabunge. Katika maswali hayo mawili ndani yake kuna maswali makubwa mawili yanayoendana nayo. Kwanza, je, Rais kutoka Chama cha Mapinduzi apewe nafasi nyingine ya kuongoza taifa na pili, je Bunge linalotakana na wabunge wengi wa Chama cha Mapinduzi lirudi tena kama lilivyo au tufikirie chama kingine?

Maswali haya yote mawili yana umuhimu wa kipekee kwenye mwaka huu wa 2020. Ni nafasi kwa Watanzania kuamua kuthibitisha maamuzi yao ya 2015 au kuyatengua; kuwathibitisha tena kwenye nafasi zao viongozi wetu ama kuwatumbua. Kwa vile madaraka ya kutawala yanatoka kwa wananchi basi ni wananchi ndio wenye uamuzi wa mwisho; siyo polisi, siyo usalama wa taifa, siyo wahisani, siyo vyama vya siasa; ni wapiga kura. Hivyo, wapiga kura katika mwaka huu wanaitwa kufanya uamuzi mkubwa na kila kura itakuwa na thamani yake.

Ili wapiga kura wetu wafikie uamuzi sahihi ni lazima wawe huru kufikia uamuzi huo. Hii ina maana ya kuwa mbinu au kitu chochote kikifanywa ama na chama, vyama au dola kujaribu kuzuia wananchi kufikia uamuzi huo basi kutatia doa maana nzima ya uchaguzi. Ni kwa sababu hiyo, viongozi wote – kuanzia Rais hadi wabunge yawapasa kutambua kuwa hawana sababu ya kuwaogopa wapiga kura. Kama mwaka 2015 watu walienda na kujinadi mbele ya wapiga kura na wananchi wakawakubali basi ni wazi hakuna sababu ya kuwaogopa wananchi hao tena mwaka 2020. Ni muhimu sana kila anayechaguliwa ajijue na aonekane amechaguliwa na wananchi kweli kweli.

Kwa sababu hiyo basi mwaka huu Tume ya Taifa ya Uchaguzi na vyombo vingine vyote vinavyohusika na mchakato wa kuhakikisha uwazi, usawa na haki katika uchaguzi mkuu vinatekeleza majukumu yao kwa weledi uliopitiliza. Hii ina maana ya kutovumulia vitendo vya uvunjifu wa taratibu, upendeleo, ukandamizaji au uminyaji wa wapiga kura. Kama hili halitatokea, ni kweli tunaweza kuwapata washindi, tunaweza kupata watu watakaoitwa wamechaguliwa lakini watu watakuwa na minong’ono ya kuwa “hawakushinda bali walishindishwa”. Ni muhimu anayeshinda ajulikane ameshinda kweli kweli.

Hata hivyo, ni muhimu pia kujua kuwa demokrasia siyo kushinda tu; na si kweli kuwa demokrasia inakuwepo wakati wa kushinda tu bali pia ni kujua demokrasia ni pamoja na kushindwa. Ni lazima mifumo yetu ihakikishe kuwa mtu anaposhindwa ameshindwa kihalali na kutoa nafasi kwa watu hao au mtu huyo kukiri kushindwa (concede defeat). Swali kubwa la mwaka huu basi haliko katika kushinda tu bali pia katika kushindwa; tumekuwa na shida sana kwa watu kukubali kushindwa na wakati mwingine watu kulazimisha kushinda kana kwamba, wameumbwa kushinda! Tanzania ni ya Watanzania wote, na hata wale walioshindwa nao ni Watanzania na hata wale ambao walikuwa wameshinda 2015 lakini wakajikuta wanashindwa 2020 kujua kuwa nao ni Watanzania. Kushindwa hakumuondolei mtu Utanzania wake, na kushinda hakumfanyi mwingine kuwa Mtanzania zaidi kuliko wengine.

Hivyo, basi tunapoingia taratibu na kwa matumaini mwaka huu wa Uchaguzi Mkuu 2020 napenda kuwatakia wote kheri na fanaka na baraka kwa wale wote ambao wataitwa kulitumikia taifa letu kwa miaka mitano mingine ijayo. Wale ambao tutasimama kama wagombea, na wale ambao tutawapigia kura wagombea hao sote tutimize wajibu wetu ili kuhakikisha kuwa mwisho wa siku bado Tanzania Moja yenye hatima moja inaendelea kusonga mbele.

Kheri ya Mwaka Mpya – Tukutane Kampeni 2020.

MMM

Januari 1, 2020.
Unaposema, je, tuendelee na Magu au la una maanisha kuna uchaguzi. Hivi kwako ni kweli kuna uchaguzi Tanzania siku hizi?
 
Back
Top Bottom