Uchaguzi 2020 Ni Mwaka wa Uchaguzi Mkuu 2020: Kuthibitisha au Kutengua Maamuzi ya 2015?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
1577913660336.png

Mwaka 2020 ni mwaka wa kufanya uamuzi kuhusiana na utawala na mwelekeo wa taifa letu. Huu ni mwaka wa Uchaguzi Mkuu, mwaka wa Uamuzi Mkuu. Watanzania wataitwa kutoa jibu la maswali makubwa mawili. Je, tuendelee na Rais yule yule aliyechaguliwa mwaka 2015 au tufikirie mtu mwingine? Na pili, Je tuendelee na wabunge wale wale waliochaguliwa 2015 au tufikirie kundi jipya la wabunge. Katika maswali hayo mawili ndani yake kuna maswali makubwa mawili yanayoendana nayo. Kwanza, je, Rais kutoka Chama cha Mapinduzi apewe nafasi nyingine ya kuongoza taifa na pili, je Bunge linalotakana na wabunge wengi wa Chama cha Mapinduzi lirudi tena kama lilivyo au tufikirie chama kingine?

Maswali haya yote mawili yana umuhimu wa kipekee kwenye mwaka huu wa 2020. Ni nafasi kwa Watanzania kuamua kuthibitisha maamuzi yao ya 2015 au kuyatengua; kuwathibitisha tena kwenye nafasi zao viongozi wetu ama kuwatumbua. Kwa vile madaraka ya kutawala yanatoka kwa wananchi basi ni wananchi ndio wenye uamuzi wa mwisho; siyo polisi, siyo usalama wa taifa, siyo wahisani, siyo vyama vya siasa; ni wapiga kura. Hivyo, wapiga kura katika mwaka huu wanaitwa kufanya uamuzi mkubwa na kila kura itakuwa na thamani yake.

Ili wapiga kura wetu wafikie uamuzi sahihi ni lazima wawe huru kufikia uamuzi huo. Hii ina maana ya kuwa mbinu au kitu chochote kikifanywa ama na chama, vyama au dola kujaribu kuzuia wananchi kufikia uamuzi huo basi kutatia doa maana nzima ya uchaguzi. Ni kwa sababu hiyo, viongozi wote – kuanzia Rais hadi wabunge yawapasa kutambua kuwa hawana sababu ya kuwaogopa wapiga kura. Kama mwaka 2015 watu walienda na kujinadi mbele ya wapiga kura na wananchi wakawakubali basi ni wazi hakuna sababu ya kuwaogopa wananchi hao tena mwaka 2020. Ni muhimu sana kila anayechaguliwa ajijue na aonekane amechaguliwa na wananchi kweli kweli.

Kwa sababu hiyo basi mwaka huu Tume ya Taifa ya Uchaguzi na vyombo vingine vyote vinavyohusika na mchakato wa kuhakikisha uwazi, usawa na haki katika uchaguzi mkuu vinatekeleza majukumu yao kwa weledi uliopitiliza. Hii ina maana ya kutovumulia vitendo vya uvunjifu wa taratibu, upendeleo, ukandamizaji au uminyaji wa wapiga kura. Kama hili halitatokea, ni kweli tunaweza kuwapata washindi, tunaweza kupata watu watakaoitwa wamechaguliwa lakini watu watakuwa na minong’ono ya kuwa “hawakushinda bali walishindishwa”. Ni muhimu anayeshinda ajulikane ameshinda kweli kweli.

Hata hivyo, ni muhimu pia kujua kuwa demokrasia siyo kushinda tu; na si kweli kuwa demokrasia inakuwepo wakati wa kushinda tu bali pia ni kujua demokrasia ni pamoja na kushindwa. Ni lazima mifumo yetu ihakikishe kuwa mtu anaposhindwa ameshindwa kihalali na kutoa nafasi kwa watu hao au mtu huyo kukiri kushindwa (concede defeat). Swali kubwa la mwaka huu basi haliko katika kushinda tu bali pia katika kushindwa; tumekuwa na shida sana kwa watu kukubali kushindwa na wakati mwingine watu kulazimisha kushinda kana kwamba, wameumbwa kushinda! Tanzania ni ya Watanzania wote, na hata wale walioshindwa nao ni Watanzania na hata wale ambao walikuwa wameshinda 2015 lakini wakajikuta wanashindwa 2020 kujua kuwa nao ni Watanzania. Kushindwa hakumuondolei mtu Utanzania wake, na kushinda hakumfanyi mwingine kuwa Mtanzania zaidi kuliko wengine.

Hivyo, basi tunapoingia taratibu na kwa matumaini mwaka huu wa Uchaguzi Mkuu 2020 napenda kuwatakia wote kheri na fanaka na baraka kwa wale wote ambao wataitwa kulitumikia taifa letu kwa miaka mitano mingine ijayo. Wale ambao tutasimama kama wagombea, na wale ambao tutawapigia kura wagombea hao sote tutimize wajibu wetu ili kuhakikisha kuwa mwisho wa siku bado Tanzania Moja yenye hatima moja inaendelea kusonga mbele.

Kheri ya Mwaka Mpya – Tukutane Kampeni 2020.

MMM

Januari 1, 2020.
 
Inaonekana kama the only mpiga kura ambaye haki zake za utu na za kisiasa zinaheshimiwa angalau kidogo ktk utawala huu ni yule "anayeunga mkono juhudi". Kwa wengine waliobaki unaweza jikuta hata "unapotea" kwa kutokuunga mkono juhudi. Hiyo tu ikupe picha kama uchaguzi wa mwaka huu utakuwa uchaguzi halisi au maigizo na vituko kama vile vilivyo jitokeza kwenye chaguzi za serikali za mitaa recently.
 
Ikiwa siasa zimezuiliwa, na uchaguzi una husu vyama vya siasa, sasa tutachaguaje ikiwa aliyebaki ulingoni ni mmoja peke yake?

Yeye anasema, anapenda wanasiasa wanaopanda jukwaani na kuanza kumsifu yeye, anawaita hao ni wastaarabu na anawapa vyeo huko kwenye chama chake. Lakini wanapotaja kasoro za utawala wake yeye anasema hao wanamtukana na anasema hao hata waruhusu ng'o kufanya siasa.

Kwa assessment kama hii utaona hatutakuwa na uchaguzi, maana vyama vyote vinavyomsifu vimesha sema havita simamisha mgombea wa nafasi ya urais.

Ikiwa ndivyo na vyama vyenye kumkosoa havitaruhusiwa, basi hii inatosha kusema hakutakuwa na uchaguzi mkuu 2020.
 
Maswali haya yote mawili yana umuhimu wa kipekee kwenye mwaka huu wa 2020. Ni nafasi kwa Watanzania kuamua kuthibitisha maamuzi yao ya 2015 au kuyatengua; kuwathibitisha tena kwenye nafasi zao viongozi wetu ama kuwatumbua. Kwa vile madaraka ya kutawala yanatoka kwa wananchi basi ni wananchi ndio wenye uamuzi wa mwisho; siyo polisi, siyo usalama wa taifa, siyo wahisani, siyo vyama vya siasa; ni wapiga kura. Hivyo, wapiga kura katika mwaka huu wanaitwa kufanya uamuzi mkubwa na kila kura itakuwa na thamani yake.
Helooo, sijafika huko chini, lakini nimefurahi sana kuisoma hii aya.

Mkuu Mzee Mwanakijiji, natumaini huko chini hukutibua tena uzuri wa maneno uliyoyaweka hapa. Ngoja nikamalizie...
 
Nanye Go,
Siasa hazijazuiliwa bana; usiamini sana maneno hayo. Siasa zinafanyika na ni jambo baya kukubali kuwa siasa zimezuliwa. Sasa kama hakuna siasa uchaguzi utafanyikaje?
 
Hivyo, basi tunapoingia taratibu na kwa matumaini mwaka huu wa Uchaguzi Mkuu 2020 napenda kuwatakia wote kheri na fanaka na baraka kwa wale wote ambao wataitwa kulitumikia taifa letu kwa miaka mitano mingine ijayo. Wale ambao tutasimama kama wagombea, na wale ambao tutawapigia kura wagombea hao sote tutimize wajibu wetu ili kuhakikisha kuwa mwisho wa siku bado Tanzania Moja yenye hatima moja inaendelea kusonga mbele.
Sina tofauti kabisa nawe kuhusu bandiko lako hili..., ila nikukumbushe tu mitego tayari ilishawekwa kuufanya uchaguzi huu usiwe wa huru na wa haki. Hata wewe hilo unalijua.

Ni juzi tu tumeona jinsi CCM walivyofurahia ushindi wa 98% katika serikali za mitaa.

Hapa tusijifanye hilo hatulikumbuki, lipo tayari, na mengine kama hilo yanafuata katika uchaguzi mkuu.

Lakini nisikulaumu wewe kwa mitego na matokeo hayo, bali nikulaumu kwa kutoyazungumzia, na kuonya juu yake katika bandiko zuri sana hili uliloweka hapa.

Ngoja nikupe ukweli wangu mweupe kabisa. Niamheshimu sana Rais Magufuli akiruhusu uchaguzi utokee katika hali kama ulivyoieleza hapa.
Na akishinda uchaguzi huo hata kama ni kwa kura moja tu, heshima zangu zote ni kwake kwa kuwapa waTanzania HAKI yao ya msingi ya kuwachagua viongozi wao wanaowataka wawaongoze.

Na hata akishindwa uchaguzi huo katika hali ya namna hiyo, bado heshima kubwa ataistahiri na kuwaomba walioguswa na misukosuko katika miaka yake hii wasamehe machungu yaliyotokea.
 
Siasa hazijazuiliwa bana; usiamini sana maneno hayo. Siasa zinafanyika na ni jambo baya kukubali kuwa siasa zimezuliwa. Sasa kama hakuna siasa uchaguzi utafanyikaje?
Nakubaliana nawe kwa maana ya kwamba vyama vya upinzani hawajazuiwa kuwatafuta wanachama wapya na kujitangaza kwa njia mbalimbali isipokuwa ya mikutano ya hadhara kitaifa.
Lakini kuna matukio huko mikoani ya wakuu wa mikoa na Wilaya walivyokuwa wanawawekea vizingiti wapinzani,; ushahidi huo upo mwingi tu!

Wakati hayo yakitokea, CCM, na hasa Mwenyekiti wake na Katibu wamekuwa kazini siku zote na kuhodhi vyombo vya habari ili viwatangaze wao tu. TBC imesahau kabisa kwamba hiyo ni mali ya waTanzania wote.

Tusibeze juhudi zilizofanyika hadi sasa katika kutafuta njia za kuwadhoofisha wapinzani kwa njia mbalimbali. Lakini nakubali kwamba walitakiwa watafute njia mbadala ambazo bado zipo za kuwafikia wananchi na kufanya siasa zao.
 
Kalamu1,
Hivi, wakati wa Kikwete upinzani uliruhusiwa sana kufanya siasa bila vizingiti vyovyote? mbona siasa zilifanyika pamoja na songombingo zote za kisiasa?
 
Kalamu1,
..Magufuli amezuia vyama vyote vya upinzani kufanya siasa kwa miaka minne sasa. Na wakati wote huo yeye na chama chake wamekuwa wakifanya siasa bila vikwazo vyovyote vile.

..Sasa uchaguzi ukifanyika, na Magufuli akashinda, ushindi wake utakuwa halali kweli?

..Tuchukue mfano rahisi. Tuwe na timu A, timu B, na chama cha mpira.

..Halafu timu A na chama cha mpira wanashirikiana kuhujumu timu B ikiwemo kuizuia kufanya mazoezi.

..Sasa hizi timu mbili zikija kucheza, na timu A ikashinda, je ushindi huo utakubalika kuwa ni halali na wa haki?
 
Wapinzani wa Magufuli na CCM walipoanza kulalamika kuhusu Magufuli kuvunja katiba 2025, nikajua kwamba washakubali kwamba wameanza kukubali kushindwa 2020.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kiranga, hili ni suala la strategy; what should they do? fight a losing battle, or fight a battle that they could win or even draw?
 
Hivi, wakati wa Kikwete upinzani uliruhusiwa sana kufanya siasa bila vizingiti vyovyote? mbona siasa zilifanyika pamoja na songombingo zote za kisiasa?

..but why should we have songombingo ktk siasa zetu?

..Na songombingo zenyewe ni za ccm na dola kuwadhulumu wapinzani.

..kama tunataka songombingo ziwe sehemu ya siasa zetu basi kuwe na haki sawa ktk kufanya songombingo.

..lakini mimi sidhani kama tukiruhusu hilo nchi hii itakuwa salama.

..Vita vya wenyewe kwa wenyewe mara nyingi chanzo chake ni watawala wanaofanya songombingo.

..Mauaji ya kimbari ya Rwanda yalipangwa na chama tawala cha nchi hiyo, na yalitekelezwa na umoja wa vijana wa chama tawala cha Rwanda.

..Watanzania tuwe makini na CCM. Kwangu mimi inaonekana kila awamu wanazidisha UKATILI na sijui mwisho wake ni nini.
 
..Watanzania tuwe makini na CCM. Kwangu mimi inaonekana kila awamu wanazidisha UKATILI na sijui mwisho wake ni nini.

JokaKuu, mojawapo ya mambo mabaya sana ambayo yametokea na yanaendelea kutokea ni hii imani kuwa migogoro ya kisiasa mwisho wake ni ubaya tu. Demokrasia hujengwa kwa migogoro, kupingana na wakati mwingine huokolewa kwa jasho na damu. Hakuna nchi iliyojenga demokrasia ya kweli bila mivutano, misuguano, na hata minyukano. Sasa minyukano si lazima kwa demokrasia, lakini mivutano ni lazima. Tusiogope hii mivutano vinginevyo itakuwa ni kujaribu kuahirisha kisichoepukika. Hofu yangu tunajaribu kuchelewesha kinachotakiwa kufanyika.
 
JokaKuu, mojawapo ya mambo mabaya sana ambayo yametokea na yanaendelea kutokea ni hii imani kuwa migogoro ya kisiasa mwisho wake ni ubaya tu. Demokrasia hujengwa kwa migogoro, kupingana na wakati mwingine huokolewa kwa jasho na damu. Hakuna nchi iliyojenga demokrasia ya kweli bila mivutano, misuguano, na hata minyukano. Sasa minyukano si lazima kwa demokrasia, lakini mivutano ni lazima. Tusiogope hii mivutano vinginevyo itakuwa ni kujaribu kuahirisha kisichoepukika. Hofu yangu tunajaribu kuchelewesha kinachotakiwa kufanyika.

..mnadhimu mkuu wa kambi ya upinzani kupigwa risasi 16 ktk eneo ambalo kwa kawaida lina walinzi wa serikali hiyo unaita ni mivutano na minyukano?

..na kwanini jasho na damu iwe kwa upande wa upinzani tu?

..mimi bwana SIUNGI MKONO dhuluma au ukatili wa aina yoyote ile ktk siasa zetu.

..kama ni minyukano basi iwe minyukano ya HOJA au SERA, lakini siyo minyukano ya KIJINAI,au KIGAIDI.

..kama wazee wetu walipata UHURU bila kumwaga DAMU, kwanini sisi watoto wao, au wajukuu wao, tumwage damu kwa ajili ya demokrasia.
 
Back
Top Bottom