Steve Dii
JF-Expert Member
- Jun 25, 2007
- 6,402
- 1,254
Vijana waliojitokeza kugombea nafasi za ubunge na uongozi katika ngazi nyinginezo kwa tiketi ya CCM ni wengi na wanazidi kuongezeka. Wengi wa vijana hawa ni wasomi na wenye shahada za juu kielimu, na baadhi yao wamebahatika kuishi nchi mbalimbali za ng'ambo na kujionea yaliyoko huko.
Hatua wanazochukua kufanya hivyo ni haki yao na ni jambo la kupongezwa pale ambapo nia na malengo ni maendeleo ya Taifa letu. Lakini kwa kuwa wengi wao ni vijana walio elimika (nakujua vyanzo vya matatizo yetu), inakuwakuwaje wanagombea kupitia CCM? Nasema hivi kwani kitu kimojawapo ninachoamini kuwa ni kikwazo katika kuleta kasi ya maendeleo ya Taifa letu ndani ya mfumo wa vyama vingi ni kutokuwepo kwa uwakilishi wa kutosha wa upinzani, haswa katika ngazi ya ubunge.
Basi nauliza:
--- wakiwa ni vijana wasomi, nini kinawafanya waende CCM hali chama hicho kina wabunge wengi tayari tena wanaozidi wapinzani maradufu?
--- je, hawaamini kuwa kuendeleza upinzani ni jambo la msingi kwa maendeleo ya Taifa letu?
--- ni nini ambacho wanaweza kubadilisha wakiwa ndani ya CCM ambacho imeshindwa kukifanya mpaka leo hii kama chama tawala?
--- wanahofia nini kuingia upinzani na kuundeleza wakiwa kama vijana wenye lengo la kuendeleza Taifa hili kwa nia njema kabisa huku wakiujenga mfumo wa vyama vingi?
---
Steve Dii
Hatua wanazochukua kufanya hivyo ni haki yao na ni jambo la kupongezwa pale ambapo nia na malengo ni maendeleo ya Taifa letu. Lakini kwa kuwa wengi wao ni vijana walio elimika (nakujua vyanzo vya matatizo yetu), inakuwakuwaje wanagombea kupitia CCM? Nasema hivi kwani kitu kimojawapo ninachoamini kuwa ni kikwazo katika kuleta kasi ya maendeleo ya Taifa letu ndani ya mfumo wa vyama vingi ni kutokuwepo kwa uwakilishi wa kutosha wa upinzani, haswa katika ngazi ya ubunge.
Basi nauliza:
--- wakiwa ni vijana wasomi, nini kinawafanya waende CCM hali chama hicho kina wabunge wengi tayari tena wanaozidi wapinzani maradufu?
--- je, hawaamini kuwa kuendeleza upinzani ni jambo la msingi kwa maendeleo ya Taifa letu?
--- ni nini ambacho wanaweza kubadilisha wakiwa ndani ya CCM ambacho imeshindwa kukifanya mpaka leo hii kama chama tawala?
--- wanahofia nini kuingia upinzani na kuundeleza wakiwa kama vijana wenye lengo la kuendeleza Taifa hili kwa nia njema kabisa huku wakiujenga mfumo wa vyama vingi?
---
Steve Dii