Ni mradi upi ungerudisha mtaji wa uwekezaji kwa TPDC?

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Jul 7, 2020
6,316
8,227
Mada: Ni mradi upi ungerudisha mtaji wa uwekezaji kwa TPDC kwa haraka zaidi

Habari za leo wa kuu,

Mimi ni kijana wenu, leo nimekuja na mada hii yenye tija kwa taifa.

Taifa letu linayo gesi asilia ambayo, ina matumizi mengi

1. Gesi asilia inatumika kupikia majumbani
2. Gesi asilia inatumika kutengenezea mbolea zinazotumika kwenye kilimo. Mbolea zote tunazo agiza nje ya nchi zinatengenezwa kwa kutumia gesi asilia.
Sitaweza kuelezea kanuni zinatumika hapa ila ukitaka kujua zaidi waweza kuni PM kwasababu hivi ndio vitu navyo shinda navyo.
3. Lakini pia gesi asilia inatumika kutengenezea mafuta safi ya petrol na diesel ukiachana na haya yanayopatika kwa kuitenganisha mafuta ghafi.
4. N. k

Kwa analysis za kiuchumi nilizo fanya, Miradi miwili huo wa kutengeneza mbolea na wa kusambaza gesi majumbani inaweza kufanywa na serikali yetu bila kushirikiana na kampuni za nje (Joint venture ama sharing agreement).

Nimezungumza hivi ili niitoe Liquified Natural Gas Project (LNG) ambao ni mradi wenye tija zaidi ila unahitaji mtaji mkubwa kuwekeza. Hivyo lazima serikali ishirikiane na kampuni za nje ili kuwekeza mradi huu.

Basi nikirudi kwenye maada tajwa pale juu. Wote tunajua idadi ya watu Tanzania inayo weza kumudu kununua gesi asilia ni kubwa. Tatizo linalo kuja gesi asilia inahitaji uwekezaji mkubwa wa bomba za kuwasambazia wateja waliopo mikoani. Hivyo basi swala hilo kiukweli huchukua muda kujenga miundo mbinu ya kusafirishia hiyo gesi.

Kwenye swala la mbolea, nako pia wote tunajua kwamba kilimo ndio uti wa mgongo wa taifa letu na mtanzania yeyote yule hata maskini anajua kwamba ili aweze kulima kilimo Bora kitacho mpatia mazao mengi na Bora anahitaji mbolea. Hivyo mbolea inatumika mahali pote Tanzania, hata watu maskini kabisa nao pia hutumia mbolea.

Hivyo mbolea ikitengenezwa Tanzania ninao uhakika kwamba itaweza kununuliwa na asilimia kubwa ya Watanzania.

Faida moja kubwa ya kuwa na kiwanda cha kutengeneza mbolea Tanzania
1. Tutaondoa adhaa ya kuagiza mbolea kutoka nje ya nchi, hii inasaidia kupanda kwa uchumi wa nchi
2. Zipo faida nyingi ila mimi nime egemea kwenye hiyo ya kwanza.

Swali:
1. Je, ni mradi upi wenye tija ya haraka kwa serikali na wananchi?

2. Ni mradi upi ungerudisha mtaji wa uwekezaji kwa TPDC kwa haraka zaidi

Msisahau kwamba Miradi mingi ya mafuta na gesi huchukua muda mrefu sana kuanza kuleta faida. Hivyo ili urudishe gharama ulizo tumia kuwekeza inabidi uwe na soko imara na la uhakika.

Ni mimi: Meneja wa makampuni
Elimu: Bachelor of Science in Oil and Gas Chemistry
University: Aberdeen University
 
hapo ni kufanya utafit kidogo ili jibubliwe na tija.

Tungejiuliza sisi kama nchi tuna import Mbolea kiasi gani kwa mwaka na kwa gharama ipo na kwa gesi tunaimport volume ipi kwa kiasi gani cha fedha

tukishapata Jubu tuchukue Bithaa yenye import cost kubwa kisha tuzalishe nchini ili tuokoe fedha ambayo ingekwenda Nje
 
hivi kuna lile gorofa walilo nyang'anywa TPDC na 'wajanja' wa mujini pale posta mpya, nadhani huu ungekuwa wakati muafaka kwa TPDC kulidai kwani hiki kingekuwa kitega uchumi kizuri tuu.

Vile vile hawa jamaa wangejikita kwenye utafiti wa gas, petroleum na hata kuwa na hata kuwa na geo-database zitakazo wawezesha kuzaa data kwa makampuni ya mafuta na gas, nadhani mambo hayo yanaweza watoa zaidi, yaani wanahitaji ubunifu zaidi na kuwa 'modernized' ili waweze ku- deliver zaidi, haiingi akilini kusema nchi hii haina deposits za mafuta wakati maeneo mengi tuu hayaja fanyiwa utafiti wa mafuta wa kina na wakutosha, na kimsingi taasisi inayopaswa kufanya tafiti hizi ni TPDC .....
 
Mada: Ni mradi upi ungerudisha mtaji wa uwekezaji kwa TPDC kwa haraka zaidi

Habari za leo wa kuu,
Mimi ni kijana wenu, leo nimekuja na mada hii yenye tija kwa taifa.

Taifa letu linayo gesi asilia ambayo, Ina matumizi mengi
1. Gesi asilia inatumika kupikia majumbani
2. Gesi asilia inatumika kutengenezea mbolea zinazotumika kwenye kilimo.
Mbolea zote tunazo agiza nje ya nchi zinatengenezwa kwa kutumia gesi asilia.
Sitaweza kuelezea kanuni zinatumika hapa ila ukitaka kujua zaidi waweza kuni PM kwasababu hivi ndio vitu navyo shinda navyo.
3. Lakini pia gesi asilia inatumika kutengenezea mafuta safi ya petrol na diesel ukiachana na haya yanayopatika kwa kuitenganisha mafuta ghafi.
4. N. k

Kwa analysis za kiuchumi nilizo fanya, Miradi miwili huo wa kutengeneza mbolea na wa kusambaza gesi majumbani inaweza kufanywa na serikali yetu bila kushirikiana na kampuni za nje (Joint venture ama sharing agreement).

Nimezungumza hivi ili niitoe Liquified Natural Gas Project (LNG) ambao ni mradi wenye tija zaidi ila unahitaji mtaji mkubwa kuwekeza. Hivyo lazima serikali ishirikiane na kampuni za nje ili kuwekeza mradi huu.

Basi nikirudi kwenye maada tajwa pale juu. Wote tunajua idadi ya watu Tanzania inayo weza kumudu kununua gesi asilia ni kubwa. Tatizo linalo kuja gesi asilia inahitaji uwekezaji mkubwa wa bomba za kuwasambazia wateja waliopo mikoani. Hivyo basi swala hilo kiukweli huchukua muda kujenga miundo mbinu ya kusafirishia hiyo gesi.

Kwenye swala la mbolea, nako pia wote tunajua kwamba kilimo ndio uti wa mgongo wa taifa letu na mtanzania yeyote yule hata maskini anajua kwamba ili aweze kulima kilimo Bora kitacho mpatia mazao mengi na Bora anahitaji mbolea. Hivyo mbolea inatumika mahali pote Tanzania, hata watu maskini kabisa nao pia hutumia mbolea.
Hivyo mbolea ikitengenezwa Tanzania ninao uhakika kwamba itaweza kununuliwa na asilimia kubwa ya Watanzania.

Faida moja kubwa ya kuwa na kiwanda cha kutengeneza mbolea Tanzania.
1. Tutaondoa adhaa ya kuagiza mbolea kutoka nje ya nchi, hii inasaidia kupanda kwa uchumi wa nchi
2. Zipo faida nyingi ila mimi nime egemea kwenye hiyo ya kwanza.

Swali:
1. Je Ni mradi upi wenye tija ya haraka kwa serikali na wananchi?

2. Ni mradi upi ungerudisha mtaji wa uwekezaji kwa TPDC kwa haraka zaidi

Msisahau kwamba Miradi mingi ya mafuta na gesi huchukua muda mrefu sana kuanza kuleta faida. Hivyo ili urudishe gharama ulizo tumia kuwekeza inabidi uwe na soko imara na la uhakika.

Ni mimi: Meneja wa makampuni
Elimu: Bachelor of Science in Oil and Gas Chemistry
University: Aberdeen University
Mkuu si wameamua kufungua Vituo vya Mafuta na Kimoja kimeshafunguliwa na Waziri kule Mara sasa hata vituo Viwili hamjafikisha unakuja kutafuta wazo mbadala tena.
 
Mkuu si wameamua kufungua Vituo vya Mafuta na Kimoja kimeshafunguliwa na Waziri kule Mara sasa hata vituo Viwili hamjafikisha unakuja kutafuta wazo mbadala tena.
Yeah ni kweli, TPDC wana miradi mingi ambayo inaendelea mpaka sasa.
 
hivi kuna lile gorofa walilo nyang'anywa TPDC na 'wajanja' wa mujini pale posta mpya, nadhani huu ungekuwa wakati muafaka kwa TPDC kulidai kwani hiki kingekuwa kitega uchumi kizuri tuu.

Vile vile hawa jamaa wangejikita kwenye utafiti wa gas, petroleum na hata kuwa na hata kuwa na geo-database zitakazo wawezesha kuzaa data kwa makampuni ya mafuta na gas, nadhani mambo hayo yanaweza watoa zaidi, yaani wanahitaji ubunifu zaidi na kuwa 'modernized' ili waweze ku- deliver zaidi, haiingi akilini kusema nchi hii haina deposits za mafuta wakati maeneo mengi tuu hayaja fanyiwa utafiti wa mafuta wa kina na wakutosha, na kimsingi taasisi inayopaswa kufanya tafiti hizi ni TPDC .....
Tatizo lao kubwa hawana mtaji wa kufanya hizo biashara.
 
hapo ni kufanya utafit kidogo ili jibubliwe na tija.

Tungejiuliza sisi kama nchi tuna import Mbolea kiasi gani kwa mwaka na kwa gharama ipo na kwa gesi tunaimport volume ipi kwa kiasi gani cha fedha

tukishapata Jubu tuchukue Bithaa yenye import cost kubwa kisha tuzalishe nchini ili tuokoe fedha ambayo ingekwenda Nje
Yeah, ni kweli. Lakini nikifikiria tu naweza kusema taifa letu lina import mbolea nyingi sana aise.
 
hapo ni kufanya utafit kidogo ili jibubliwe na tija.

Tungejiuliza sisi kama nchi tuna import Mbolea kiasi gani kwa mwaka na kwa gharama ipo na kwa gesi tunaimport volume ipi kwa kiasi gani cha fedha

tukishapata Jubu tuchukue Bithaa yenye import cost kubwa kisha tuzalishe nchini ili tuokoe fedha ambayo ingekwenda Nje
Alafu pia gesi hatu import, ipo ndani ya nchi
 
Gesi inayotumika kutengenezea mbolea tunayo nchini, inazalishwa mtwala. Inaitwa methane (natural gas)

Ile tunayo agiza ni ya kupikia, inaitwa liquified petroleum gas (LPG) ina mchanganyiko wa propane and butane. Hiyo haitumiki kutengenezea mbolea.

Kuliko gesi???? Mbolea nyingi kwa ajili ya kilimo, je secta ya kilimo imefika wapi nchi hiii
 
Kuliko gesi???? Mbolea nyingi kwa ajili ya kilimo, je secta ya kilimo imefika wapi nchi hiii
Pamoja na kwamba mbolea huagizwa kwa wingi lakn sina hakika kama huwa inatoshereza. Ila ukumbuke watu wengine hushindwa kutumia mbolea kwasababu hawana pesa za kununulia mbolea.
 
Waende wakajifunze kwa Saudi Aramco pale Saudia, Petronas Malysia au Patrobas ya Brazil.. Dunia ya sasa hupashwi kuumiza kichwa sana maana tayari kila kitu kipo ni yeye kustudy na kuimplement kwenye maeneo yako..

Tayari tuna gas ya kutosha ardhini as per exploration done, tayari data zipo sijui tunalalala nini... Watu wako maabara daily wanatafuta mbadala wa kila kitu duniani hapa na unaweza kushtuka ukakuta tayari gas sio dili tena bali dili ni jua, upepo na maji ambavyo kila mtu anavyo.. Akili ni nywele na kila mtu ana zake..yaani unagas ujazo wa trilioni kazaa ardhini halafu unashangaashangaa tu baada ya kutoboa mwamba na kuanza kusupply gas kila mahala inapohitajika..

TPDC wanaweza kutafuta muwekezaji akajenga LNG plant pale Ljndi immeadiately wao wakaweka shares kadhaa pale sio free carried hapana waweke mzigo kama 40% + 20% za ardhi na muwekezaji abaki na 40% wamuachie akifanya operation zote then tunakutana kwenye mgao, au TPDC waweke mzigo lete Wanorway au warusi wajenge na operate mtambo ukiwalipa operation cost wao na contractor wao with 100% state own shares...
Jenga gas plant kubwa yenye capacity mpaka 5000MW itangazie dunia nauza umeme, pelekaa waya Rwanda, Malawi, Uganda na kila mahala kwa majirani hapo TPDC analipwa gas yake na Tanesco na tanesco anauza umeme wake...

Tuache usingizi wapono na kupiga kelele za siasa kila uchwao tufanye kazi, hamuwaoni warusi wanaisumbua west europe na gas yao, mkizingua tunafunga gate valve mnakufa na baridi huko...
 
Kuliko gesi???? Mbolea nyingi kwa ajili ya kilimo, je secta ya kilimo imefika wapi nchi hiii
Pamoja na kwamba mbolea huagizwa kwa wingi lakn sina hakika kama huwa inatoshereza. Ila ukumbuke watu wengine hushindwa kutumia mbolea kwasababu hawana pesa za kununulia mbolea.
 
Waende wakajifunze kwa Saudi Aramco pale Saudia, Petronas Malysia au Patrobas ya Brazil.. Dunia ya sasa hupashwi kuumiza kichwa sana maana tayari kila kitu kipo ni yeye kustudy na kuimplement kwenye maeneo yako..

Tayari tuna gas ya kutosha ardhini as per exploration done, tayari data zipo sijui tunalalala nini... Watu wako maabara daily wanatafuta mbadala wa kila kitu duniani hapa na unaweza kushtuka ukakuta tayari gas sio dili tena bali dili ni jua, upepo na maji ambavyo kila mtu anavyo.. Akili ni nywele na kila mtu ana zake..yaani unagas ujazo wa trilioni kazaa ardhini halafu unashangaashangaa tu baada ya kutoboa mwamba na kuanza kusupply gas kila mahala inapohitajika..

TPDC wanaweza kutafuta muwekezaji akajenga LNG plant pale Ljndi immeadiately wao wakaweka shares kadhaa pale sio free carried hapana waweke mzigo kama 40% + 20% za ardhi na muwekezaji abaki na 40% wamuachie akifanya operation zote then tunakutana kwenye mgao, au TPDC waweke mzigo lete Wanorway au warusi wajenge na operate mtambo ukiwalipa operation cost wao na contractor wao with 100% state own shares...
Jenga gas plant kubwa yenye capacity mpaka 5000MW itangazie dunia nauza umeme, pelekaa waya Rwanda, Malawi, Uganda na kila mahala kwa majirani hapo TPDC analipwa gas yake na Tanesco na tanesco anauza umeme wake...

Tuache usingizi wapono na kupiga kelele za siasa kila uchwao tufanye kazi, hamuwaoni warusi wanaisumbua west europe na gas yao, mkizingua tunafunga gate valve mnakufa na baridi huko...
Mawazo yako ni mazuri
 
Hii LPG ya Mihan, lake gase, Oryx tunaitoa wapi
LPG ni kifupisho cha Liqufied Petroleum Gas (LPG), ambao ni mchanganyiko wa gesi ya propane (CH[SUB]3[/SUB]CH[SUB]2[/SUB]CH[SUB]3[/SUB]) na gesi ya butane (CH[SUB]3[/SUB]CH[SUB]2[/SUB]CH[SUB]2[/SUB]CH[SUB]3[/SUB]). Mchanganyiko huo una contain propane (85%) na Butane (15%).

Asilimia kubwa ya LPG hupatikana baada ya kutenganisha mafuta ghafi (crude oil). Bidha ya kwanza kabisa wakati wa kutenganisha huwa ni LPG.

Lakini pia LPG nyingine hupatikana wakati wa kuchakata gesi asilia (Natural Gas) ambayo ina contain kiwango kikubwa cha propane na Butane.

Gesi yetu ya mtwala ni natural gas ina contain kiwango kikubwa cha gesi ya methane (CH[SUB]4[/SUB]) kwa 97%.
Hivyo hatuwezi kuzalisha LPG kutoka kwenye natural gas yetu inayochimbwa Tanzania.

Badala yake LPG yote inayo uzwa Tanzania inaagizwa kutoka nchi za nje.
 
LPG ni kifupisho cha Liqufied Petroleum Gas (LPG), ambao ni mchanganyiko wa gesi ya propane (CH[SUB]3[/SUB]CH[SUB]2[/SUB]CH[SUB]3[/SUB]) na gesi ya butane (CH[SUB]3[/SUB]CH[SUB]2[/SUB]CH[SUB]2[/SUB]CH[SUB]3[/SUB]). Mchanganyiko huo una contain propane (85%) na Butane (15%).

Asilimia kubwa ya LPG hupatikana baada ya kutenganisha mafuta ghafi (crude oil). Bidha ya kwanza kabisa wakati wa kutenganisha huwa ni LPG.

Lakini pia LPG nyingine hupatikana wakati wa kuchakata gesi asilia (Natural Gas) ambayo ina contain kiwango kikubwa cha propane na Butane.

Gesi yetu ya mtwala ni natural gas ina contain kiwango kikubwa cha gesi ya methane (CH[SUB]4[/SUB]) kwa 97%.
Hivyo hatuwezi kuzalisha LPG kutoka kwenye natural gas yetu inayochimbwa Tanzania.

Badala yake LPG yote inayo uzwa Tanzania inaagizwa kutoka nchi za nje.

Ndio maana nasema Kama tunaagiza LPG, hatuwez acha na tukatumia LNG badala yake
 
kusema eti TPDC wajikite kwenye kuuza mafuta, sijui kutengeneza mbolea etc ni kuwa 'under-utilize' kwa nguvu walinayo hawa wanatakiwa kujikita zaidi kwenye ku-explore petroleum & petroleum products kwenye ma-aquifer yaliyopo Rufiji delta, mabaharini, coastal region, lakes zones, etc.. hili la kusema kuwa hawana mtaji halikubaliki kwani hii ni taasisi ya serikali, wenzetu wa Brazili na Angola 'TPDC' zao zimewatoa kweli kweli, mara nyingine tukubali kujifunza njia walizo pitia adi kupata mafanikio, haingii akili kabisaa kwa 'Rufiji delta' kukosa mafuta au hata gesi ukweki ni kuwa hatuja fanya exploration za kutosha kwenye maeneo 'potential' mengi tuu yaliyopo nchini
 
Ndio maana nasema Kama tunaagiza LPG, hatuwez acha na tukatumia LNG badala yake
Yeah inawezekana LNG ina kazi nyingi sana kupikia, kuwashia, malighafi viwandani n.k

Changamoto za LNG
1. Inahitaji ujenzi wa kiwanda kikubwa pamoja na miundo mbinu ya gharama ili kuweza kuizalisha na kuisafirisha
2. Hatuwezi kujenga LNG kwa kutumia fedha za ndani Itakua ni hatari kiuchumi kwani tutatumia muda mrefu sana ili kuweza kurudisha gharama tutakazo tumia kujenga hicho kiwanda
mfano kwa ile gesi yetu ya, mtwala tunahitaji
$30bn ambazo ni sawa na Trilion 70 ili kujenga kiwanda ya LNG.
Hiyo pesa ni nyingi kuingiza kwenye biashara ni risk kwa nchi yetu.
 
Back
Top Bottom