witnessj
JF-Expert Member
- Mar 22, 2015
- 28,710
- 47,093
Ikawaje sasa mkuu??Nilimpenda binti mmoja hv basi nikawa na date nae basi siku akapata ajali ya Pikipiki jicho lake moja nusura litoke huku mazaake hana mpunga kwa dingi yake napo ndo hivyo walikuwa wameshaachana kitambo, basi nikapigiwa simu na rafiki yangu kuwa manzi kapata ajali na mazaake hana pesa za matibabu na wako hospitali, nikatoka home kwenda kumuangalia manzi pale hospitalini nimefika basi kumkuta manzi analia tu mazaake nae yupo tu hana ramani na matibabu bado kabisa, mwanaume nikaingia chumba cha daktari nikamuuliza huyu mgonjwa atapona kwa sh? Akajibu 20000 nikamcash palepale daktari. Akaanza matibabu pale akawa anaenda kuchoma sindano asubuhi na jioni, nilikuwa sijui akawa anaenda na mchana kumbe kuna kitu kipo nyuma ya pazia ambacho sikufahamu kumbe daktari alikuwa amemchumbia tayari na nyumbani kwao wakaelewana mahali, basi binti kwa wakati huo alikuwa ameshapona. Nyodo zikaanza na binti huyo akawa Haji kwangu na hata anaweza kushinda hayupo hata nyumbani kwao yupo kwa jamaa tu, muda huo hana kovu hata moja usoni, ikafikia hatua akawa anapita na huyo daktari wakiwa wameambatana kwa macho yangu hv naona yaani niliumia na sikuwahi kuwa na maumivu makali kiasi hicho before,,. Kumbe hata daktari mwenyewe alikuwa tapeli tu hakuna kitu. Hata hakumuoa kabisa na nikikumbuka hiki kitu kutoka moyoni nasema binti yeyote yule akiwa mbichi huwa wanajisikia saaana na tena saaana. Nakumbuka huu mkasa na nakumbuka msemo mmoja unasema, Usiheshimu kila kitu hapa duniani maana hata chumvi huonekana kama sukari.
Sent using Jamii Forums mobile app