Ni maadhimisho ya uhuru wa Tanganyika au Tanzania?

Mtego wa Noti

JF-Expert Member
Nov 27, 2010
2,591
1,599
Kwa sasa serikali imeshadadia sherehe za miaka 50 ya uhuru wa tanzania. ninachojua na wanachojua wote mnaosoma hii thread ni kuwa, Tanzania ni muungano wanchi mbili ambazo ni Tanganyika na Zanzibar ambao ulifanyika mwaka 1964.

Tanganyika ilipata uhuru mwaka 1961 na Zanzibar kama sikosei ni mwaka 1962 na mapinduzi yakafanyika mwaka 1964.

Hizi nchimbili yaani Tanganyika na Zanzibar ziliungana mwaka 1964, sasa kwa nini tusherehekee miaka 50 ya tanzania na wakati tanzania yenyewe bado haijafikisha miaka 50?

kilichofikisha miaka 50 ni tanganyika na siyo tanzania, kuna umuhimu gani kufenya hizi sherehe? Kwa maoni yangu, tanzania ilizaliwa mwaka 1964 baada ya muungano na siyo 1961.

Au ndio kusema wazanzibari siyo ishu kwa hiyo hata kabla hatujaungana walikuwani nndani ya Tanganyika?

Nomba msaada wenu, vinginevyo mimi naamini kuwa tanzania itakuwa na miaka 50 hapo mwaka 2014, hii kufanya sherehe kwa sasa ni kiherehere cha JK tu.

tujadiliane kuhusu hili.

Nawasilisha.....
 
au zenji siyo sehemu ya tanzania? au ndio maana jamaa wa zenji wanalalamika kuwa wameolewa na bara kwa hiyo ile tarehe yao haina ishu?
 
Back
Top Bottom