Ni mfumo upi mzuri wa kuacha matumizi nyumbani?

NI MTAZAMO TU

JF-Expert Member
Feb 20, 2014
1,203
998
WanaJF ninaleta kwenu iwe faida kwangu na kwa wadau wengine.

Wengi wetu tuna ndoa haijalishi mama ni mfanyakazi au lah ila majukumu ya familia yanamuhusu baba, kikubwa kilichozoeleka baba ndio mkuu wa nyumba.

Hoja yangu ni mfumo upi unapaswa kufuatwa katika kuacha matumizi ya ndani?

Namaanisha kuacha kila siku pesa ya matumizi; mfano, elfu kumi au tano kutegemea na kipato na ukubwa wa familia, au kumwachia mwanamke pesa ya mwezi mzima, ili ikiisha mwanaume atakuwa hapo hahusiki.

Nyumba nyingi zimeingia katika shida kubwa sana, mwanaume mwingine utasikia nilikuwa naacha pesa ya matumizi kwa mwezi, ila ikawa haifiki mwisho wa mwezi mwanamke anadai pesa imekwisha, na kumwingiza kwenye mipango mipya ya kutafuta pesa ili kuifikisha familia hiyo mwisho wa mwezi.

Na mwishoe kuepuka hilo wengine huamua kutoa pesa ya matumizi kwa kila mwezi kwa kupanga kiasi.. Wengine 5,000 , 10,000 kutegemea na kipato na ukubwa wa familia.

Naomba mchango wenu wadau. Wengine sisi wachanga kwenye ndoa tunahitaji kujuzwa na wazoefu.
 
Siku hizi mpango ni mmoja tu, mama anaandaa list ya vyakula vya mwezi esp visivyokuwa perishable mf mchele, unga, mafuta, maharage, sukari nk then mnaenda kununua vyote. Vile perishable mf nyama, nyanya, majani, matunda, maziwa fresh nk mtanunua vikihitajika, bajeti yake huwa sio kubwa. Kama ni familia ya watu 4, laki 3 inawatosha kabisa kwa kila kitu na hata chenji kubaki; kwa familia za kawaida.
 
Kawaida mnatakiwa mnunue unga mchele maharage mafuta nk muweke ndani

Then muende sokoni kununua vitu vya jumla kama nyanya (ndoo au kisado), vitunguu karoti nk

Kisha kama mwapenda samaki mnaweza kupita feri mkachukua wa kutoshA

Vitu vinginevidogo vidogo kama sabuni nk (ambavyo haviexpire mapema) mnaweza kununua vya jumla mkahifadhi

Baada ya hapo mkabidhi mkeo kiasi Mbacho mnadhani kitatosha kwa mwezi (kutegemea na Mahitaji yenu, hii ni ya kununua vitu vidogo vidogo vitakavyopelea)
 
Tatizo kubwa ni kuwa
kukiwa na vitu vingi ndani ndivyo na matumizi yanakua ya hovyo.House
girl anakata kitunguu nusu anatupa mafuta anamimina tuu kwa kuwa kuna
galoni Tabu tupu

mkuu pole, house girl ni janga. hawajui thamani ya pesa. Mama anapaswa awe ana monitor kwa ukaribu jinsi anavyotumia. ikishindikana kila kitu anampa kwa kiasi vingine store.

hawa viumbe hashindwi kukupikia wali nusu sufuria ni ukoko. au ugali lundo kisa kaona unga, ukibaki haumwagwi huo.. kwa friji na mlaji wa kwanza awe yeye ajifunze.

utaratibu wa kununua vitu kwa jumla ni mzuri kama uwezo unaruhusu.
 
Wanawake wa siku hizi jinga sana. Hivi jana si ilikuwa yao sijui yamejazana ujinga gani tena mwaka huu?
umeamua kumkosea heshima mama yako kwa nini? Au umesahau mama nae ni mwanamke au unajua mwanamke ni mkeo tu? Da pana shida kidogo hapa juu ya jinsi tunavyoichukulia istilahi hii muhimu kwa uwepo wa wanadamu wote. Kuhusiana na mada inategemea na jinsi familia ilivyojipanga cha msingi epuka sana utoaji wa matumizi wa rejareja manake ni hatari katika ustawi wa familia na mpango huu sio sustainable kuna siku utailaza njaa familia. Nawasilisha.
 
Siku hizi mpango ni mmoja tu, mama anaandaa list ya vyakula vya mwezi esp visivyokuwa perishable mf mchele, unga, mafuta, maharage, sukari nk then mnaenda kununua vyote. Vile perishable mf nyama, nyanya, majani, matunda, maziwa fresh nk mtanunua vikihitajika, bajeti yake huwa sio kubwa. Kama ni familia ya watu 4, laki 3 inawatosha kabisa kwa kila kitu na hata chenji kubaki; kwa familia za kawaida.

Naungana nawe. hapa utaweza kuzibiti magumizI yasiyo rasmi.
 
kama mke nae anafanya kazi, mnaweza kujiwekea utaratibu kua, kuhusu mambo ya chakula ndani ya nyumba, mwanamke ndio atakua responsible...

Mambo mengine kuhusu umeme, maji, school fees, na mambo mengine mwanaume ndo atafanya.. ukitumia mfumo huu mwanamke atakua makini sana na vitu vya ndani

NB: sio kila family huu mfumo unaweza fanya kazi, mm napendelea sana hizi system na imefanya kazi vizuri
 
Mkewangu anataka elfu 10 kwa siku na kila kitu kipo ndani kasoro mboga tu, umeme maji vyote nalipia mie je hii ni sawa?


Upo sawa kabisaa,bado kuuguaa na penyewe ni kutoa pesa,bado nguo matumiz hayaishagiii
 
  • Thanks
Reactions: SDG
mkuu pole, house girl ni janga. hawajui thamani ya pesa. Mama anapaswa awe ana monitor kwa ukaribu jinsi anavyotumia. ikishindikana kila kitu anampa kwa kiasi vingine store.

hawa viumbe hashindwi kukupikia wali nusu sufuria ni ukoko. au ugali lundo kisa kaona unga, ukibaki haumwagwi huo.. kwa friji na mlaji wa kwanza awe yeye ajifunze.
utaratibu wa kununua vitu kwa jumla ni mzuri kama uwezo unaruhusu.
Wewe utakuwa unamfahamu dada kazi wetu(wali nusu ukoko) hiyo taabu tunayo mimi na mama watoto!hafundishiki huyo binti japo tunamkubali sana kwenye masuala ya usafi na kulea zile toto zetu!
 
Wadau hii bhana imekuwa ngumu sana, maana nakumbuka nilisafiri kidogo miezi sita nikaacha 480,000 watt wadogo 3 binti wa kazi mama mzazi na mke wangu ila mwanamke alilalamika sana kwamba ninamuumiza sana akili kupanga bajeti maana maisha yamepanda na pesa haitoshi,

ila niliporudi home nikanunua vyakula vyote ikanigharimu 250,000 kisha nikamkabidhi 150,000 mkononi,

amin usiamin ilifika mwisho wa mwezi bila tatizo na 80,000 iliyobaki nikampa mwisho wa mwezi ili aone kuwa sio ngumu..


Kinachosumbua wakezetu uvivu wa kufikiri tu na kupanga mahitaji husika...
 
Back
Top Bottom