Ni maisha ya aina gani uliyapitia wakati unaishi kwa ndugu? Karibu tukumbushane na tujifunze!

Fohadi

JF-Expert Member
Jul 24, 2020
770
2,408
Miaka kadhaa nyuma elimu ilinitenganisha na familia yangu. Shule niliyotakiwa kusoma ilikuwa mbali sana na nyumbani kwetu (Ile shule wazee walikuwa wanaipenda kiasi kwamba waliamini ile ndio pekee inayonifaa kitaaluma). Ni mwendo wa masaa 18 kwa bus kutoka mkoa niliokuwepo (Nyumbani) kwenda kule ambako nilitakiwa nikasome (pia wapo ndugu).

Hii ilionesha dhahiri kuwa isingekuwa rahisi hata kurudi nyumbani mara kwa mara wakati wa likizo kwani ni mda ambao ilitakiwa niutumie kwa tuition na kupumzika. Ilibidi kukubali uhalisia kuwa sasa naenda mbali na nyumbani na nitakaa kwa dada yake baba. Kabla ya hapo niliwahi kuonana nae mara 2 tu maishani (kiufupi hatufahamiani kwa 98%).

Maisha mapya katika makazi mapya yalianza. Nakumbuka kuna kipindi kama miaka 2 mfululizo tulipitia changamoto kubwa sana ya kimaisha mimi na shangazi. Mlo mmoja kwa siku ndio ilikuwa bajeti yetu, chai na ubwabwa ilikuwa ni misamiati tu ambayo tuliishia kusikia harufu kwa majirani. Bajeti ya sh. 1000 kwa siku ilikuwa inatutosha kabisa mimi na shangazi yangu. Yalikuwa ni maisha chini ya nusu dollar kwa siku.

Sio kwamba shangazi alikuwa ananitesa, HAPANA!, bali upepo wa maisha ulibadilika tu. Sio kwamba wazazi wangu au ndugu zetu wengine kwenye ule mkoa walikuwa hawapo tayari kusaidia, HAPANA!, ila shangazi tu hakuwa tayari na siku zote alinisisitiza kupambana na kila hali na kutopenda kulia liashida mara kwa mara kwa watu wengine. Shangazi alinifundisha somo la maisha na hadi leo linaniongoza. Kuna kipindi shangazi alikuwa analala njaa ili mimi "mtoto' nile kile kidogo alichojaaliwa kesho niwe na nguvu za darasani. Kiufupi malezi/maisha yangu ya miaka 5 kwa shangazi yalijaa upendo wa hali ya juu na furaha tele.

Huyu ndiye shangazi yangu wa dhahabu, mama yangu wa pili baada ya mama yangu mzazi. Nashukurur sasa nimekuwa na ninajitegemea. Siku zote nimekuwa najitahidi kushea kidogo ninachokipata na shangazi yangu. Najua siwezi mlipa wema wake ila siku zote namuomba Mungu anijalie mafanikio ili nije nimlipe japo nusu tu.

Kuna muda nikisikia manyanyaso wanayopata wengine wanaoishi na ndugu zao (mfano Dada, shangazi, mamdogo, shemeji au wifi n.k), huwa naumia sana na nazidi kumshukuru Mungu kwa kunibariki mlezi wa thamani.

Ni kweli, nakiri kuwa upendo wangu kwa shangazi hauwezi kuzidi upendo nilionao kwa wazazi wangu na ndugu zangu wa damu. Ila thamani yake kwangu ni kama ile ya mama na mwana. She is my second Mother!

Dear Aunt, thank you for the precious scene you played in my life series.

 
Hakuna changamoto ngumu kama kulea mtoto wa mtu au kulelewa na mtu mwingine tofauti na wazazi wako. Yote mawili nimepitia.

Nimewalea wadogo zangu watatu wa mama mmoja huyu wa mwisho yupo form six na wawili wamemaliza chuo nimeambulia kupata Hypertension at below 40 years.

Wazazi wangu waliachana nikiwa na 6 months kwa mama nilitoka nikiwa na 3 years baada ya hapo sikulelewa na baba wala mama.
 
Hakuna changamoto ngumu kama kulea mtoto wa mtu au kulelewa na mtu mwingine tofauti na wazazi wako. Yote mawili nimepitia.

Nimewalea wadogo zangu watatu wa mama mmoja huyu wa mwisho yupo form na wawili wamemaliza chuo nimeambulia kupata Hypertension at below 40 years.

Wazazi wangu waliachana nikiwa na 6 months kwa mama nilitoka nikiwa na 3 years baada ya hapo sikulelewa na baba wala mama.
Mkuu natamani kujua zaidi kupitia wewe, hivi ni kwanini ukimsaidia mtu mfano kumsomesha na baada tu ya huyo mtu ku fanikiwa inakuwa Vita kubwa.
 
Nilisoma boading kwa raha kama zote ila o level, nilikuwa nje ya tz kidogo kiasi kwamba mapumziko kama ya wiki mbili nililazimika kwenda kwa anti yangu.

Mtoto wa anti mkubwa tulisoma shule moja yeye akinizidi kidato. So tukifunga tunaenda wote kwao.
Maisha pale nyumbani yalikuwa ya kawaida. Nilipenda kujiongeza coz ndivyo nilivyolelewa nyumbani, saa 12 nishaamka kazi zote nimemaliza. Napika chai nawaamsha wanakunywa, baadae nampelekea anti chai shambani. Hata kulima nilikuwa nalima na anti tho alikuwa akinikataza nibaki home nisome na wengine.nikawa nakataa coz nilijua nakula bure

Huyo binti yake anti alikuwa hanipendi kiviile basi tu hana namna.
Siku moja tumekaa na anti story kibao huyo bint akamwambia anti, yaani mama yake hivi:

" yaani mama unavyompenda luckyline akinya kwenye sahani unaweza kuilia chakula bia kuiosha"🤭🤭🤭 .hata anti aliona aibuu.

huyo binti wakati huo alikuwa f4 so alimaanisha sio kwamba alikuwa mdogo hapana.

Iliniuma sana. Tho haiwezi niuma kama mtu trh 28 kukataa kwenda kupiga kura akisingizia mvua.
Kazi ya kulinda kura sio yako, weka tiki rudi nyumbani, mwenye nazo atazilinda.
 
Hakuna changamoto ngumu kama kulea mtoto wa mtu au kulelewa na mtu mwingine tofauti na wazazi wako. Yote mawili nimepitia.

Nimewalea wadogo zangu watatu wa mama mmoja huyu wa mwisho yupo form na wawili wamemaliza chuo nimeambulia kupata Hypertension at below 40 years.

Wazazi wangu waliachana nikiwa na 6 months kwa mama nilitoka nikiwa na 3 years baada ya hapo sikulelewa na baba wala mama.

Hebu endelea kidogo mkuu, nitalipia ikibidi.
 
Sitaki hata kukumbuka maana ni hatari lkn Leo wamekuwa kila shida wanakimbilia kwangu, ni vile tu tumeumbwa na moyo wa msamaha ndani
 
Baada ya kufeli darasa la saba (enzi hizo) nikachukuliwa na ndugu aliyeamini katika elimu, aliona uwezo wangu sio mbaya ila mazingira hivyo akanipeleka kuishi naye mjini.

Nikarudi shule, darasa moja na kijana wake ambaye ni rika moja na mimi... ikawa nikimnyoosha darasani anakuja kulialia kwa mama hivyo tukaanza kama chuki kati yetu.

Ni utoto tu, ego... ila maisha ya nyumbani yalikuwa fair na kwangu niliona mazuri ukizingatia nimetoka bushi ndani ndani huko choka mbaya.

Stori iko hapa:
Kwa sasa maisha angalau ila kiukweli nilimtosa mno huyu ndugu yangu aliyenishika mkono na kunirudisha shule, ingawa hakunisomesha ila njia yangu na mwanga kupitia elimu ulianzia kwenye mikono yake.

Namshukuru Mungu huyu Mzee yupo hai, kwa sasa ni mstaafu... maisha yake ni ya kawaida hana njaa kwa vile pia ana sapoti za watoto wake wale wengine huku mimi nikipambana kuokoa jahazi kule bushi kwetu.

Basi kuanzia leo, nitaanza kumjali huyu mlezi wangu... asanteni kwa uzi huu umesaidia kunikumbusha mema niliyotendewa.
 
Msalimie shangazi..Shangazi ana watoto??

Kuna ndugu ukiishi kwao ni shida...Hata ukienda kuoga watakwambia unachafua sabuni..
 
Ukiishi kwa ndugu unapaswa kufahamu kinaga ubaga kwamba sio kwenu hapo, fata sheria na taratibu za hiyo familia, kama wanakula mara moja kwa siku kubali usilalamike in short kubali yote ukifanikisha kilochokupeleka ondoka.
 
Mkuu natamani kujua zaidi kupitia wewe, hivi ni kwanini ukimsaidia mtu mfano kumsomesha na baada tu ya huyo mtu ku fanikiwa inakuwa Vita kubwa.
Ni kwasababu unakuwa unafanya kama unawekeza kumbe ule siyo uwekezaji.
Yani wewe mlee msaidie tu kama vile watoa sadaka. Akifanikiwa akakusaidia shukuru asipokusaidia shukuru.
Sasa watu wengi tunakuwa tuna mategemeo makubwa kwamba pale akifanikiwa atalipa fadhila. My brother hayo mawazo yaache, siku hizi hata watoto wanaweza wasiwasaidie wazazi wao sembuse ndugu?
 
Back
Top Bottom