Ndugu, wadau nimekuwa nikiitizama Nchi yetu kwa muda mrefu na kuutafakari uelekeo wetu na kushindwa hata kuamua kwa vitu vidogo kabisa. Hebu fikiria hadi leo hii, Tanzania na ikiwa ni hivi majuzi tu, tumetoka kusheherekea nusu karne ya kuutumikia uhuru wetu, lakini bado tumeshindwa hata mambo madogo kabisa. Mathalani wadau hadi leo hii ni lipi hasa gari linalotumika hasa na serikali yetu, yaani ukipita barabarani basi uwe na urahisi wa kutambua kwamba hili ni gari la serikali na hili ni aina ya gari la mtu binafsi.
Hata sasa tembea huko mitaani utaona Hyundai, Toyota Landcruiser ya aina yeyote,Corolla, Landlover,Mitsubishi, Rav 4 na nyingine za aina mbalimbali zikiwa zote zinatumika na serikali yetu. Tunashindwa kweli kuwa na sera au muongozo wa kusema kwamba magari ya serikali ni haya! Hayumkini katika kipindi kifupi kijacho sasa serikali yetu itatumia Hammer na Vogue. Waziri Mh. Dk John Pembe Magufuli waziri mwenye dhamana uko wapi.
Wadau tuijadili hiyo, mwenye majibu please!
Hata sasa tembea huko mitaani utaona Hyundai, Toyota Landcruiser ya aina yeyote,Corolla, Landlover,Mitsubishi, Rav 4 na nyingine za aina mbalimbali zikiwa zote zinatumika na serikali yetu. Tunashindwa kweli kuwa na sera au muongozo wa kusema kwamba magari ya serikali ni haya! Hayumkini katika kipindi kifupi kijacho sasa serikali yetu itatumia Hammer na Vogue. Waziri Mh. Dk John Pembe Magufuli waziri mwenye dhamana uko wapi.
Wadau tuijadili hiyo, mwenye majibu please!