rodrick alexander
JF-Expert Member
- Feb 12, 2012
- 15,189
- 20,156
Ni lini Uganda italipa fidia ya vita vya Kagera pamoja na mahusiano mabaya kati ya Tanzania na Uganda kwenye miaka ya mwanzoni ya 70 hasa baada ya Tanzania kuamua kumpa hifadhi ya kisiasa rais aliyepinduliwa Milton Obote.
Mzozo huo uliingia hatua nyingine baada ya majeshi ya Uganda yakiongozwa na Idd Amin Dada yalipovuka mpaka na kuua raia,kufanya uharibifu wa mali kama kuharibu kiwanda cha sukari,kuvunja daraja na kuitangaza Kagera kuwa sehemu ya uganda.
Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa Mwalimu Nyerere iliingia vitani ili kukomboa sehemu ya nchi yetu na pia iliamua kuingia hadi Uganda na kumng'oa Idd Amin madarakani.
Baada ya vita, Uganda ilitakiwa kulipa gharama zilizotokana na uharibifu wa mali na upotevu wa maisha uliofanywa na majeshi ya Uganda yalipovamia Tanzania.
Baada ya vita mbali na baadhi ya askari wetu kupoteza maisha,wengine walipata vilema na wengine kupata maradhi kama matatizo ya akili hali hii haikuwaathiri wao tu bali iliziathiri hata familia zao,jambo lakusikitisha wengi wa askari hao hawakulipwa fidia na hata familia zao nazo zimeishi maisha duni hadi sasa.
Katikati ya miaka ya 2000 tulisikia kauli ya rais Museveni akiiomba serikali ya Tanzania ilifute deni lilitokana na vita vya Kagera lakini kwa bahati mbaya sikusikia kauli yoyte toka serikali ya Tanzania kama wamekubaliana naye au la.
Ingawa binafsi sikubaliani na ombi hilo labda wajadiliane kuhusu riba iliyotokana na deni hilo,nina hakika serikali ya Uganda inaweza hatakupunguza deni hilo kwa kulipa kidogokidogo kwani chini ya utawala wa rais Museveni tumeshuhudia matumizi makubwa ya kijeshi ikiwamo kushuhudia ikishirikiana na majeshi ya Rwanda kuvamia Kongo.
Mzozo huo uliingia hatua nyingine baada ya majeshi ya Uganda yakiongozwa na Idd Amin Dada yalipovuka mpaka na kuua raia,kufanya uharibifu wa mali kama kuharibu kiwanda cha sukari,kuvunja daraja na kuitangaza Kagera kuwa sehemu ya uganda.
Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa Mwalimu Nyerere iliingia vitani ili kukomboa sehemu ya nchi yetu na pia iliamua kuingia hadi Uganda na kumng'oa Idd Amin madarakani.
Baada ya vita, Uganda ilitakiwa kulipa gharama zilizotokana na uharibifu wa mali na upotevu wa maisha uliofanywa na majeshi ya Uganda yalipovamia Tanzania.
Baada ya vita mbali na baadhi ya askari wetu kupoteza maisha,wengine walipata vilema na wengine kupata maradhi kama matatizo ya akili hali hii haikuwaathiri wao tu bali iliziathiri hata familia zao,jambo lakusikitisha wengi wa askari hao hawakulipwa fidia na hata familia zao nazo zimeishi maisha duni hadi sasa.
Katikati ya miaka ya 2000 tulisikia kauli ya rais Museveni akiiomba serikali ya Tanzania ilifute deni lilitokana na vita vya Kagera lakini kwa bahati mbaya sikusikia kauli yoyte toka serikali ya Tanzania kama wamekubaliana naye au la.
Ingawa binafsi sikubaliani na ombi hilo labda wajadiliane kuhusu riba iliyotokana na deni hilo,nina hakika serikali ya Uganda inaweza hatakupunguza deni hilo kwa kulipa kidogokidogo kwani chini ya utawala wa rais Museveni tumeshuhudia matumizi makubwa ya kijeshi ikiwamo kushuhudia ikishirikiana na majeshi ya Rwanda kuvamia Kongo.