Ni lini Spika Job Ndugai atajibu tuhuma za yeye na Wabunge kuhongwa Pesa na serikali ya Magufuli ili kupitisha miswada mibovu ya sheria kandamizi?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
116,495
215,349
Mh Mbowe katika hotuba yake kwa Taifa pamoja na mambo mengine mengi aliyoyazungumza, pia alizungumza kwa msisitizo sana jinsi Bunge la Tanzania lilivyogeuzwa kuwa Muhuri wa kupitisha Sheria mbovu za ukandamizaji pamoja na kuunga mkono bajeti za serikali zenye makando kando.

Mbowe alitamka bila kumung'unya maneno kwamba Spika na Naibu wake waligeuzwa kuwa Watumishi wa serikali kwa kulazimishwa kuhudhuria kila hafla ya Magufuli , kama haitoshi Mbowe aliendelea kusema Spika na Wabunge wa CCM walihongwa pesa taslimu ili kupitisha bajeti na miswada ya hovyo , huku akisema anao ushahidi wa jambo hilo na akiombwa atauweka hadharani bila shaka yoyote ile

Sasa swali langu dogo ni hili, ni LINI JOB NDUGAI atajitokeza hadharani kukanusha hili ama kulitolea ufafanuzi?
 
Mambo ni mengi muda mchache...!

Huyu Mbowe atoe tu ushahidi kwani anataka nini. Eti mpaka aombwe Mfyuuu zake
 
Nadhani kama watanzania tusisubiri yeye apange ni wakati gani bali tumlazimishe kupitia kwenye majukwaa mbali mbali .
 
Sheria kandamizi huwaathiri wananchi wengi wakawaida. Hivi ni hawahawa wanachi ambao walijitokeza kwa wingi(pengine haijawahi kutokea) kumsindikiza hayati JPM ktk safari yake ya mwisho ndiyo waliogandamizwa na sheria za awamu ya tano? Kama ni kweli kwamba watanzania hawa waliomsikitikia kwa kiwango kile ndiyo wanaogandamizwa na sheria hizo basi tunasafari ndefu sana mkuu.
 
1618302414332.png
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom