Ni lazima sasa Rais ale kiapo cha kuitii Katiba!!

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,088
33,576
Kwa mujibu wa Katiba yetu, Rais wa Tanzania anapoapishwa uahidi "kulinda na kuitetea" Katiba ya Jamhuri ya Muungano Tanzania. Maana ya kuilinda ni dhidi ya mtu, watu, ama kundi jingine. Kwa maneno mengine kiapo hakimlazimishi Rais kujilinda yeye binafsi kuvunja katiba.

Rais wetu huilinda Katiba yetu dhidi ya watu wengine, jee yeye ni nani anayemlinda dhidi ya uvunjaji wa Katiba yetu? Usiseme Bunge wala Mahakama zetu kama zilivyo hivi sasa, kwani kwa muundo wa Katiba yetu hii dhaifu na iliyojaa viraka, vyombo hivyo viwili haviwezi kutunishiana Misuli linapokuja suala la maslahi binafsi ya Rais katika uvunjwaji wa Katiba.

Kwa mtazamo wangu ni vizuri sasa kikaongezwa kipengere ama maneno ya kumtaka Rais kuitii Katiba ya Jamhuri ya Muungano Tanzania katika kiapo siku ya kuapishwa kwa Rais. Hii itamlazimsha Rais Kumlazimisha kutii Katiba kwani akienda kinyume cha hata mtu wa kawaida tu anaweza kwenda Mahakamani kulalamika kwamba Rais ameshindwa kuitii Katiba.


John Pombe Magufuli akila Kiapo cha kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania
 
Katiba Ipi?
Ya Chama Tawala
Ama Ya JMT
Unwritten Constitution
 
Mkuu kwaiyo unamaanisha raisi Magufuli ameshundwa kufuata na kuieshimu katiba?
 
Mkuu kwaiyo unamaanisha raisi Magufuli ameshundwa kufuata na kuieshimu katiba?
Hoja si Magufuli bali kuwe na kipengere ama maneno kwenye kiapo cha Rais kwamba ataitii Katiba. Kwa kuwa wakati mwingine bila ya kuwepo kwa maneno hayo inakuwa vigumu sana kumzuia Rais kutenda mambo nje ya Katiba!!
 
Kukiuka katiba ni miongoni mwa mambo yanayoweza kusababisha rais kuondolewa madarakani kama bunge lingekua na meno
 
Kukiuka katiba ni miongoni mwa mambo yanayoweza kusababisha rais kuondolewa madarakani kama bunge lingekua na meno
Bunge la katiba hii nusu yake ni Rais, yaani Rais ana 50% na wabunge wote wana 50%. Kwa maneno mengine Bunge kumchukulia hatua Rais imekaa kinadharia zaidi kuliko kiuhalisia. Bunge linaweza kushughulika na Waziri Mkuu pekee.
 
Kwa mfumo huu wa katiba hii mbovu ambayo inamfanya rais kuwa mungu mtu ndani ya nchi usahau mkuu kuitikii hii katiba inayompa mamlaka makubwa hata kufanya lolote bila kuguswa na yeyote

Ili tuweze kuwa na mabadiliko ya kimfumo yaliyo strong ni sharti kwanza tuizike hii katiba mbovu inayowapa viongozi wakuu uhuru wa kufanya lolote lile na hakuna wa kuwagusa

Lazima tuwe na mifumo ya mahakama, bunge na serikali inayojitegemea na iliyo huru, siyo mkuu wa mhimili wa mahakama anateuliwa na rais, huku katibu wa bunge ambaye kimamlaka ndiyo mwezeshaji wa bunge naye anateuliwa na rais, hatuwezi kufika kwa kuwa na mihimili mi tatu jina tu, lakini kiuhalisia mhimili uko mmoja tu ambao ni serikali

Tuwe na katiba inayompora rais mamlaka ya kuteua mkuu wa jeshi la polisi na maafisa wengine wa polisi wa ngazi za juu, Jaji mkuu na Katibu wa bunge.

RC na DC hizi nafasi ziondolewe ama ziwe za kuchaguliwa na wananchi wa mkoa/wilaya husika

Tuwe na katiba inayotambua uwepo wa mfumo wa vyama vingi vya kisiasa, hii katiba ya sasa iko na mapungufu mengi sana kwenye uhuru na uwanja sawa wa kufanya siasa kati ya chama tawala na upinzani kwa ujumla wake
 
Hizi asasi za kigeni zinawajaza ujinga watanzania. Vipi kama rais anailinda katiba kwa kutoonyesha unyonge dhidi ya matakwa ya matajiri ambao wanatumia nguvu za madalali wao?.

Aliyeiletea siasa Afrika hakuwa ni mpango wa Mungu wa moja kwa moja, bahati mbaya hakufahamu kwamba anatumika.
 
Back
Top Bottom