Mtuache
JF-Expert Member
- Mar 12, 2021
- 251
- 637
Habari za wakati huu,
Nimekuwa nikisoma nyuzi mbali mbali humu Jamii Forums na nimefurahishwa nazo. Ila sifurahishwi na hii tabia ya mtu kupachika mstari wa kiingereza eti ndo kuonesha Msisitizo wa Mawazo yake.
Kwa mfano, utakuta mtu anaongelea kuhusu kutokuwepo kwa Mungu, anaadika hivi "kiuhalisia hakuna Mungu THERE'S NO GOD......"
Kwani ukitumia kiswahili tu hutoeleweka? Yaani sababu kuu kwa kutumia kiingereza katikati ya uzi wako ni nini? Ingekuwa labda kuna neno unataka kulisema lakini hujui kwa kiswahili sawa ila sio kutafsiri kile kile. Yaani umeandika sentensi ya kiswahili alafu mbele unaandika hiyo hiyo ila kwa lugha ya kiingereza
Sisemi kwamba msitumie kiingereza hapana, tumieni. Maneno yangu mimi sio sheria.
Karibuni kwa maoni.
Nimekuwa nikisoma nyuzi mbali mbali humu Jamii Forums na nimefurahishwa nazo. Ila sifurahishwi na hii tabia ya mtu kupachika mstari wa kiingereza eti ndo kuonesha Msisitizo wa Mawazo yake.
Kwa mfano, utakuta mtu anaongelea kuhusu kutokuwepo kwa Mungu, anaadika hivi "kiuhalisia hakuna Mungu THERE'S NO GOD......"
Kwani ukitumia kiswahili tu hutoeleweka? Yaani sababu kuu kwa kutumia kiingereza katikati ya uzi wako ni nini? Ingekuwa labda kuna neno unataka kulisema lakini hujui kwa kiswahili sawa ila sio kutafsiri kile kile. Yaani umeandika sentensi ya kiswahili alafu mbele unaandika hiyo hiyo ila kwa lugha ya kiingereza
Sisemi kwamba msitumie kiingereza hapana, tumieni. Maneno yangu mimi sio sheria.
Karibuni kwa maoni.