Ni lazima kumgharamia mwanamke kila kitu hapaswi kusaidia hata kama ana kazi

Wezere

Senior Member
Nov 2, 2010
109
24
Wadau naombeni mnijuze kwa hili.
Unapokuwa kwenye serious relationship means unaishi na mwanamke au umeoa.Je bill zote na gharama zote i mean outing,hospital,rent,shelter,cloth,saloon,fees and other miscellaneous expenses must be covered by men hata kama mwanamke ana kipato.


Mi naona mambo ni kusaidiana ila maendeleo yapatikane.Man can provide alot but woman also must have her share.But to my relationship ni tofauti mpenzi wangu akilipa bill hata moja atongea siku nzima japokuwa ana kazi na kipato chake ni cha wastani.


Jamani nishaurini is that ryt for a woman to share part of the bill au hapaswi kujigusa kabisa?
 
mambo kama hayo huwa nikusaidiana wekeni wote vipato vyenu pamoja mpange wote mwezi huu kipi kinahitajika bila kujali huyu anakipato kikubwa ama kidogo mwelimishe mkeo nyumba hujengwa na wote sasa kama hadi salon ulipe wakati ana mshahara wake una kazi gani?siku hizi nikusaidiana ndo maana akaenda shule na kazi akawanayo
 
Kama kipato chako ni cha kawaida ni sawa kabisa kusaidiana ila kuna wale wanaume wanakuwa wana mabiashara makubwa, au kipato chake ni kikubwa sana, anamwachia tu mkewe pesa yake inakuwa ya salon na mambo mengine madogomadogo
 
Mwanamke daima huwa hawezi kujiamini kuwa anaweza fanya kitu flani mwenyewe hata awe na kipato au kazi nzuri,hata kama anapesa zake atahitaji umpatie wewe.Kimsingi ni vizuri watu wakasaidiana katika hilo lakini kutokujiamini kwa wanawake waliowengi ndo imekuwa tatizo
 
Mwanamke daima huwa hawezi kujiamini kuwa anaweza fanya kitu flani mwenyewe hata awe na kipato au kazi nzuri,hata kama anapesa zake atahitaji umpatie wewe.Kimsingi ni vizuri watu wakasaidiana katika hilo lakini kutokujiamini kwa wanawake waliowengi ndo imekuwa tatizo
Kujiamini vipi? nature inasemaje kwani?mbona mnakwepa sana majukumu yenu vijana wa siku hizi kwa kigezo cha kusaidiana? mie sikatai kusaidia,ila nature inasemaje? au hata Mungu mnapingana nae aliposema mwanaume atakula kwa jasho lake na atatunza familia yake mwenyewe?
 
Kama kipato chako ni cha kawaida ni sawa kabisa kusaidiana ila kuna wale wanaume wanakuwa wana mabiashara makubwa, au kipato chake ni kikubwa sana, anamwachia tu mkewe pesa yake inakuwa ya salon na mambo mengine madogomadogo

Shantel, yani kama tulikuwa pamoja hivyo ndo nilivyomwomba mwenzako hataki kusikia hata hayo mambo madogo madogo,yani kwa kifupi agharamiwe kila kitu
 
Kujiamini vipi? nature inasemaje kwani?mbona mnakwepa sana majukumu yenu vijana wa siku hizi kwa kigezo cha kusaidiana? mie sikatai kusaidia,ila nature inasemaje? au hata Mungu mnapingana nae aliposema mwanaume atakula kwa jasho lake na atatunza familia yake mwenyewe?

Hatupingani na Mungu Shantel mambo siku hizi yamebadilika sana.We have alot of challenges in our life na pia wanawake wa siku hizi sio kama mama zetu wengi wao walikuwa magolikipa tu.Wanawake mnatakiwa kujifunza kwa mataifa yalioendelea sana kiuchumi tusiende mbali angalia kwa majirani zetu wakenya sharing ipo katika kila kitu.Hatusemi mfanye kila kitu ila mambo madogo madogo kama saloon na vingine vidogovidogo mnamaliza na mkishindwa tunasaidiana.
Na nina wapongeza sana wanawake wa kichaga ni mfano mzuri sana kwa hili na wote ni mashahidi kwa kufanya hivyo wameendelea sana
 
Shantel, yani kama tulikuwa pamoja hivyo ndo nilivyomwomba mwenzako hataki kusikia hata hayo mambo madogo madogo,yani kwa kifupi agharamiwe kila kitu
Kama una kipato kikubwa achana na kumwambia asaidie, w mtunze tu mpe pesa ya salon mwisho wa siku tajikuta anafanya mwenyewe kwa kujua ulishamwambia na sasa umemu ignore
 
inaonyesha kabisa ni jinsi gan mtoa mada hilo tatizo lako lilivyo kuumiza na nahitaji msaada wa kimawazo, kwanza busara hapo lazima ishike mkondo wake ili kumshauri huyo mpenzi wako.tafuta muda mzuri mtoe out na umueleze yanayokusibu nadhani ataelewa na kama anakupenda kweli basi atajitahidi kubadilika japo kwa asilimia fulani

ni hayo tu nimewamssii JF wote
 
Kama una uwezo mpe huduma zinazostahili mkeo why not bana
 
Mwanamke daima huwa hawezi kujiamini kuwa anaweza fanya kitu flani mwenyewe hata awe na kipato au kazi nzuri,hata kama anapesa zake atahitaji umpatie wewe.Kimsingi ni vizuri watu wakasaidiana katika hilo lakini kutokujiamini kwa wanawake waliowengi ndo imekuwa tatizo
Ngoja wakusikie...lol
 
Kama mlikutania baa sawa ila kama mnapendana huwa hamhesabian kwamba huyu kafanya nini na yule kafanya nini yote ni mafanikio ya familia moja na ndoo maana inafika sehemu mna waza kuuwana bila sababu za msingi ili kuridhi mali pole sana kwa huyo aliye kamatwa hivyo
 
Kama una uwezo mpe huduma zinazostahili mkeo why not bana
Sawa,lakini yeye kamshahara kake anapeleka wapi?hata vitunguu ninunue mimi!inakera bwana,kama mshahara wake hauna mchango wowote basi haina maana yeye kufanya kazi.
 
Mkuu mimi hlo kwangu nimelitatua na sasa ni raha mustarehe, mnafungua joint account kipato chake anaweka humo, wote mnakuwa na rty ya kudrow, kwa kuwa wanawake ni wavivu kulipa bili we usimsumbue go & drow & spend nae
ingawa pesa ni zake ila ukilipa wewe anasikia raha sana c wajua akili zao zipo nyuma yetu!
 
Hakuna sababu yoyote inayoeleza kwa nini mwanaume anapaswa zaidi kulipa everything. Si lazima ufuate sexist norms kama hizi, ninyi ni huru kufanya uamuzi wo wote unaokufaani (ninyi wawili na sio mke wangu tu) zaidi. Nafikiri kwamba yafaa mwenye kipato kubwa zaidi (awe mwanamke au mwanaume) achangie zaidi katika kulipa kwa bills. Mwenye kipato kidogo bado anapaswa kuchangia though, isipokuwa mke/mume wake ana pato kubwa sana kama waziri au mfanyabiashara successful.
 
Mkuu mimi hlo kwangu nimelitatua na sasa ni raha mustarehe, mnafungua joint account kipato chake anaweka humo, wote mnakuwa na rty ya kudrow, kwa kuwa wanawake ni wavivu kulipa bili we usimsumbue go & drow & spend nae
ingawa pesa ni zake ila ukilipa wewe anasikia raha sana c wajua akili zao zipo nyuma yetu!

Umetisha kaka,hiyo strategy ni nzuri i like it
 
Hiyo ni nature na haiwezi kubadilishwa kirahisi kwa ajili ya kipato.Nijuavyo ni kuwa mwanaume anatakiwa ampende mke wake na mke amtii,apokee maagizo kutoka kwa mume wake.Kama unampenda utamghamia kila kitu kwa sababu ndiyo sheria ya upendo.Upendo hauhesabu gharama,upendo hauhusudu,hautakabali,upendo huona kuwa kila atendacho mwenzako ni sawa.Hivyo kuanza kuhesabu yeye ana mshahara au ana kipato kunizidi,ndugu yangu hapo hakuna upendo.
MPENDE MKEO.UPENDO HAUHESABU GHARAMA.
 
Back
Top Bottom