Ni Kweli ZFA wapenda migogoro au kuna namna?????

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
haya wale magwiji wa michezo ambao mlikuwa mkifatilia kwa muda mrefu mvutano uliopo kati ya ZFA na TFF hii inatokana na kuwa ZFA ni wapenda migogoro au kuna namna.

jee huyu mwakalebela hutumia kutofahamina kati ya ZFA na SMZ ni kisingizio cha kuhalalisha ufifilishi wao kwa ZFA na zanzibar kwa ujumla?
ZFA ni wapenda migogoro - Mwakalebela
2008-06-18 09:03:14
By Somoe Ng\'itu


Shirikisho la soka nchini (TFF) limesema kuwa Chama cha Soka cha Zanzibar (ZFA) kinatumia muda mwingi kuanzisha malumbano na migogoro inayohusiana na safari za nje ya nchi badala ya kuandaa programu za maendeleo ya mchezo huo visiwani humo.

Akizungumza na Nipashe jana, Katibu Mkuu wa TFF, Frederick Mwakalebela alisema kuwa viongozi wa ZFA ambao hivi karibuni wametangaza rasmi kutoshirikiana na shirikisho hilo kuhusiana na timu ya taifa, Taifa Stars kila siku wamekuwa wakianzisha `hoja` zinazopingana na serikali yao na pia wakilalamikia vitu ambavyo ufafanuzi wake wanaufahamu na kuipotosha jamii.

Mwakalebela alisema kuwa katika kuonyesha kuwa chama hicho kinatumia muda mwingi `kulumbana` badala ya kufanya shughuli za maendeleo kimetangaza kutoshirikiana na TFF huku timu zao za vijana za umri chini ya miaka 17 ziko jijini Dar es Salaam na zinashiriki katika mashindano yanayojulikana zaidi kwa jina la Copa Coca Cola yanayoendelea katika viwanja mbalimbali.

``ZFA wanashindwa kujielewa mambo wanayosema na wanayofanya, kama wamevunja ndoa na TFF ni kwanini wameleta timu katika mashindano ya U-17 na mjumbe wao pia yupo,`` alisema Mwakalebela.

Aliongeza kuwa kila inapotokea safari ya viongozi wa TFF wanakwenda katika mikutano ya kimataifa kuiwakilisha nchi ndio malalamiko yanapoanza na wao wanashindwa kuwaelewa ZFA ambao wanafahamu wazi kuwa waalikwa wa mikutano hiyo ni TFF ndio wanachama wa mashirika ya soka ya kimataifa.

Alisema pia kila kinachofanywa na TFF kinatokana na maelekezo yaliyopo katika katiba na wao ZFA wana katiba yao inaowaongoza katika shughuli za kila siku za kuongoza soka hapa nchini.

Alisema kuwa ZFA mara kadhaa wameshindwa kukubali kuihudumia timu ya taifa, Taifa Stars inapotaka kwenda visiwani humo na wakati TFF imeisaidia timu yao, Zanzibar Heroes na kuinunulia vifaa ilipokuja katika mashindano ya Kombe la Chalenji mwaka jana lakini yote hayo hayasemwi.

``Umefika wakati wakaacha kuipa kipaumbele migogoro na kuangalia mambo ya msingi ya maendeleo, TFF ni wanachama wa FIFA (Shirikisho la soka la kimataifa) tutafanya kila kinachotakiwa kukuza soka hapa nchini,`` aliongeza.

Siku moja kabla ya Stars haijacheza na timu ya taifa ya Cameroon, Makamu wa Rais wa ZFA, Haji Ameir alikaririwa akisema kuwa wao wamevunja `ndoa` na TFF na kudai kuwa Stars ni timu ya Tanzania Bara.

SOURCE: Nipashe
 
Kwa wale wote ambao walikuwa wakibeza juhudi za Farouk Karim sasa watatia akili akiwepo huyo mwenyeki wa sasa wa ZFA... Mapungufu ya TFF na SMZ kuingilia mara kwa mara maamuzi ya ZFA ndio yamempa mdomo hiyo Katibu Mkuu wa TFF.
 
TFF nao wamezidi safari za Taifa stars wanaenda wao tu walau wachukue mtu mmoja kutoka ZFA ile ni timu ya Taifa sio bara hawajui hata kura na kipofu! halafu wakilalamika mnasema wanapenda migogoro
 
SMZ yaipinga ZFA
2008-06-23 10:32:01
By Mwinyi Sadallah,Zanzibar


Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imesema kuwa haikubaliani na tamko lililotolewa na Chama cha soka cha Zanzibar (ZFA) juu ya kujitenga na kuvunja ushirikiano na Shirikisho la mchezo huo Tanzania (TFF).

Akizungumza juzi visiwani hapa, Naibu Waziri Kiongozi na Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo, Ali Juma Shamhuna alisema kuwa SMZ haikuwatuma viongozi wa ZFA kutamka kauli hizo na kuongeza kuwa wao wanaitambua TFF na wataendelea kushirikiana nao katika mambo mbalimbali ya maendeleo ya soka hapa nchini.

Waziri Shamhuna alisema kwamba uamuzi uliotolewa na ZFA kupitia Makamu wake wa Rais, Haji Ameir uliishitua serikali na kuongeza kuwa chama hicho hakina mamlaka ya kuvunja ushirikiano wa kimichezo baina ya Zanzibar na Tanzania Bara.

``Ushirikiano wa TFF na ZFA uko pale pale, na hakuna mtu mwenye mamlaka ya kuuvunja,`` alisema Shamhuna.

Alisema kwamba timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars ni timu ya watanzania na sio timu ya TFF au ZFA, na kwa msingi huo viongozi wa ZFA hawakupaswa kutoa tamko la kumtaka kocha msaidizi wa Stars Ali Bushiri pamoja na wachezaji wa timu hiyo wanaotoka Zanzibar kurejea nyumbani kwa madai ya kuwa kuwepo kwao katika timu hiyo hakuifanyi timu hiyo kuwa na sura ya Muungano.

Alisema kwamba Serikali haitovumilia watu wanaotaka kuvuruga Muungano kwa kisingizio cha michezo na kwa kufanya hivyo wanakwenda kinyume na katiba ya nchi inayozungumzia kuwa Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aliongeza kuwa kutokana na uzito wa maneno yaliyotolewa na kiongozi huyo wa ZFA, atakutana na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo wa Muungano, George Mkuchika ili kuzungumzia tofauti zilizojitokeza baina ya taasisi hizo zinazoongoza michezo Tanzania Bara na Visiwani baada ya vikao vya bajeti vinavyoendelea Dodoma na Zanzibar kumalizika.

Alisema ni jambo la kushangaza shutuma za ZFA zinatolewa huku baadhi ya viongozi wake wakiwa wanashiriki katika mashindano ya Copa Coca Cola yanayoshirikisha vijana wenye umri chini ya miaka 17 ambayo yanalenga kuinua vipaji vya vijana.

Alisema kwamba ZFA hivi sasa inapaswa kuwaeleza wanamichezo kuwa ina mikakati gani ya kuinua kiwango cha michezo Zanzibar hasa ikizangatiwa kuwa ni sehemu pekee inayoendelea kuendesha ligi yake katika muda wa mapumziko.

SOURCE: Nipashe
 
Kariim ndio aliye anzisha jitihada za Zenj kujulikana na FIFA na CAF, akiwa katika hatua za mwisho mwisho wakamletea za kuleta na yeye akaweka madaluga chini...

vipi kuhusu Ali Tamim Fereji ? nnakumbuka yeye ndio alikuwa akienda mbio na hili?


halafu kwa nn Shamhuna na ZFA(viongozi) picha haziendi?
 
vipi kuhusu Ali Tamim Fereji ? nnakumbuka yeye ndio alikuwa akienda mbio na hili?


halafu kwa nn Shamhuna na ZFA(viongozi) picha haziendi?
Picha siku zote hazitakwenda kati ya ZFA na Wizara yao.. Kwani kumekuwewpo na mitazamo tofauti juu ya uendeshaji wa soka hapo kisiwani.. Siku zote wizara inataka watu ambao watasimamia matakwa ya wizara katika kuendesha shughuli za ZFA, wakati ZFA inatakiwa kuendeshwa kwa katiba yao na sio kwa kauli za waziri wa michezo.

Ndio maana kila waziri aingiae kwenye wizara hiyo lazima atapandikiza mtu wake.... hapo ZFA tena mwenye uwezo wa kutoa uwamuzi...
 
Picha siku zote hazitakwenda kati ya ZFA na Wizara yao.. Kwani kumekuwewpo na mitazamo tofauti juu ya uendeshaji wa soka hapo kisiwani.. Siku zote wizara inataka watu ambao watasimamia matakwa ya wizara katika kuendesha shughuli za ZFA, wakati ZFA inatakiwa kuendeshwa kwa katiba yao na sio kwa kauli za waziri wa michezo.


Ndio maana kila waziri aingiae kwenye wizara hiyo lazima atapandikiza mtu wake.... hapo ZFA tena mwenye uwezo wa kutoa uwamuzi...

nimekuelewa sana, sasa safari hii vipi wizara ilishindwa kuplant mtu wao au kulikoni ?


halafu kwa nini wasitafute njia yakukaa nakujadili kwa kina njia bora ya kuendesha soka visiwani.

maana mambo yakienda hivi ni aibu kwa taifa na kama mwakalibela alivyotukebehi.
 
nimekuelewa sana, sasa safari hii vipi wizara ilishindwa kuplant mtu wao au kulikoni ?


halafu kwa nini wasitafute njia yakukaa nakujadili kwa kina njia bora ya kuendesha soka visiwani.

maana mambo yakienda hivi ni aibu kwa taifa na kama mwakalibela alivyotukebehi.
Nahisi ZFA kiwe chombo huru... Kiwe na katiba yake ambayo haitaweza kubanwa na smz, kiwe chombo kinachojitegemea pasipo kuwa omba omba toka smz.. ila katiba yao isivunje katiba ya muungano. Katiba hiyo iweke bayana nafasi ya ZFA katika TFF na iwapo siku Zenj itakapokubalika FIFA basi mazagazaga ya TFF yawekwe pembeni.

Baraza la michezo Zenj nalo litokane na katiba mama ya ZFA.. na kiwe ni chombo cha rufaa ya faida ya soka la Zenj badala ya kusimamia matakwa ya smz katika soka la visiwa hivyo.
 
TFF, ZFA kujadili tofauti


VIONGOZI wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na wale wa Chama cha soka Visiwani Zanzibar (ZFA), mwishoni mwa mwezi huu, wanataraji kukutana kujadili changamoto zinazowakabili.

Akizungumza mwishoni mwa wiki, Katibu Mkuu wa TFF, Fredrick Mwakalebela alisema kikao hicho cha siku moja, kitajadili masuala mbalimbali muhimu ikiwamo mwelekeo wa soka ya Tanzania.

Hivi karibuni, ZFA ililalamika kubaguliwa na TFF katika masuala muhimu ya kimuungano, ukiwamo kunyimwa mgawo wa dola 250,000 za Marekani zinazotolewa kila mwaka na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA).

Baada ya malalamiko hayo kufika hadi katika vikao vya Bunnge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, TFF na ZFA, zilikutana kuangalia dosari zilizopo kwa nia ya kuzifanyia kazi.

Kikao kijacho, kitakuwa cha tatu ambako wajumbe wa pande zote mbili, watawasilisha mezani taarifa ya majukumu waliyopeana.

Katika vikao hivyo, TFF imekuwa ikiwakilishwa na Makamu wa Kwanza wa Rais, Crescentius Magori, Makamu wa Pili, Jamal Bayser, Mwenyekiti wa Kamati ya Waamuzi Tanzania, Joseph Mapunda na Katibu Mkuu wa TFF, Mwakalebela.

ZFA, ni Hafidh Ali, Makamu Mwenyekiti wa ZFA, Haji Ameir, mjumbe wa ZFA, Mzee Zam na Masoud Atai.


Source: TZ Daima
 
Zimamoto team dispute ZFA ban

Zanzibar`s Fire Brigade Unit is contemplating to pull out of all sports activities in the Isles following last week`s shocking relegation of their first division team, Zimamoto FC.

Zimamoto`s sports department secretary Hamza Hamza levelled accusations against Zanzibar Football Association leadership for slapping a heavy penalty to his team.

ZFA relegated Zimamoto FC from first to third division following crowd trouble that led to stabbing of referee Hamis Maswa last week.

Hamza said ZFA leaders have overreacted to impose such a harsh penalty that has demoralised efforts by the fire brigade unit to implement government sports policy.

Hamza said ZFA leaders are not running the association in the proper direction to culminate into soccer downfall in the Isles.

Beside the Zimamoto soccer team, the fire brigade unit has active teams in netball, basketball and ngoma cultural troupe.

Hamza alleged that ZFA leaders are deliberately sabotaging the fire brigade unit`s efforts to promote sports, especially the football team.

Hamza said his sports department is contemplating to notify the unit`s commissioner with regard to their pulling out decision.

He said Zimamoto FC has been under constant awful surveillance by the soccer body ever since winning promotion into the first division.

``We are intending to pullout from sports activities in the Isles as a result of poor cooperation from sports bodies such as ZFA which has rocked our efforts to surge ahead,`` said Hamza.

According to Hamza, ZFA officials were supposed to make thorough investigation into the circumstances leading to the stabbing of the referee.

The fire brigade official said the incident that led to stabbing of the referee was framed up by joint efforts of some first division teams competing in the league. He did not mention the teams.

Besides the relegation penalty, ZFA has also banned its coach Juma Yussuf for three years.

Yussuf is alleged to have inspired his players and fans to fuel the fracas that culminated into injury of the referee who was later rushed to hospital and stitched six times.

ZFA has also slapped a fine to the tune of 200,000/= plus payment of 20,000/= to recover the referee’s wrist watch that was lost during the riots.

Zimamoto fans went on the rampage to unofficially protest a 2-2- match result when their team played Ngome in the first division league match played at Fuoni a fortnight ago.

Ngome pulled a surprise last-gasp equaliser that paralysed Zimamoto fans who had already set up their minds in celebrating the victory that was not to be.


SOURCE: GUARDIAN
 
haya wale magwiji wa michezo ambao mlikuwa mkifatilia kwa muda mrefu mvutano uliopo kati ya ZFA na TFF hii inatokana na kuwa ZFA ni wapenda migogoro au kuna namna.

jee huyu mwakalebela hutumia kutofahamina kati ya ZFA na SMZ ni kisingizio cha kuhalalisha ufifilishi wao kwa ZFA na zanzibar kwa ujumla?
ZFA ni wapenda migogoro - Mwakalebela
2008-06-18 09:03:14
By Somoe Ng\'itu


Shirikisho la soka nchini (TFF) limesema kuwa Chama cha Soka cha Zanzibar (ZFA) kinatumia muda mwingi kuanzisha malumbano na migogoro inayohusiana na safari za nje ya nchi badala ya kuandaa programu za maendeleo ya mchezo huo visiwani humo.

Akizungumza na Nipashe jana, Katibu Mkuu wa TFF, Frederick Mwakalebela alisema kuwa viongozi wa ZFA ambao hivi karibuni wametangaza rasmi kutoshirikiana na shirikisho hilo kuhusiana na timu ya taifa, Taifa Stars kila siku wamekuwa wakianzisha `hoja` zinazopingana na serikali yao na pia wakilalamikia vitu ambavyo ufafanuzi wake wanaufahamu na kuipotosha jamii.

Mwakalebela alisema kuwa katika kuonyesha kuwa chama hicho kinatumia muda mwingi `kulumbana` badala ya kufanya shughuli za maendeleo kimetangaza kutoshirikiana na TFF huku timu zao za vijana za umri chini ya miaka 17 ziko jijini Dar es Salaam na zinashiriki katika mashindano yanayojulikana zaidi kwa jina la Copa Coca Cola yanayoendelea katika viwanja mbalimbali.

``ZFA wanashindwa kujielewa mambo wanayosema na wanayofanya, kama wamevunja ndoa na TFF ni kwanini wameleta timu katika mashindano ya U-17 na mjumbe wao pia yupo,`` alisema Mwakalebela.

Aliongeza kuwa kila inapotokea safari ya viongozi wa TFF wanakwenda katika mikutano ya kimataifa kuiwakilisha nchi ndio malalamiko yanapoanza na wao wanashindwa kuwaelewa ZFA ambao wanafahamu wazi kuwa waalikwa wa mikutano hiyo ni TFF ndio wanachama wa mashirika ya soka ya kimataifa.

Alisema pia kila kinachofanywa na TFF kinatokana na maelekezo yaliyopo katika katiba na wao ZFA wana katiba yao inaowaongoza katika shughuli za kila siku za kuongoza soka hapa nchini.

Alisema kuwa ZFA mara kadhaa wameshindwa kukubali kuihudumia timu ya taifa, Taifa Stars inapotaka kwenda visiwani humo na wakati TFF imeisaidia timu yao, Zanzibar Heroes na kuinunulia vifaa ilipokuja katika mashindano ya Kombe la Chalenji mwaka jana lakini yote hayo hayasemwi.

``Umefika wakati wakaacha kuipa kipaumbele migogoro na kuangalia mambo ya msingi ya maendeleo, TFF ni wanachama wa FIFA (Shirikisho la soka la kimataifa) tutafanya kila kinachotakiwa kukuza soka hapa nchini,`` aliongeza.

Siku moja kabla ya Stars haijacheza na timu ya taifa ya Cameroon, Makamu wa Rais wa ZFA, Haji Ameir alikaririwa akisema kuwa wao wamevunja `ndoa` na TFF na kudai kuwa Stars ni timu ya Tanzania Bara.

SOURCE: Nipashe
mwakalebela asipotoshe umma, kujidai kuwa mwaka jana waliisadia tumu ya zanzibar heroes vifaa kwa mashindano ya challenge, ule haukuwa msaada bali ni sehemu ya matumizi ambayo yanatokana na misaada inayotolewa na taasisi za kimataifa kwa jina la Tanzania na misaada hiyo kuishia mikononi mwa TFF tu, zanzibar wakiambulia masimbulizi na masimango wanapodai sehemu yao. Mwakalebela hawaambii ukweli watanzania kudai kuwa ZFA inalalamikia safari za nje, huo ni uzushi , inacholalamika ZFA ni kuwa fursa za kimataifa zinazokuja kwa jina la Tanzania kama nyenzo na mambo mengine, zinatumika upande mmoja tu wakati Zanzibar ni sehemu ya fursa hizo mfano project za FIFA n.k
kama suala ni safari za nje, kitu ambacho si kweli kama anavyodai Mwakalebela, zanzibar imekuwa ikipata mialiko mingi tu ya kimataifa kwa jina la zanziba mpaka mengine inaingiliana katika ratiba,Mwakalebela aseme ukweli asipotoshe nini kinafanyika katika maslahi yanayohusu pande mbili, wanajilimbikizia wao tu....
 
TFF sasa imetulia baada Tenga kuwa bosi

ZFA watafute mbinu za kuendeleza soka wapunguze kulalamika..Ona Bara Vodacom, Serengeti na TBL wanvyomwaga pesa TFF!

Sasa nani alaumiwe??
 
Back
Top Bottom