Umati wa wanachama na wapenzi wa simba, waliofika klabuni hapo jana mchana, na kushinikiza Wambura arudishwe kwenye uchaguzi, au wapewe sababu za Wambuea kuenguliwa!
Je, Wambura kweli hastili kwa mujibu wa taratibu za soka, au anaogopwa?
Mkuu hebu soma maoni haya niliyoyadadavua sehemu:-Unajua viongozi wa soka wa nchi hii hawajui kumaliza masuala yao kidiplomasia.Kilichotakiwa kufanyika ni kumruhusu kugombea halafu kumnyima kura. Uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya Simba chini ya Wakili Msomi mwenzangu Dr.Damas Ndumbaro umeacha shaka kuu.
Katika uamuzi huo,Kamati imejikita katika sababu kuu mbili.Ya kwanza ni kwamba Wambura aliwahi kupeleka suala la soka Mahakamani.Ya pili ni kuwa aliwahi kufukuzwa uanachama. Lakini,hata Mwenyekiti wa sasa wa Simba,Ismail Aden Rage alimteuwa Wambura kuwa Mjumbe wa Kamati ya Utendaji.
Sasa, aliteuliwaje mtu asiye mwanachama wa Simba kuwa kwenye Kamati Tendaji? Halafu,Wambura,kama si mwanachama wa Simba,alipewaje fomu za kugombea na kuruhusiwa kufanya mchakato mzima wa kugombea nafasi ya Urais. Nikiwa na heshima kubwa kwa Kamati ya Wakili Msomi mwenzangu Ndumbaro,nauona uamuzi wa kumuengua kama uliojaa ukakasi na bifu la kimichezo tu.
Suala hili kwasasa linaonekana dogo.Lakini,baadaye litakuwa kubwa na kuibua mgogoro Klabuni hapo ambao unaweza kuepukwa sasa.
Muhimu : Mimi si mwanachama wa Klabu yoyote Tanzania lakini ni mshabiki wa Klabu ya Yanga ya Tanzania na AC Milan/Barcelona za Ulaya.
huu uzi umetulia. binafsi ni mwanayanga ila sifurahishwi na upuuzi huu wa ndumbaro na wenzake. natoa rai kwa malinzi na tff yake kumtendea haki wambura ikizingatiwa kuwa malinzi nae alishakuwa muhanga wa ubabaishaji kama huu
Unajua viongozi wa soka wa nchi hii hawajui kumaliza masuala yao kidiplomasia.Kilichotakiwa kufanyika ni kumruhusu kugombea halafu kumnyima kura. Uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya Simba chini ya Wakili Msomi mwenzangu Dr.Damas Ndumbaro umeacha shaka kuu.
Katika uamuzi huo,Kamati imejikita katika sababu kuu mbili.Ya kwanza ni kwamba Wambura aliwahi kupeleka suala la soka Mahakamani.Ya pili ni kuwa aliwahi kufukuzwa uanachama. Lakini,hata Mwenyekiti wa sasa wa Simba,Ismail Aden Rage alimteuwa Wambura kuwa Mjumbe wa Kamati ya Utendaji.
Sasa, aliteuliwaje mtu asiye mwanachama wa Simba kuwa kwenye Kamati Tendaji? Halafu,Wambura,kama si mwanachama wa Simba,alipewaje fomu za kugombea na kuruhusiwa kufanya mchakato mzima wa kugombea nafasi ya Urais. Nikiwa na heshima kubwa kwa Kamati ya Wakili Msomi mwenzangu Ndumbaro,nauona uamuzi wa kumuengua kama uliojaa ukakasi na bifu la kimichezo tu.
Suala hili kwasasa linaonekana dogo.Lakini,baadaye litakuwa kubwa na kuibua mgogoro Klabuni hapo ambao unaweza kuepukwa sasa.
Muhimu : Mimi si mwanachama wa Klabu yoyote Tanzania lakini ni mshabiki wa Klabu ya Yanga ya Tanzania na AC Milan/Barcelona za Ulaya.
Simba hawamtaki ila Yanga wanamtaka awe kiongozi wa Simba. ADUI MWOMBEE NJAA
unasemaje juu ya mtu asiye mwanachama kushiriki vikao halali vya chama na kupitisha katiba ya chama? ni kama mtu asiyejiandikisha kupiga kura, je hiyo kura itakuwa ni halali? si ndio uchaguzi wote utakuwa ni batiliMimi naishangaa jamii yetu Watanzania. Inaelekea wengi wetu tunashindwa kuelewa nia na madhumuni ya Katiba, sheria, kanuni na taratibu. Katiba za FIFA, TFF na Simba zinamruhusu kila mwanachama wa Simba kugombea nafasi ya uongozi. Wambura alifanya hivyo akiamini yeye ni mwanachama wa Simba. Aliziwiwa? Hapana kwa sababu Katiba haimziwii mgombea kuwasilisha fomu ya kugombea. Katiba inaruhusu mwanachama kumwekea pingamizi mgombea anayemwona hastahiki. Wanachama wamefuata katiba hiyo na kuweka pingamizi dhidi ya Wambura. Katiba imeipa uwezo Kamati ya uchaguzi ya Simba kusikiliza pingamizi hizo na kuzitolea maamuzi. Ndicho kilichofanyika. Katiba inaishia hapo? Hapana. Inampa uhuru asiyeridhika na maamuzi hayo kukata rufaa TFF. ndicho kilichofanyika. Huko kufunga mtaa kwa maandamano na kujitoa ugombea ni ishara kwamba hao wahusika (wagombea na wafuasi wa Wambura) hawana uelewa wa mchakato wa kikatiba ya timu yao wenyewe. Wataongoza na kuongozeka vipi? Maoni yanayofaa kukubalika kuwa ndio ukweli ni ya waliopewa jukumu la kusikiliza na kuamua kesi kisheria pekee. Tuliobaki tunapaswa kuwacha maoni yetu yawe maoni yetu, tusiyafanye maoni yetu kuwa ndio ukweli wenyewe. Kasoro hii ndani ya jamii yetu ndio iliotufikisha tulipo hata kwenye mchakato wa Katiba ya nchi yetu. Halafu eti tunawashangaa Wabunge!
vyovyote nitakavyosema, yatabaki kuwa ni maoni yangu. Wa kujibu hoja hiyo ni mamlaka iliyopewa jukumu la kutoa maamuzi. Ila kwa maoni yangu hayohayo, kura hiyo ni batili, lakini si lazima maamuzi yote ya kikao hicho yawe batili. Kama maamuzi hayo yalipita kwa tofauti ya kura moja, yanaweza kuwa ni maamuzi batili. Kwa sababu kuna haki ya kuamini kwamba kura hiyo batili ndiyo iliyopitisha maamuzi hayo. Lakini kama maamuzi yalipitishwa kwa tofauti ya zaidi ya kura moja, bado yatabaki kuwa ni maamuzi halali kwa sababu hata kura hiyo batili ingefutwa, bado kungebaki kura za kutosha kupitisha maamuzi hayo. Nasisitiza tena kwamba hayo ni maoni yangu.unasemaje juu ya mtu asiye mwanachama kushiriki vikao halali vya chama na kupitisha katiba ya chama? ni kama mtu asiyejiandikisha kupiga kura, je hiyo kura itakuwa ni halali? si ndio uchaguzi wote utakuwa ni batili