Eti ulikuwa ndani hujui ni redio gani, kama wewe mwenyewe unaona aibu kutaja source huoni kuwa kuna walakini na habari yenyewe.Nilikua ndani,mwenye radio yuko nje sijajua ni redio gani,..
ila kaongelea mda mrefu habari ya sugu na uhamasishaji wake
wewe unataka gazeti gani liandike ili ujue kama ni tatizo? Mtu anapochemka kwenye masuala ya msingi anatakiwa kusemwa ili asirudie kwani ni aibu kubwa kwa mbunge kunena hayo. Niliwahi sikia mtu akivuta bangi hata akiacha ile athari humtoka baada ya miaka 40.kwahiyo asiwe alipanda jukwaani akiwa amesha pandisha mzuka. maana siamini kama mtu mzima wa akili anaweza kuongea hayo mbele ya wapiga kura wake.Ivi anadhani wapiga kura ni mazuzu?mara nyingi ukiwa pale jukwaani ongea uwezavyo lakini ukitoka pale ujue ima umejijenga au umejibomoa kwani wanachi watabaki wanayajadili maneno yako na kujua kama unawafaa kwa maendeleo au la
kwa wakati huu mi naona wabondwe mawe tu...na ikibidi hata mapana wacharazwe,sio watu wa kuwaonea huruma wahujumu uchumi...na sugu nae akiboronga acharazwe mapanga,hadi kieleweke.The leaders need to serve the people and not their stomach and family.
Acha wivu wa kike wewe... Sugu alipata kura 48,000 na kumuacha mpinzani wake kwa kura 27,000. Sio ushindi wa kubeza hata kidogo na hapo uchakachuaji ulifanyika. Kura za sugu ni nyingi kuliko za wabunge wote wa CCM Zanzibar ukizijumlisha kwa hiyo sio wa kubahatisha kama akili yako mbovu inavyokudanganya. Suala la kuelezea hisia halizingatii kuwa watu kama wewe watafurahia au la, kama kiongozi hamumpendi mzomeeni tu, na hao viongozi tusiowataka wakija Mbeya tunawazomea vilevile. Mbona hata Slaa alizomewa na mujahidina pale Tabora, kwani kuna mtu alilalamika? Watu walikuwa wanatoa hisia zao za kiislamsugu uwezo wake ni miziki ya kufokafoka na sio siasa, hata hivo sugu kushinda ccm walimpambanisha na mtu aliyekuwa hakubaliki ndani ya ccm yenyewe. Nilisha wahi changia kuwa Sugu uchaguzi ujao hawezi shinda tena, kwani uwezo wake ni mfinyu mno.Maneno aliyoyaongea ni kama tulivosikia na mara baada ya yeye kuchemka Slaa na Mbowe wakaona aibu na mbowe pale pale akasimama na kumkosoa vikari kwa upupu aliouongea,yaani anazidi kujizika yeye mwenyewe.waswahili tunasema mazoea hujenga tabia, sugu alizoea toka akiwa mwana muziki katika majukwaa ni kuimba miziki ya kupaka(kutukana,kujisifu ...) kwahiyo nawashauri viongozi wa chadema watu kama hao musiwape nafasi ya kusimama kwenye majukwaa.
Wewe hukuwepo uwanjani vinginevyo ungekiri kwamba Mh Mbowe alifafanua maana ya kupiga mawe kuwa ni kususia mambo yanayofanywa na mafisadi. Hata Sugu mwenyewe alifafanua kwamba kupiga mawe ni kutokwenda kwenye matamasha ya wasanii mafisadi, mikutano yao na hata magazeti yao ni kususia. Sugu aliongea kisanii lakini Mbowe alifafanua kirefu sana tena kwa kina. Tuache ushabikiMimi kwa sasa niko Mbeya, na bahati nzuri nilikuwepo uwanjani. Ni kweli nilimsikia Sugu akisema mafisadi wapondwe mawe. Mwanzoni nilihisi anasema kinadharia, lakini baadaye ikaonesha kama kweli ni mawe halisia, kwa kuwa hakufafanua nadharia niliyodhani, na watu wote tumetoka viwanja vya Ruanda Nzovwe tukijua tuwaponde mawe mafisadi. Sentensi ya mwisho ya salamu zake, Sugu alisisitiza tena kwamba mafisadi wapondwe mawe na hasa Mwanjelwa (Kkoo ya Mbeya). Sitaki mafisadi, ila pale Sugu alinichefua. Inakuwa kama siasa za kihuni. Bahati mbaya haikufafanuliwa na viongozi waandamizi waliomfuatia kutoa nasaha zao. Heri angesema wazomee tu. Wanasiasa wanatakiwa kuwa makini sana na maneno wayasemayo, kwani ama yatawabomoa wao mbele za uso wa jamii au yawabomoe wananchi.
Nimesikia kwenye habari za magazetini asubuhi
hii kwamba mbunge wa mbeya mjini
ame hamasisha wana nchi wa mbeya kwamba
akija kiongozi ambaye hawamtaki,...
au kiongozi yeyote,hata kama "ni raisi" ni haki yao kumkataa
haka kwa kumpiga mawe!
Kama hii ni kweli,basi Dr.Slaa na wazee wengine ndani ya chadema
mna kazi ya kuwafundisha wabunge vijana
jinsi ya kuongea kwenye public na jinsi ya kutembea "normal" ukiwa na uheshimiwa!
Hizi sio kauli za kutolewa na kiongozi yeyote yule,...
kuna watu walio kuwa wanataka kujiunga na chadema,au walio
muunga mkono sugu,..na ambao ni wastaarabu watakua hawaja furahiswa na
kauli hii,...
na hao wataendelea kuamini kuwa chadema wana hamasisha vurugu!
Ombi:
Naomba viongozi wa chadema,walioko huko kwenye maandamano
wakanushe maneno haya (kama sio kweli kwamba sugu haku yatamka)
maana naamini kila alosikia habari hii kasikitishwa sana,...
kama ni hayo magazeti na wasipo kanusha haitakua na impact au?