Ukifumba macho na kuangalia miezi takribani sita au saba iliyopita unaweza leo hii ukabaki mdomo wazi, kipindi hicho Mtibwa sugar ilikuwa inaongoza ligi ya Tanzania na ndicho kipindi Mecky Mexime alikuwa anaonekana kocha bora mpaka wenye matege yakufikiri wakawa wanapendekeza apewe timu ya taifa.
Mwenyewe Mexime ndicho kipindi alichokuwa anaropoka hovyo na hata kufikia hatua kuwaponda makocha wenzake, lakini wachache tulibaki tu kumsikiliza na kujiuliza kwa ukocha gani alionao?
Lakini hivi tunavyozungumza Mtibwa inapigania kushuka daraja na Mexime mdomo ameufyata lakini pia ukifumba macho na kuiangalia ligi ya msimu uliyopita, utaona jinsi Mbeya city walivyoleta amsha amsha katika ligi ya tanzania na style yao yakurudisha wanachokipata kwa wananchi wahitaji.
Mashabiki wao walikuwa na style yakwenda mahospitalini kuwaona na kuwafariji wagonjwa na mwisho wa siku waliweza kujitolea kufanya usafi katika jiji lao, watu tukasema sasa timu ya kijamii imepatikana.
Lakini kilichotea hivi sasa kila mtu anashika kichwa, walianza kutimuana wenyewe kwa wenyewe, siasa za kimkoa zikawatafuna hatimaye wamepotea na usishangae msimu ujao tukawakuta wakiwa katika nafasi yakupigania kutoshuka daraja.
Haya siyo mapya kwa sisi tuliokula chumvi nyingi kidogo kuyaona katika ligi ya tanzania, kulikuwepo na timu nyingi tu za aina hii, kwa kawaida timu kama hizi, tunaziita timu mlipuko.
Walikuwepo kajumulo fc, chini ya tajiri wa kitanzania Alex Kajumulo ambaye maisha yake yalikuwa pale Marekani na ambaye alikuwa mwanachama wa Simba alikuja kwa mbwembwe kubwa, Tukuyu Stars, Parsons chini ya tajiri ambaye alikuwa anamiliki migodi ya dhahabu na alikuwa mwanachama wa Simba, ushirika Moshi, hawa wote walikuwepo na wamepotea tatizo ni nini?
Tatizo kubwa linaloziathiri timu hizi mlipuko ni moja tu nalo ni malengo yao yakuwepo ligi kuu malengo yao siku zote hayawi katika kuchukua kombe la ligi kuu bali malengo yao ni kuja kushindana na Yanga na Simba, hasa hasa Yanga, hapo ndipo wanapoanza wenyewe kujipoteza.
Ukiiangalia Azam fc utaona kama ni klabu ambayo ipo kisasa zaidi ni kweli ina kila kitu tena kuzishinda klabu nyingi na muda mwingine hata ulaya kwenyewe, lakini zaidi yakuchukua kombe la ligi kuu ya vodacom nini kingine hasa ambacho wanaweza kusimama mbele ya watu na kujivunia na utajiri wote ambao wanao?
Malengo ya uanzishwaji wa azam yalikuwa yapi? kwanza ieleweke Azam ni chimbuko la timu ya wafanyakazi wa Bakhresa Group of Campanies ambao waliamua kuunda timu yao kwa ajiri ya kujifariji baada ya kazi ngumu za kukanda unga wa chapati na kuuza juice, mwisho wa siku waliamua kununua haki za kipawa Combine fc, na rasmi kuanza kushiriki ligi za ngazi ya chini.
Mzee Bakhresa ambaye ni mshabiki na mwanachama mkubwa wa Simba alipoona mawazo yake yakuiendesha klabu ya simba kisasa yamekataliwa ndani ya Simba ndipo rasimi alipoamua kuwekeza nguvu kwa azam akiwa na lengo kuu lifuatalo; kuhakikisha azam na simba wanashika nafasi mbili za juu huku Yanga ikishika kuanzia nafasi ya tatu, ndipo alipokuja na sera zakubadilishana na kuuziana wachezaji wa simba kwenda azam na wa Azam kwenda Simba.
Hii ndiyo sumu kubwa ambayo Azam walijitengenezea wenyewe na kuamua kuinywa, ingawa Yanga ilipitia misukosuko mingi ikiwemo Azam kuingiza mkono katika mechi nyini za Yanga lakini haikusaidia kitu zaidi yakuiacha yanga ikiwa imara zaidi na kuendelea kubaki katika nafasi mbili za juu, huku swahiba mkuu Simba akibaki kupotea katika mbili bora
Maji sasa yamezidi unga kwa Simba wamechoka sasa nao wanaitaji kujikwamua kutoka katika aibu ya kila mwaka ya kukosa nafasi mbili bora ndipo tunapoona ndugu kwa ndugu wameanza kuombeana mabaya.
Simba sasa anamuombea Azam apoteze mechi zake ili apate nafasi ya pili na azam naye anamuombea simba apoteze mechi zake ili apate nafasi ya pili wote hawa hakuna anayemuombea yanga apoteze mechi zake kwa sababu wanajua wazi Yanga haiwezekani tena.
Azam kabla yakupambana na Yanga alipaswa kwanza kujua asili na chanzo cha mkubwa wake simba, Simba ni zao la yanga ata jina lenyewe la Simba lilipendekezwa na mwanachama namba moja wa Yanga mzee Karume rais wa kwanza wa Zanzibar siku zote ninawaheshimu Yanga,
Azam wasipobadilika kimtazamo nao watapotea na uwanja wa Chamanzi utabaki kama sehemu ya kuhifadhia makontena au maonyesho kuwa kulikuwepo na timu ya Azam dalili zinaanza kuonekana, hatua ya juzi, siku walipocheza na Mbeya city viongozi wao kutukanana hadi kushikana mashati ni dalili tosha.
Siku zote chenye nguvu kina maisha marefu na kinadumu
Mwenyewe Mexime ndicho kipindi alichokuwa anaropoka hovyo na hata kufikia hatua kuwaponda makocha wenzake, lakini wachache tulibaki tu kumsikiliza na kujiuliza kwa ukocha gani alionao?
Lakini hivi tunavyozungumza Mtibwa inapigania kushuka daraja na Mexime mdomo ameufyata lakini pia ukifumba macho na kuiangalia ligi ya msimu uliyopita, utaona jinsi Mbeya city walivyoleta amsha amsha katika ligi ya tanzania na style yao yakurudisha wanachokipata kwa wananchi wahitaji.
Mashabiki wao walikuwa na style yakwenda mahospitalini kuwaona na kuwafariji wagonjwa na mwisho wa siku waliweza kujitolea kufanya usafi katika jiji lao, watu tukasema sasa timu ya kijamii imepatikana.
Lakini kilichotea hivi sasa kila mtu anashika kichwa, walianza kutimuana wenyewe kwa wenyewe, siasa za kimkoa zikawatafuna hatimaye wamepotea na usishangae msimu ujao tukawakuta wakiwa katika nafasi yakupigania kutoshuka daraja.
Haya siyo mapya kwa sisi tuliokula chumvi nyingi kidogo kuyaona katika ligi ya tanzania, kulikuwepo na timu nyingi tu za aina hii, kwa kawaida timu kama hizi, tunaziita timu mlipuko.
Walikuwepo kajumulo fc, chini ya tajiri wa kitanzania Alex Kajumulo ambaye maisha yake yalikuwa pale Marekani na ambaye alikuwa mwanachama wa Simba alikuja kwa mbwembwe kubwa, Tukuyu Stars, Parsons chini ya tajiri ambaye alikuwa anamiliki migodi ya dhahabu na alikuwa mwanachama wa Simba, ushirika Moshi, hawa wote walikuwepo na wamepotea tatizo ni nini?
Tatizo kubwa linaloziathiri timu hizi mlipuko ni moja tu nalo ni malengo yao yakuwepo ligi kuu malengo yao siku zote hayawi katika kuchukua kombe la ligi kuu bali malengo yao ni kuja kushindana na Yanga na Simba, hasa hasa Yanga, hapo ndipo wanapoanza wenyewe kujipoteza.
Ukiiangalia Azam fc utaona kama ni klabu ambayo ipo kisasa zaidi ni kweli ina kila kitu tena kuzishinda klabu nyingi na muda mwingine hata ulaya kwenyewe, lakini zaidi yakuchukua kombe la ligi kuu ya vodacom nini kingine hasa ambacho wanaweza kusimama mbele ya watu na kujivunia na utajiri wote ambao wanao?
Malengo ya uanzishwaji wa azam yalikuwa yapi? kwanza ieleweke Azam ni chimbuko la timu ya wafanyakazi wa Bakhresa Group of Campanies ambao waliamua kuunda timu yao kwa ajiri ya kujifariji baada ya kazi ngumu za kukanda unga wa chapati na kuuza juice, mwisho wa siku waliamua kununua haki za kipawa Combine fc, na rasmi kuanza kushiriki ligi za ngazi ya chini.
Mzee Bakhresa ambaye ni mshabiki na mwanachama mkubwa wa Simba alipoona mawazo yake yakuiendesha klabu ya simba kisasa yamekataliwa ndani ya Simba ndipo rasimi alipoamua kuwekeza nguvu kwa azam akiwa na lengo kuu lifuatalo; kuhakikisha azam na simba wanashika nafasi mbili za juu huku Yanga ikishika kuanzia nafasi ya tatu, ndipo alipokuja na sera zakubadilishana na kuuziana wachezaji wa simba kwenda azam na wa Azam kwenda Simba.
Hii ndiyo sumu kubwa ambayo Azam walijitengenezea wenyewe na kuamua kuinywa, ingawa Yanga ilipitia misukosuko mingi ikiwemo Azam kuingiza mkono katika mechi nyini za Yanga lakini haikusaidia kitu zaidi yakuiacha yanga ikiwa imara zaidi na kuendelea kubaki katika nafasi mbili za juu, huku swahiba mkuu Simba akibaki kupotea katika mbili bora
Maji sasa yamezidi unga kwa Simba wamechoka sasa nao wanaitaji kujikwamua kutoka katika aibu ya kila mwaka ya kukosa nafasi mbili bora ndipo tunapoona ndugu kwa ndugu wameanza kuombeana mabaya.
Simba sasa anamuombea Azam apoteze mechi zake ili apate nafasi ya pili na azam naye anamuombea simba apoteze mechi zake ili apate nafasi ya pili wote hawa hakuna anayemuombea yanga apoteze mechi zake kwa sababu wanajua wazi Yanga haiwezekani tena.
Azam kabla yakupambana na Yanga alipaswa kwanza kujua asili na chanzo cha mkubwa wake simba, Simba ni zao la yanga ata jina lenyewe la Simba lilipendekezwa na mwanachama namba moja wa Yanga mzee Karume rais wa kwanza wa Zanzibar siku zote ninawaheshimu Yanga,
Azam wasipobadilika kimtazamo nao watapotea na uwanja wa Chamanzi utabaki kama sehemu ya kuhifadhia makontena au maonyesho kuwa kulikuwepo na timu ya Azam dalili zinaanza kuonekana, hatua ya juzi, siku walipocheza na Mbeya city viongozi wao kutukanana hadi kushikana mashati ni dalili tosha.
Siku zote chenye nguvu kina maisha marefu na kinadumu