Mimi ningetamani Rais aendelee na ziara zake kutembelea majirani zetu kama vile Visiwa vya Comoro, DRC, Burundi, n.k. huku akiongozana na kundi kubwa la wafanyabiashara na wawekezaji wazawa ili kusaini mikataba mbalimbali ya kibiashara kama wanavyofanya China, Marekani, nk. na hizo nchi. Yaani akatafute fursa nyingine nje ya mipaka yetu ili pesa ya wawekezaji wetu wazawa watakao wekeza huko, irudi nchini kuliko hii ya kuwanufaisha wageni tu mfano Wachina kupitia miradi mbalimbali ya miundombinu huku wazawa tukikamuliwa kweli kweli kupitia kodi na tozo mbalimbali kuwalipa hao Wachina na mwisho wa siku hela zetu wanaenda kujengea nchi yao.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.