Ni kweli ni mkutano wa kilele kuhusu Demokrasia au kuna ajenda nyingine?

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,000
1,019
VCG111335075139.jpg

Na Fadhili Mpunji

Tarehe 9 na 10 mwezi huu Rais Joe Biden wa Marekani atakuwa mwenyeji wa unaoitwa “mkutano wa kilele kuhusu Demokrasia” ambao utawakutanisha viongozi kutoka serikalini, mashirika ya kiraia na sekta kibinafsi. Mkutano huo unatarajiwa kuangazia changamoto na fursa zinazokabili demokrasia duniani na washiriki wanatarajiwa kutangaza ahadi binafsi na za pamoja, mageuzi na mipango ya kulinda na kutetea demokrasia na haki za binadamu ndani na nje ya nchi zao. Kwa mujibu wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani, viongozi watakaoshiriki kwenye mkutano huo watahimizwa kutangaza hatua fulani na ahadi zenye maana kuhusu mageuzi, ili kukabiliana na utawala wa kiimla, kupambana na ufisadi na kuhimiza haki za binadamu.

Marekani imeitisha mkutano huu wakati dunia nzima inakumbuka kilichotokea Marekani katika miaka miwili iliyopita, ambapo vitendo vya Rais aliyepita Donald Trump kama vile zuio dhidi ya waislamu (muslim ban), kuwafukuza wahamiaji haramu kwa njia ya kikatili na hata kuwaweka watoto katika mazingira magumu, vilitajwa kuwa ni vitendo vinavyokwenda kinyume na demokrasia na haki za binadamu. Na baya zaidi ni tukio lilitokea Januari 6 ambapo wahuni walivamia jengo la bunge la Marekani na kufanya vurugu. Kutokana na matukio hayo na mengine mengi, Marekani imeshuka kwenye faharisi ya uhuru duniani kwa nafasi 11, na mwaka jana peke yake ilishuka kwa nafasi 3.

Kuna maswali mengi ya kujiuliza kuhusu nia hasa ya Marekani kuitisha mkutano huu, mbali na inachosema kuwa ni mkutano wa kilele wa Demokrasia. Kwanza ni nchi na maeneo 110 kati ya nchi 195 duniani walioalikwa kwenye mkutano huo, pamoja na umoja wa Ulaya. Ni kigezo gani kimetumika kuwaalika? Kwa mfano, haijulikani ni kwanini Umoja wa Ulaya umealikwa wakati baadhi ya nchi za Ulaya hazijaalikwa, na kwanini Umoja wa Afrika haujaalikwa wakati nchi 17 za Afrika zimealikwa. Hata tukiangalia kati ya nchi 17 za Afrika zilizoalikwa, kimsingi zina hali inayofanana sana na nchi ambazo hazijaalikwa. Ukiangalia baadhi ya nchi zilizoalikwa unaweza kuona kuwa zimejaa vurugu na mauaji ya mara kwa mara, na nchi nyingine zenye utulivu zimeachwa.

Pili, Marekani imeuita mkutano huo kuwa ni mkutano wa demokrasia, lakini kilichotajwa ni kuwa mkutano huo una malengo makuu matatu makuu, kwanza kujilinda dhidi ya tawala za kiimla, pili ni kujadili namna ya kupambana na ufisadi, na tatu kuhimiza kuheshimu haki za binadamu. Kama kweli haya ndio malengo ya mkutano huo, ambayo karibu kila nchi inakubaliana nayo, kwanini isizialike nchi nyingi zaidi? Ni kweli Marekani ina nia ya kuhimiza mambo hayo duniani, au inataka kutumia mambo hayo kuleta mgawanyo duniani na kuzilenga nchi fulani?

Tatu, je mkutano huo ni mwendelezo wa hatua za Marekani kuvuruga utaratibu wa dunia? Tukiangalia swala la haki za binadamu, tunaweza kuona kuwa kuna majukwaa rasmi ya kimataifa yanayojadili mambo hayo, kama Baraza la haki za binadamu. Kwa kuwa jambo hilo linagusa watu wote na nchi zote duniani, basi baraza hilo ni chombo sahihi kujadili kipengele hicho. Anachokifanya Bw. Biden hakina tofauti kubwa na alichokifanya Rais wa Marekani aliyepita Bw. Donald Trump, ambaye alipuuza kabisa utaratibu wa kimataifa kwenye kushughulia mambo ya dunia, na kuanzisha mambo yeye binafsi aliyoona yanafaa. Tofauti ni kuwa Rais Biden anatumia lugha tamu kufanya yaleyale aliyofanya Bw. Trump.

Tukiiangalia Marekani yenyewe kwenye kipengele cha haki za binadamu, bila shaka tunaweza kuona kuwa haina mamlaka ya kimaadili (moral authority) ya kuitisha mkutano huo wakati hali yake yenyewe inatia mashaka sana. Marekani ina rekodi chafu kwenye eneo hilo kuliko hata baadhi ya nchi ambazo hazijaalikwa kwenye mkutano huo. Kila mtu anajua jinsi polisi wa Marekani wanavyoua watu, au kuwatendea vibaya watu wasio wazungu au wazungu wasio matajiri. Hii ni mbali na vitendo vya ukiukaji wa haki za binadamu vilivyofanywa na Marekani katika maeneo mbalimbali ya mashariki ya kati na kwingine duniani.

Tukiangalia mambo hayo kwa ujumla, inakuwa vigumu kujua lengo hasa la mkutano huo na kama kweli ni wa demokrasia, au kama kweli Marekani ina mamlaka ya kimaadili ya kuitisha mkutano kama huo.
 
Nimesoma hadi mwisho kutafuta orodha ya nchi zilizoalikwa na ambazo hazikualikwa, hola. Mada yako ingenoga zaidi kama makundi hayo ungeyataja ili tuone mlengo na hali ya demokrasia .
 
Naona imekuuma baada ya kuona tz hatumo kati ya waalikwa.

Huu mkutano huwa upo miaka yote, ww utakuwa umeusikia mwaka huu.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom