Ni kweli kuwa Jijini Arusha kila watu 100, 80 wanamiliki bastola?

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,367
Wadau, akiuliza maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alitaka kujua mikakati ya serikali katika kuzagaa kwa silaha ikiwemo bastola. Lema alisema kuwa jijini Arusha, kila penye watu 100, watu 80 wanamiliki silaha ambazo huzitumia kuhatarisha usalama wa watu wengine. Amesema kuwa watu hao wengi wanamiliki silaha isivyo halali na wengine wamepewa kwa malengo yasiyojulikana.

binafsi nimetafakari sana maneno hayo ya Lema na hakika sikupata uhalisia na ndipo nilipoamua kuleta hoja hii hapa ili tudadavue kujua uhalisia wake au pengine Lema alikuwa na lengo la kujijenga kisiasa tu. watu wa Arusha naomba mtusaidie katika hili. Hapa matusi na itikadi za kisiasa tuziweke pembeni
 
Wadau, akiuliza maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alitaka kujua mikakati ya serikali katika kuzagaa kwa silaha ikiwemo bastola. Lema alisema kuwa jijini Arusha, kila penye watu 100, watu 80 wanamiliki silaha ambazo huzitumia kuhatarisha usalama wa watu wengine. Amesema kuwa watu hao wengi wanamiliki silaha isivyo halali na wengine wamepewa kwa malengo yasiyojulikana.

binafsi nimetafakari sana maneno hayo ya Lema na hakika sikupata uhalisia na ndipo nilipoamua kuleta hoja hii hapa ili tudadavue kujua uhalisia wake au pengine Lema alikuwa na lengo la kujijenga kisiasa tu. watu wa Arusha naomba mtusaidie katika hili. Hapa matusi na itikadi za kisiasa tuziweke pembeni

Nadhani amefanya vyema kulisemea hili! liwe la ukweli ama sivyo nilazima lichukuliwe umakini maana likipuuzwa kwa hoja ya "anataka kujijenga kisiasa" itakuwa ni uzembe kitahadhari juu ya usalama wa nchi/raia na mali zao!
 
huu utafiti naukataa maana katika jamaa zangu wengi ninaoishi nao R ni wachache mno wenye hiyo kitu labda kama wanamiliki isivyo ,ni janga kama majanga mengine tu.
 
Ni kweli.Mimi na my wife kila mmoja anayo ya kwake.Baba mkwe naye pia ana yake na watoto wake pia.
Dah mkuu, kwa nini mnamiliki silaha kiasi hicho? Kuna tatizo gani huko?
 
huu utafiti naukataa maana katika jamaa zangu wengi ninaoishi nao R ni wachache mno wenye hiyo kitu labda kama wanamiliki isivyo ,ni janga kama majanga mengine tu.
Mkuu, inawezekana Lema hata huo utafiti hakuufanya bali ameongea kwa hisia zake tu
 
Maneno ya sema-sikia hayo!!!!!

Umiliki ni siri yeye kapata wapi hyo data???!!!!
Hata akisema kaenda CAR bado wengi wanarudisha armoury baada ya kujua kuwa utunzaji ni zaidi ya kazi ya ziada!!!!
 
hizo ni takwimu za wabunge wasiojua kujenga hoja, wanatafuta cheap popularity
 
Mkuu, inawezekana Lema hata huo utafiti hakuufanya bali ameongea kwa hisia zake tu

Yuko mmoja wa Sakina ashatabiwa Mawenzi na Mirembe anayo na kwenye mkesha wa mwaka mpya 2011 alipiga mtu wakati akishangilia bahati nzuri alijeruhi tu....... Kwa statistics za Lema sina uhakika!!! Ila bastola zinamilikiwa holela vijana wengi wa kitaa wanazo na ni watu wa kawaida sana, wengine ni vijana kula kulala kwa Shikamoo lakini wanazo na wanamiliki kihalali!! Wengine hata busara za kumiliki manati hawana, lakini wana bastola ..... Serikali isilichukulie kwa wepesi hili suala kweli Arusha kuna umiliki "holela" wa silaha za moto.
Man Utd kafungwa watu wanapiga risasi hewani!!!! Wanatunyima raha Aaaaahkkkk!!!
 
inawezekani ni kweli maana mda si mrefu kuna mtu kapigwa ya tumbo maeneo ya soko kuu.umilikaji wa silaha huku arusha ni mkubwa sana na ndio maana matukio ya kuuana kwa risasi ni mengi mno.mkitofautiana na mtu kidogo tu,tayari maisha yako yanakuwa hatarini!
 
Silaa za moto bado haijawa noma kwa Arusha.
Wanaomiliki bado ni wachache sana na imekua kama fashion pia.
Lakini kubwa ni kua imeleta heshima kitaa.
Mambo ya kutishiana mabero imebaki ngaleloo tu.
Na ungese kama wa westgate sio rahisi kutokea maana watu kibao wemejikoki mamida yote
Lemma aachane na hiyo mambo maana pia imesaidia kupunguza uwizi wa majumbani.
Yeye mwenyewe analisoma game la gemstone na umuhimu wa kua nahio makitu.
Asitafute maujiko kwa kutumia hiyo point.
Otherwise Rombo si mbali, watu watamiliki hata za chini ya uvungu.
 
inawezekani ni kweli maana mda si mrefu kuna mtu kapigwa ya tumbo maeneo ya soko kuu.umilikaji wa silaha huku arusha ni mkubwa sana na ndio maana matukio ya kuuana kwa risasi ni mengi mno.mkitofautiana na mtu kidogo tu,tayari maisha yako yanakuwa hatarini!

Vipi umesahau mida ya zamani kidogo watu kuuliwa kwa mabeto ilikua kitu ya kawaida?
Kuchukuliwa madem club na masela wenye bisibisi tu?
Kuvunjiwa maghetto na majomba wenye mapanga na sime tu?
Saa tano usiku ilikua inaonekana ni mida michafu?
Deal za mawe zinafanyikia chumbani?
Hii kitu imeleta amani.
Ingawa ina disadvantages zake, lakini advantages zake ni kubwa kuliko.
 
Hiyo ina maana 80% ya wakazi wa Arusha wanazo silaha za moto (bastola). Hakuna ukweli hapo! karopoka tu!

kama population ya arachugga ni 2.2million. Ina maana watu 1,760,000 wanazo. Idadi kuu ya hizo silaha yaweza kuwa ni zaidi ya 1.76m (wengine wanamiliki zaidi ya moja)

Hii statistic alitakiwa mzee wa namba za kichwani (Pombe Makufuli) ndo atamke
Lema bado.
 
Yuko mmoja wa Sakina ashatabiwa Mawenzi na Mirembe anayo na kwenye mkesha wa mwaka mpya 2011 alipiga mtu wakati akishangilia bahati nzuri alijeruhi tu....... Kwa statistics za Lema sina uhakika!!! Ila bastola zinamilikiwa holela vijana wengi wa kitaa wanazo na ni watu wa kawaida sana, wengine ni vijana kula kulala kwa Shikamoo lakini wanazo na wanamiliki kihalali!! Wengine hata busara za kumiliki manati hawana, lakini wana bastola ..... Serikali isilichukulie kwa wepesi hili suala kweli Arusha kuna umiliki "holela" wa silaha za moto.
Man Utd kafungwa watu wanapiga risasi hewani!!!! Wanatunyima raha Aaaaahkkkk!!!
Hiyo ya man u kufungwa na watu kurusha risasi hewan mbona kali sana, Ila ni kweli umiliki wa silaa kwa arusha upo kwa hali ya juu sana, na sana ni hawa vijana wanaofanya biashara ya madini akipata kafaida ka milioni kumi na kagari(foresta) anaweka bastola pembeni.
 
Dogo mmoja muarusha jana alipaki escudo new morden pale nbc wenye cheni kama kawaida wakapiga cheni sababu amepaki kwenye mistari; dogo katoka kafungua gari katoa chuma akamwambia jamaa utafungua au niende jela kwa sababu yenu faster jamaa wakafungua akasepa .
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom