Ni kweli kuna watumwa wa ngono?

Mbega Mzuri

Member
Aug 1, 2008
44
2
Wanajamii wenzangu nakuja na mada hii. Msinielewe vibaya, lakini kwa faida na ustawi wa jamii.

Ngono: ni neno linalozungumzia kwa mapana mambo mengi sana yakiwemo kutazama picha za ngono, kujichua na mambo mengineyo. Lakini kwa baadhi ya watu, wingi wa ngono na titendo vyake, vinavyochangiwa na utamaduni wa Kimagharibi umekuwa mtego, ambao ni mgumu kuweza kuukwepa. Utumwa au uraibu wa ngono – baadhi wanauita ugonjwa uliojificha. Wengine wanauita “dhambi isiyozungumza.”

Wakati watu wengi huweka taswira ya wanyama waliopagawishwa na mapenzi, ukweli wa utumwa wa ngono uko tofauti. Wengi wa waathirika siyo wahalifu kifikra na siyo kwamba wazembe.

Lakini ni nani hawa watumwa wa ngono? Hapa ndipo naamua kuileta hoja mbele ya wanaforum ingawa jibu linaweza kukushangaza. Mtu yeyote anaweza kuwa mtumwa wa ngono, kwa sababu ndiyo njia ambayo tumekuzwa nayo tangu tukiwa watoto na tuliendelea nayo mpaka kwenye balehe. Siyo inatokea wakati tukiwa na umri wa miaka 40. Na wengine wanasema kwamba hiyo ndiyo sababu watu wasishangae kuhusu kashfa za ngono zinazotokea ndani ya jamii zetu. Mwathirika wa utumwa huu hawaelewi chochote, na kwa mtu wa kawaida, tabia hii inaonekana kuwa mbali sana na haisadikiki, hawawezi kusadiki.

Ukweli kwamba waathirika wengi wa utumwa wa ngono ni watu wenye familia zao, kazi zao na hata ni waumini ama viongozi wa dini unaweza kuwashangaza watu wengi sana na kuleta matatizo makubwa kwa wahusika wenyewe na jamii kwa ujumla.

Fikiria, unaweza kumkuta baba mzima mwenye familia yake na fedha zake akitangatanga na watoto wadogo, tena wale wa shule, huku akimwacha mama watoto wake akiwa hajui lolote. Mama mzima mwenye fedha na maisha ya hali ya juu, anamwacha mumewe na kutafuta vijana ili waidhi kiu yake ya mapenzi, kwa madai kwamba mumewe amechoka na akifika mshi’do mmoja yuko taabani kabisa!

Vijana wanakwenda kujiunga na kwaya kanisani kwa sababu tu ya kumpata binti fulani, na wengine hufikia hata hatua mbaya zaidi kwa kuamua kutangaza wameokoka ili wawe karibu tu na msichana mwenye msimamo anayemcha Mungu kwa bidii.

Mapadre wanasema kwamba hawaruhusiwi kuoa, lakini kutokana na utumwa wa ngono unaowasakama utakuta ama wanafanya mapenzi na watawa wa kike au kutafuta wanawake wa pembeni, na tayari kuna mashauri mengi hapa Tanzania ya aina hiyo. Wapo wachungaji wengi wa Kondoo wa Bwana ambao wamekwishashikwa ugoni ama wakiwa na wake za watu au wake zao kuwafumania na wahudumu wa kanisa. Wapo mashekhe ambao pamoja na kuwa na wake wanne kama dini ya Kiislamu inavyoelekeza, lakini utakuta wana vimada zaidi ya sita mitaani!

Lakini niseme tu kwamba, huu ni ule upande wenye giza. Ni upande ule wa kuzifurahisha tamaa zao za mwili ambazo zimetengana na fikra zao za kawaida, mpaka watakapokamatwa au kufumaniwa au kitu fulani kilete dunia hizi mbili pamoja na kuleta mgongano.

Wapo ambao utumwa wao wa ngono unatokana na mambo mengi: makahaba, picha za ngono, klabu za usiku ambako wanawake wanacheza uchi na kupendelea kuchukua wanawake tofauti kila siku (one-night stands). Lakini utumwa wa ngono haumaanishi kwamba mpaka ufanye mapenzi na mtu mwingine. Unaweza kuwa unajichua mwenyewe, kutazama picha na sinema za ngono na mambo mengine. Hizi ni tabia za mapenzi zinazozidi na kuhamasisha zaidi.

Kwamba mtu hatimaye huanzisha uhusiano na tabia hiyo na kuifanya tabia hiyo katika kuleta madhara makubwa. Mwathirika “ataendelea kufanya ngono nje” pamoja na uwezekano wa kuipoteza familia yake au kupoteza kazi na heshima pia.

Waathirika mara nyingi hupoteza maelfu ya fedha katika vitendo vyao, wakiziacha familia zao zikiteseka kwa kukosa msaada wa kifedha. Nyumba ndogo, kama wenyewe wanavyoita, hutaka kutimiziwa haja zao haraka sana bila kujali hali ya kipato ya mwanaume husika, na matumizi yao mara nyingi ni makubwa kuliko ya nyumbani kwao. Waathirika mara nyingi hupenda kutumia fedha ili kununua mapenzi na kuwaonyesha hao vimada kwamba wanawajali, lakini wakisahau kwamba huko nyumbani moto unawaka na paka kalala mekoni! Aibu na hatia huchukua nafasi haraka katika raha zao na baadaye huanza kujilaumu kwa vitendo hivyo, ambavyo hata hivyo huwa ni vigumu kwao kuviacha. Njia pekee ambayo wanaweza kuifanya katika kukabiliana na aibu, hatia na maumivu ni kuendelea kufanya vitendo hivyo.

Uga wa saikolojia umekuwa mgumu kukubali kwamba utumwa wa ngono ni uraibu kama ilivyo kwa pombe na dawa za kulevya, lakini wataalamu wanasema unaweza kubomoa maisha ya watu katika njia na kiwango kile kile kama pombe na dawa za kulevya.

Utumwa wa ngono siyo ni kiasi gani au mara ngapi mtu anafanya mapenzi. Utumwa wa ngono ni kuhusu mtu fulani kutumia mapenzi ili kukidhi haja zake za kiakili. Wanatumia kama kimbilio – kupambana na msongo wa mawazo. Wanatumia kupambana na maumivu yaliyopita. Wanatumia ili wapendwe – wakubalike. Wanakimbilia kwenye ulimwengu wa kufikirika badala ya ulimwengu halisi. Ni kama kuwa katika ukuta wa kioo. Unaweza kuuona ulimwengu, lakini huwezi kuugusa na wala wenyewe hauwezi kukugusa. Hivi ndivyo ulivyo utumwa huu. Unataka kuwafikia watu, lakini huwezi, unakuwa umekwama na unajiona kama maisha yako yamepotea na kubomolewa.

Ni kitu gani kinachosababisha tumwa huu? Kama uraibu mwingine, wanasaikolojia wengine wanaamini kwamba ubongo wa baadhi ya watu umeachiliwa huru kwa ajili ya uraibu, iwe pombe, dawa za kulevya chakula au ngono. Tatizo jingine kubwa ni unyanyasaji wa kimapenzi (tutakuja kujadili siku zijazo). Asilimia 82 ya waraibu wa ngono wameshawahi kunyanyaswa kimapenzi wakati wakiwa watoto.

Ninawaomba wanaforum, changieni suala hili maana linatuhusu sote wanajamii. Ninaamini inawezekana kabisa utumwa wa ngono ndio unaoweza kuchangia kwa kiasi kikubwa hata maambukizi ya maradhi mbalimbali ya zinaa, ikiwa ni pamoja na umaskini ; wa fikara na kipato.

Karibuni sana !!!

________________________________________________
If a woman cant do her job, let other women do it for her!!
 
Kila mmoja ana uelewa wake na namna ya kuyafasili mambo. Yeyote anaweza kuzungumza vile anavyoona ama anavyoamini, lakini ikumbukwe kwamba hakuna hata mwizi mmoja aliyewahi kukiri kwamba yeye ni mwizi. Hulka inaweza kumfanya mtu aamini kile anachokifanya kuwa ni sahihi hata kama si sahihi.
 
Watumwa wa ngono ni wale tu malaya wanaofanya biashara ya ngono tu. wengine ni starehe kama mpenda kunywa bia, msoma novels etc etc etc
 
Nafikiri mazingira na umaskini unachangia sana utumwa wa ngono,nikitoa mfano hai mimi wakati niko nyumbani bongo nilitawaliwa na huo utumwa lakini tangu nije huku kwa Brown ni miaka kazaa sasa sijadokoa nje,hii ni ktukana na mazingira halisi ya huku.kazi sana,ukirudi nyumbani umechoka, hali ya kifedha kwani kipato unachopata unatakiwa ulipe kodi kibao,chakula n.k,bado utajitahidi mwenzangu na mimi tuliotoka maisha duni kutuma vijisenti japo hata ndugu waweze kupata mlo ,huwezi kwenda bar kama huna hela kwani hata kama uko na marafiki bili ikija ni 50/50,Dada poa huku ni ghali kweli kweli ukifikiria kutoa paundi 150 ukikumbuka nyumbani unaona bora nitume huu mshiko home,weather is a critical factor pia kwani baridi inavyokung"uta ukitoka job unawaza kufika home shala.

In general kuna factors nyingi lakini mpaka hapo umepata picha flani,hakuna kitu kizuri katika maisha kama kuwa so busy and tight kwani wazo la ngono litakuja pale uko na mkeo
 
Kingingine labda ni hali ya sasa ambapo imekosekana athari ya moja kwa moja ya jamii husika kwa mtendaji wa jambo lolote lisilokubalika.

wote tunajua ngono zembe si jambo zuri kijamii.

Zamani mtendaji wa jambo hili alitengwa au aliadhibiwa kwa staili thabiti ya jamii husika.

Hii ilikuwa funzo kwa jamii iliobakia,siku hizi, watuhumiwa sugu, wagonjwa, watoto, wote wanapewa adhabu moja, kifungo bila kufiria zaidi, malengo ya adhabu au athari zingine.
 
Watumwa wa ngono ni wale tu malaya wanaofanya biashara ya ngono tu. wengine ni starehe kama mpenda kunywa bia, msoma novels etc etc etc
..Ni kweli starehe au hitaji muhimu kwa aliyekamilika??? some one to clarify please!!
 
Nilisikia toka kwa wazee wa kichaga kuwa ilikuwa ikijulikana kuwa kijana au msichana au mume au mke ametefaya ngono bila kufuata utaratibu uliokuwako(kufunda ndoa) walikuwa wanalazimishwa mwanaume kulalia mwanamke kifuani halafu wanachomwa mkuki mmoja mgongoni kwa mmoja unapenya hadi kutokezea mgongo wa mwingine. offcourse wanakufa, na wanaachwa porini, hakuna mazishi.

Ilikuwa ngumu sana kuona kitendo hicho kikifanyika kwani hakuna aliethubutu kuachia mawazo yake yatamani ngono zembe kwa hofu kubwa.
 
..Ni kweli starehe au hitaji muhimu kwa aliyekamilika??? some one to clarify please!!

...Kwa mujibu wa vitabu vya kidini, ni starehe na hitaji muhimu kwa waliooana tu. Namini hata wale wasio na dini, (wenye imani nyingine) pia wanataratibu zao za jambo hili.

Hakuna Mtumwa wa Ngono, ni ukosefu tu wa nidhamu ya mwili wako, kama sio 'ugonjwa' wa akili!
 
Sasa kama we uko ndani ya ndoa halafu unataka kila siku kama chakula nawe utaitwaje? au ni jina hili hili mtumwa wa ngono?
 
nafikiri mazingira na umaskini unachangia sana utumwa wa ngono,nikitoa mfano hai mimi wakati niko nyumbani bongo nilitawaliwa na huo utumwa lakini tangu nije huku kwa Brown ni miaka kazaa sasa sijadokoa nje,

Sasa huu ndio ufisadi wa maneno, miaka kadhaa (Kazaa), mhhh, kwa hiyo unataka kutuambia nini hapa,ulikuwa unajishusha mnazi nini au mhhhhh,kwa maana kama unakula vizuri, nadhani hormones lazima zirespond hata kama uko busy vipi, busy several years! una ED nini?
 
sasa huu ndio ufisadi wa maneno, miaka kadhaa (Kazaa), mhhh, kwa hiyo unataka kutuambia nini hapa,ulikuwa unajishusha mnazi nini au mhhhhh,kwa maana kama unakula vizuri, nadhani hormones lazima zirespond hata kama uko busy vipi, busy several years! una ED nini?

... GROW Up !!
 
... unataka kutuambia nini hapa,ulikuwa unajishusha mnazi nini au mhhhhh,kwa maana kama unakula vizuri, nadhani hormones lazima zirespond hata kama uko busy vipi, busy several years! una ED nini?



:)...duuuuh! salaaaale, hivi una matani na huyu jama wewe? ha ha ha haaa...
 
sasa kama we uko ndani ya ndoa halafu unataka kila siku kama chakula nawe utaitwaje? au ni jina hili hili mtumwa wa ngono?

Ubavu wa kufanya mapenzi au ngono unatofautiana kati ya mtu na mtu. Kuna wengine wanaweza kujipiga mara tatu hadi nne kwa siku kama SO 'haumwi kichwa' au 'kachoka' na kama SO yuko fit anafurahia hali hiyo maana anaona uwezekano wa SO kuwa anashughulika nje ni mdogo maana yuko busy na SO mtindo mmoja. Na kuna wengine akijipiga mara mbili kwa ametosheka kabisa. Kwa hiyo yule mwenye ubavu wa kupiga raundi tatu au nne kwa siku tuimuone kama ni mtumwa wa ngono, bali anatumia vizuri uwezo wake aliojaliwa na Mungu bila kutumia Viagra, Cialic au mkuyati
 
sasa kama we uko ndani ya ndoa halafu unataka kila siku kama chakula nawe utaitwaje? au ni jina hili hili mtumwa wa ngono?

Zombi nadhani umenielewa maana yangu. hawa wengine wanataka kuruka mada. nimesema kufikiria ngono kila mara ni matatizo, hata kama mko kwenye ndoa. hivi wanataka kusema ndoa ni kufanya mapenzi tu kila mara? hakuna mengine ya kuwaza ama kupanga?

Tena basi kama mtu aliye kwenye ndoa anapenda kufanya tendo hilo kila wakati nadhani ana matatizo, ya kiakili. hata wataalamu wanashauri kwamba, ili tendo hilo liwe la kuvuta na lenye maana stahili, ni lazima kupanga wewe na mwenza wako, walau mara tatu kwa wiki.

Kwa sababu wanasema bao moja ni sawa na kukimbia kilometa tisa. sasa bora ukimbie utakuwa umeupa mwili mazoezi, lakini fikiria kuzipoteza nguvu zote kitandani au weherever. na je, mwanamke akiwa ametembelewa na mgeni wa 'koti jekundu' na nyie ama wewe umeshazowea kila siku kudandia inakuwaje?

Wengine huchukua hata wiki nzima, sasa kipindi hiki mnafanyaje? au ndo utaamua kuogelea hivyo hivyo? hata vitabu vya dini vinakataza mwanamke kuingiliwa akiwa katika hali hiyo.
 
kuna pepo la ngono ... likikupata basi ... ukikosa mwanamke hata mtoto utamkamata au hata mbuzi, mbwa, ngombe na kadhalika kwa wanaume ... kwa wanawake hata mtu asiye na hadhi unaweza ukajikuta kakuparamia, tena huoni aibu hata ndugu au nani .. yeyote atakae jitokeza ukiwa na kiu ni lazima akutimizie, mwengine asipopata wanaume watatu kwa siku bado hajafanya kitu ... hii si kwamba analipwa la .... ila baada ya kitendo unajutia nafsi yako na kujilaumu na hata kujiuliza nimekutwa na nini ... mtu kama huyu kweli nimefanya nae tendo ... inakuwa too late .. na kama hujapata mtu unakuwa kama mwehu unaweza ukahaha mji mzima bila kuchoka ... yani mpaka unadhalilika .... nimeshakutana na mtu kama huyu .. huwa analia machozi kabisa kwa aibu ..... Subhanallah ... Mwenyezi Mungu atulinde sisi na watoto wetu na mapepo ya aina yoyote ile
 
Duh kazi kweli kweli wengine ni hobby yao kupenda sana NGONO wengine ni kutimiza matakwa ya mwili,wengine hawataki kabisa kusikia NGONO kwa hiyo miili inatofautiana.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom