#COVID19 Ni kweli hizi chanjo milioni moja hazina muda wa kuharibika (expiry date) hata ikifika mwakani? Kwanini hili suala haliwekwi wazi?

Leak

JF-Expert Member
Feb 22, 2012
52,202
42,061
Ni kweli hizi chanjo zilizo letwa wiki tatu zilizopita hazina muda wa kuharibika?

Kati ya mambo ambayo yamewashinda kabisa wizara ya afya kwenye hili chanjo ya COVID ni kuweza kutoa elimu sahihi kwa wanchi kuhusu hii chanjo na katika hili wizara imekuwa ikikimbia maswali ya watu kwa kudhani kila anayeuliza maswali basi anapinga chanjo.

Suala la muda wa kutumika kwa chanjo husika baada ya kuletwa limekuwa likiulizwa sana japo halijawai kupata majibu yake kwani tumekuwa tukiona nchi zingine wakimwaga baadhi ya chanjo baada ya kuisha muda wake wa kutumika.

Hivi ni kweli Johnson & Johnson haina expire date?

Na kama ina expire date au muda wa kuisha matumizi kwanini haiwekwi wazi?

Ni kweli hizi chanjo million moja hata zikikaa hadi mwakani bado zitakuwa ni safi kwa matumizi ya binadamu?
 
Hata Mimi nimewaza hilo... .halafu pia chanjo milion moja ni kidogo sana ukilinganisha na idadi yetu, kwaio nilitegemea ziwe zimeisha lakini waliochanja ni laki mbili tu
 
Pia chanjo zinabidi kuwekwa ktk mazingira fulani ambayo hayazifanyi ziharibike. Yaani kama ni joto lisizidi kiwango fulani au kama ni ubaridi usipungue kwa kiasi fulani. Vipi hayo yote yanazingatiwa au zimewekwa kama dozi tu za "kwinini"?
 
kwani kuna mtu asiwe daktari ataruhusiwa kushika kile kichupa cha chanjo ambako kunakaa expire date?
 
Kule Kenya kuna Chief secretary of Health Mugai kila siku anaita waandishi wa habari anatangaza hali ya maambukizi idadi ya watu, watu waliopona, maendeleo ya ugawaji chanjo, Takwimu zote kuhusu afya kwa usahihi maana kisheria ni yeye kazi yake lakini hapa Dr molle au Gwajima ni moja ya kazi zao ikiwemo kujibu maswali kama ulilouliza la chanjo kuisha muda wake.

Wabongo sijui nani katuloga yaani mtu anapewa kazi lakini hatimizi majukumu yake ila akijisikia kuibuka na spinning story utaina huyo kaita press. Haikuwa sahihi sana Shaka kumjibu ulimwengu ilihitajika Haniu Jaffar ndio ajibu hizi hoja za kina mnyika na wengineo. Hakuna uwajibikaji watu wanakula tu mishahara ya bure na kuota mabega.
 
Kule Kenya kuna Chief secretary of Health Mugai kila siku anaita waandishi wa habari anatangaza hali ya maambukizi idadi ya watu, watu waliopona, maendeleo ya ugawaji chanjo, Takwimu zote kuhusu afya kwa usahihi maana kisheria ni yeye kazi yake lakini hapa Dr molle au Gwajima ni moja ya kazi zao ikiwemo kujibu maswali kama ulilouliza la chanjo kuisha muda wake...
Nashangaa mtu akiulizwa swali kama hili anakimbilia kusemwa kuwa ni mpinga chanjo
 
Pia chanjo zinabidi kuwekwa ktk mazingira fulani ambayo hayazifanyi ziharibike. Yaani kama ni joto lisizidi kiwango fulani au kama ni ubaridi usipungue kwa kiasi fulani. Vipi hayo yote yanazingatiwa au zimewekwa kama dozi tu za "kwinini"?
Hadi leo huwa najiuliza kwani gwajima na Mollel hawajibu haya maswali?
 
Sijui kuhusu hizo za J&J, ila kwa AstraZeneca, zinahitaji mazingira flani ya hali joto. Na zimewekewa ka sensor kanatuma info muda wote kuhusu temperature, kana record baadae zinahamishiwa kwa computer.

Na vinakaa vichupa 10, ili kufungua hako lazima kuwe na idadi ya watu kumi vinginevyo vinavyobaki ni hasara.

Hii inamaana ni muhimu sana kuzingatia expire date na mazingira zinapotunzwa hizo chanjo.
 
Back
Top Bottom