Muulize Hamad Rashid ni kweli Jimboni kwake ameshindwa kuanzisha shule ya sekondari hata moja zilizopo ni zile tangu mkoloni?
Pili kwanini hakai jimboni kwake maisha yake yapo Dar? je , haoni kwamba hawatendei haki wapiga kura wake?
Tatu ni kweli alikuwa ameshashindwa kura za maoni za jimboni kwake Seif ndiye aliyemuokoa? Nne Hanatashawishi vipi kusema democrasia haijatumika na wakati kati ya wajumbe 25 wa bara 23 walihafiki kufukuzwa kwake naye anadai Bara wanampenda?
Mwisho ni kweli kwamba kuendelea kuwa katika uongozi wa CUF kwa muda mrefu Seif alijitahidi kuwashawishi wanachama wakukubali wakati wengi walikuwa hawana imani nawe kwa vile mke wako ni Afisa wa usalama wa taifa?
ikiwezekana picha au movie clips tuwekeeni tuone jinsi jamaa wanavyojichanaMasuala mujarabu kabisaa. Na kwa kuongezea baada ya swala ya ijumaa watu kule WAWI leo wanakula halua kushangilia kufukuzwa kwake.
Hayo ndo maswali ya waandishi wa tz. Yaani hivi vyuo ni vya kuchomwa moto vyote. Utakuta mpiga desa ndo anabaki kuwa lecturer. Ivi swali la heading yako(japo sijasoma ulichoandika ndani) ukimuuliza HR, unategemea atakujibu nini? Jana pia saa 3 usiku TBC1,nilikereka na kile kipindi maalumu ya wanajeshi kupandisha mwenge K/njaro, yani mtu anauliza maswali ya kiuoga ambayo, hata mtoto wa darasa la 2c anajibu.