Ni kweli Chama cha Mapinduzi(CCM) kitaendelea kutawala hadi tutakapopata vyama vya upinzani

kajekudya

JF-Expert Member
Sep 24, 2015
2,469
4,903
Siku chache zilizopita mkuu wa Kaya alitoa kauli ambayo ilipokelewa kwa hisia tofauti tofauti na wadau wa siasa, ni pale aliposema kuwa CCM itatawala milele.


Anaweza akawa hayupo sahihi kwani mambo yanabadilika na watu wanabadilika lakini kitu ambacho Kiko wazi kabisa ni kwamba CCM itaendelea kuitawala nchi hii hadi pale tutakapopata vyama vya siasa.

Ukweli mchungu ni kuwa tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi hatujawahi kuwa na vyama vya siasa kwa upande wa upinzani, bali tumekuwa tuna watu binafsi ambao kwa nyakati tofauti wamekuwa wakija na kuondoka. Ni bahati mbaya utamadumi wa nchi yetu, wananchi na mfumo( decision makers) unaonekana kutokubaliana na aina hii ya siasa za upinzani na kwa hili hata Kama hayo yote uanayosemwa kuwa mazingira magumu kwa vyama vya upinzani yakirekebishwa bado upinzani uliopo sasa hauwezi kushinda uchaguzi.

Tanzania ni taifa lililokamilika ni tofauti na Kenya, Uganda karuwanda au Kaburundi ambapo mtu mmoja mwenye nguvu au umaarufu ni rahisi watu na mfumo kumkubali unahitaji zaidi ya umaarufu na nguvu za kisiasa kuwa Rais wa Nchi hii na hapa Swala la Chama Chenye uimara kuanzia kimuundo na kimdumo bila kusahau aina na idadi ya wanachama ni mhimu.
Mrema alikataliwa, Silla alijitahidi Lowassa alikataliwa, Lissu atakataliwa, Zitto atakataliwa na hata angeletwa bwana Yesu hapa nawaapia atakataliwa tu.

Huu ndo ukweli mchungu, hivi ndivyo Taifa hili lilivyo ndivyo lilivyodizainiwa na ile ufanikiwe lazima ukubaliane na hali hii, lazima uje na muundo unaokubalika na kwa maana hiyo lazima the so called vyama vya siasa vilione hili waachane na kasumba ya kujenga watu maarufu bali watengeneze vyama vyenye mifumo na miundo imara na inayoeleweka bila kusahau watu Imara na wanaoaminika.

Watanzania, utamduni na mfumo wa nchi hii haitaki akina Kabwe, Akina Lissu au akina Lowassa, Wanataka ACT, CHADEMA, NCCR na CUF zilizo imara ndio maana Lowassa Leo Ikulu anaiskia hewani huku Anko akiwa anapunga upepo mle ndani, kabla ya July 2015 inawezekana ilikuwa hata siyo rahisi kwa Anko kupata nafasi ya kusalimiana na Lowassa, walikuwa ni mbingu na Nchi, lakini utamaduni, watanzania na mfumo vilimkataa mzee wa Monduli kwakuwa tu tu hakuwa ndani ya Chama, Hii ni Nchii, huwezi kupewa tu tuma unavopewa gari au shamba.

Kitu kimoja ambacho lazima tutambue, Watanzania na mfumo ndo watu wenye dhamana ya kuamua nani awe Rais na Wala si wanaCCM na sio kwamba watanzania au mfumo wanakipendelea Chama Cha Mapinduzi ukweli ni kwamba Chama Cha Mapinduzi ndo Chama pekee kinachokizi matakwa ya utamaduni, matakwa ya watanzania na mfumo.

Mwenyekiti Mbowe alijitahidi Sana kukijenga Chama Cha Democrasia na Maendeleo ili kukidhi mahitaji haya, bahati mbaya akaingiwa na tamaa, akaanza kugombana na vijana wake na hitimisho lilikuwa mwaka 2015, CHADEMA ya mwaka 2005-2010, Kama ingeendelea kulelewa vizuri pengine 2025 kwa Mara ya kwanza tungekuwa na vyama viwili vya siasa na hivyo kuwapatia uwanja mpana Watanzania na Mfumo
kuamua nani wa kumpa Dora bahati mbaya safari hii ya matumaini iliyoanza mwaka 2003-2004 imeishia ukingoni mnamo mwaka 2015 na hakuna jitihada zozote zinaonekana kujaribu tene kujenga Chama katika namna ambayo inakidhi matakwa ya utamaduni wa Nchi hii, wanatanzania wenyewe na mfumo, wanarukaruka tu.


Narudia na huu ni ukweli Mchungu hadi tutakapopata vyama vya upinzani ndipo utawala wa CCM utakapokoma, Zitto, Lissu, sijui Lowassa hawawezi kushindana na CCM halafu wategemee kupewa Nchi, Watanzania si wajinga, hii si Nchi inayoweza kuongozwa Kama Kashamba tuu ka mtu, hv Leo Zitto, Lissu au Mbowe akipewa Nchi na hutu tu vyama twao nani atawafung speed gavornor, kwa sababu Rais ni kiongozi mkubwa na ambaye maamuzi yake Yana athari kubwa kwa taifa hili, hivyo lazima atokane na Chama kinachoelelweka, chenye mifumo na taasisi Imara na chenye watu Imara wanaoaminika na kufahamika vyema na amabao wanaweza hata kumkemea hata Rais mwenyewe, ka ACT au KaCHADEMA ambapo hakawezi kumkemea au kumkosoa Zitto au Mbowe Leo kanawezaje kesho akiwa Rais.

Mwisho kabisa acheni kuwalaumu Watanzania na mfumo, jengeni vyama vyenu vikizi matakwa mtapewa Nchi, CCM hawana hati miliki ya Nchi hii Bali ndo Chama pekee kinachokizi vigezo kwa sasa.
 
Ungeweza kumshauri rais wako hiki ningekuona wamaana sana ,kwasababu rais wako anapiga wapinzani risasi ,kazuia mikutano ya siasa ,anawapa kesi wapinzani n.k

So mwambie asifanye hvyo ,upinzani hakuna? ,ccm itatawala milele.
 
Risasi,kesi,kupotezwa watanzania ndo et siasa za huyo mtu wako.
Stupid intellectual at the hill.
 
Ungeweza kumshauri rais wako hiki ningekuona wamaana sana ,kwasababu rais wako anapiga wapinzani risasi ,kazuia mikutano ya siasa ,anawapa kesi wapinzani n.k

So mwambie asifanye hvyo ,upinzani hakuna? ,ccm itatawala milele.
Wasiwasi wangu sijui Kama hata umeelewa nilichojiandika!
 
Ni bahati mbaya utamadumi wa nchi yetu, wananchi na mfumo( decision makers) unaonekana kutokubaliana na aina hii ya siasa za upinzani na kwa hili hata Kama hayo yote uanayosemwa kuwa mazingira magumu kwa vyama vya upinzani yakirekebishwa bado upinzani uliopo sasa hauwezi kushinda uchaguzi.
Niliposoma hii para nikagundua tu yaleyale sasa kma wananchi wamewakataa upinzani kwanni nguvu nyingi zinatumika kwenye chaguzi?? Kwanni mnazuia mikutano yao?? Kwanni mlikataa mabadiliko ya sheria za uchaguzi??

Siku katiba ikibadilishwa ndio tutajua ukweli... Mfano tu zanzibar mtu ameshinda hakutangazwa hapo mtasemaje?? Wananchi wamewakataa pia

Kwa mawazo haya itachukua miaka 100 kufikia nchi ya viwanda
 
Niliposoma hii para nikagundua tu yaleyale sasa kma wananchi wamewakataa upinzani kwanni nguvu nyingi zinatumika kwenye chaguzi?? Kwanni mnazuia mikutano yao?? Kwanni mlikataa mabadiliko ya sheria za uchaguzi??

Siku katiba ikibadilishwa ndio tutajua ukweli... Mfano tu zanzibar mtu ameshinda hakutangazwa hapo mtasemaje?? Wananchi wamewakataa pia

Kwa mawazo haya itachukua miaka 100 kufikia nchi ya viwanda
Nawe pia ni wale wale, endeeleni kulalamika hivyo hivyo!
 
Pia wasiwasi wangu kama wewe ulishndwa kupnga makonda kuvamia clouds pia utashndwa kuelewa kwanini wapnzani wanapnga risasi!!!
Ungekaa tu kimya mkuu, mm nadhani andiko limemuzidi kimo!! Unayoyaandika hata hayahusiani na nilichokiandika!
 
Siku chache zilizopita mkuu wa Kaya alitoa kauli ambayo ilipokelewa kwa hisia tofauti tofauti na wadau wa siasa, ni pale aliposema kuwa CCM itatawala milele.


Anaweza akawa hayupo sahihi kwani mambo yanabadilika na watu wanabadilika lakini kitu ambacho Kiko wazi kabisa ni kwamba CCM itaendelea kuitawala nchi hii hadi pale tutakapopata vyama vya siasa.

Ukweli mchungu ni kuwa tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi hatujawahi kuwa na vyama vya siasa kwa upande wa upinzani, bali tumekuwa tuna watu binafsi ambao kwa nyakati tofauti wamekuwa wakija na kuondoka. Ni bahati mbaya utamadumi wa nchi yetu, wananchi na mfumo( decision makers) unaonekana kutokubaliana na aina hii ya siasa za upinzani na kwa hili hata Kama hayo yote uanayosemwa kuwa mazingira magumu kwa vyama vya upinzani yakirekebishwa bado upinzani uliopo sasa hauwezi kushinda uchaguzi.

Tanzania ni taifa lililokamilika ni tofauti na Kenya, Uganda karuwanda au Kaburundi ambapo mtu mmoja mwenye nguvu au umaarufu ni rahisi watu na mfumo kumkubali unahitaji zaidi ya umaarufu na nguvu za kisiasa kuwa Rais wa Nchi hii na hapa Swala la Chama Chenye uimara kuanzia kimuundo na kimdumo bila kusahau aina na idadi ya wanachama ni mhimu.
Mrema alikataliwa, Silla alijitahidi Lowassa alikataliwa, Lissu atakataliwa, Zitto atakataliwa na hata angeletwa bwana Yesu hapa nawaapia atakataliwa tu.

Huu ndo ukweli mchungu, hivi ndivyo Taifa hili lilivyo ndivyo lilivyodizainiwa na ile ufanikiwe lazima ukubaliane na hali hii, lazima uje na muundo unaokubalika na kwa maana hiyo lazima the so called vyama vya siasa vilione hili waachane na kasumba ya kujenga watu maarufu bali watengeneze vyama vyenye mifumo na miundo imara na inayoeleweka bila kusahau watu Imara na wanaoaminika.

Watanzania, utamduni na mfumo wa nchi hii haitaki akina Kabwe, Akina Lissu au akina Lowassa, Wanataka ACT, CHADEMA, NCCR na CUF zilizo imara ndio maana Lowassa Leo Ikulu anaiskia hewani huku Anko akiwa anapunga upepo mle ndani, kabla ya July 2015 inawezekana ilikuwa hata siyo rahisi kwa Anko kupata nafasi ya kusalimiana na Lowassa, walikuwa ni mbingu na Nchi, lakini utamaduni, watanzania na mfumo vilimkataa mzee wa Monduli kwakuwa tu tu hakuwa ndani ya Chama, Hii ni Nchii, huwezi kupewa tu tuma unavopewa gari au shamba.

Kitu kimoja ambacho lazima tutambue, Watanzania na mfumo ndo watu wenye dhamana ya kuamua nani awe Rais na Wala si wanaCCM na sio kwamba watanzania au mfumo wanakipendelea Chama Cha Mapinduzi ukweli ni kwamba Chama Cha Mapinduzi ndo Chama pekee kinachokizi matakwa ya utamaduni, matakwa ya watanzania na mfumo.

Mwenyekiti Mbowe alijitahidi Sana kukijenga Chama Cha Democrasia na Maendeleo ili kukidhi mahitaji haya, bahati mbaya akaingiwa na tamaa, akaanza kugombana na vijana wake na hitimisho lilikuwa mwaka 2015, CHADEMA ya mwaka 2005-2010, Kama ingeendelea kulelewa vizuri pengine 2025 kwa Mara ya kwanza tungekuwa na vyama viwili vya siasa na hivyo kuwapatia uwanja mpana Watanzania na Mfumo
kuamua nani wa kumpa Dora bahati mbaya safari hii ya matumaini iliyoanza mwaka 2003-2004 imeishia ukingoni mnamo mwaka 2015 na hakuna jitihada zozote zinaonekana kujaribu tene kujenga Chama katika namna ambayo inakidhi matakwa ya utamaduni wa Nchi hii, wanatanzania wenyewe na mfumo, wanarukaruka tu.


Narudia na huu ni ukweli Mchungu hadi tutakapopata vyama vya upinzani ndipo utawala wa CCM utakapokoma, Zitto, Lissu, sijui Lowassa hawawezi kushindana na CCM halafu wategemee kupewa Nchi, Watanzania si wajinga, hii si Nchi inayoweza kuongozwa Kama Kashamba tuu ka mtu, hv Leo Zitto, Lissu au Mbowe akipewa Nchi na hutu tu vyama twao nani atawafung speed gavornor, kwa sababu Rais ni kiongozi mkubwa na ambaye maamuzi yake Yana athari kubwa kwa taifa hili, hivyo lazima atokane na Chama kinachoelelweka, chenye mifumo na taasisi Imara na chenye watu Imara wanaoaminika na kufahamika vyema na amabao wanaweza hata kumkemea hata Rais mwenyewe, ka ACT au KaCHADEMA ambapo hakawezi kumkemea au kumkosoa Zitto au Mbowe Leo kanawezaje kesho akiwa Rais.

Mwisho kabisa acheni kuwalaumu Watanzania na mfumo, jengeni vyama vyenu vikizi matakwa mtapewa Nchi, CCM hawana hati miliki ya Nchi hii Bali ndo Chama pekee kinachokizi vigezo kwa sasa.
Another moron person
 
Kwa sababu nilichoandika na ulichocomment hata havina uhusiano! Umenikumbusha ile hadithi ya sijaramba Sukari mkuu!
Hahahaaa mkuu mie si mwanafunzi wa kulala darasani.Andiko lako lipo kindumila kuwili.Unang'ata na kupuliza ndo maana tunakupinga.Ukweli ni kwamba wote tunajua jinsi siasa za kishindani zinaenda Duniani.Sasa unapokuja na hoja et vyama vingine havina mfumo Sisi tuñapinga kwani mifumo ipo na madhubuti kabisa ndo maana hao walio madarakani wanatumia njia dhalimu za kuua.Ili watu waogope na kisha mifumo hiyo isizidi kuwa imara zaidi ktk kwenda kutawala.Umeelewa Sasa ee?
 
Hahahaaa mkuu mie si mwanafunzi wa kulala darasani.Andiko lako lipo kindumila kuwili.Unang'ata na kupuliza ndo maana tunakupinga.Ukweli ni kwamba wote tunajua jinsi siasa za kishindani zinaenda Duniani.Sasa unapokuja na hoja et vyama vingine havina mfumo Sisi tuñapinga kwani mifumo ipo na madhubuti kabisa ndo maana hao walio madarakani wanatumia njia dhalimu za kuua.Ili watu waogope na kisha mifumo hiyo isizidi kuwa imara zaidi ktk kwenda kutawala.Umeelewa Sasa ee?
Mkuu Chama kipi tofauti na CCM!?
 
Nawe pia ni wale wale, endeeleni kulalamika hivyo hivyo!
Ni vizuri ukijibu hoja maana umeleta mada.... Nimeuliza maalim seif alipofutiwa matokeo alikuwa amekataliwa na wananchi kisa chama hakina MFUMO MZURI kama CCM??

Kingine nipe sababu moja ya wananchi kuipigia kura CCM hii hii ambayo kwa miaka 50 haikufanya lolote zaidi ya kuleta ufisadi na umasikini
 
Mkuu Chama kipi tofauti na CCM!?
Mkuu nakuhakikishia CHADEMA ipo madhubuti.Usitishwe na aina ya watu waliohamia huko.Hata wasingekuwepo ipo madhubuti na ina mfumo imara na inaweza kuendesha nchi Kwa ufanisi wa hali ya juu.Na haijadhoofu wala kufa,katika kukuthibitishia hili fanya tathimini ya namna inafanyiwa ktk chaguzi zote.Ni hujuma na mabavu tuu.Hebu fikilia mkuu kama ingekuwa tuna tume HURU KABISA, KATIBA ILIYO SAWA.na utawala wa Sheria unafuatwa ingekuwaje ktk matokeo ya chaguzi? Tafakari tu hayo mkuu then utaniambia.Japo waweza endelea kuamini vile unaamini Kaka.
 
Ni vizuri ukijibu hoja maana umeleta mada.... Nimeuliza maalim seif alipofutiwa matokeo alikuwa amekataliwa na wananchi kisa chama hakina MFUMO MZURI kama CCM??

Kingine nipe sababu moja ya wananchi kuipigia kura CCM hii hii ambayo kwa miaka 50 haikufanya lolote zaidi ya kuleta ufisadi na umasikini
Jipe nafasi ya kusoma between lines na kuelewa badala ya kukurupuka, ungekuwa umeelewa usingekuwa unauliza these fuki...stupid questions!
 
Ungekaa tu kimya mkuu, mm nadhani andiko limemuzidi kimo!! Unayoyaandika hata hayahusiani na nilichokiandika!
Ungekaa kimya pia na wewe ningekuona wamaana sana ,kama afanyavyo rais wako juu ya matukio ya wapinzani.lakini ile la mtoto wake makonda kwenye clouds aliliongelea mpka kwenye media so ungeweza kumuuliza magu ungeweza kupata mjibu mazri ya mada yako.
 
Back
Top Bottom