Ni kweli Burundi ilitaka kuunganika na Tanganyika ilivyopata Uhuru na ingekuwa sehemu ya Tanganyika?

chizcom

JF-Expert Member
Jul 31, 2016
7,581
15,709
Jana Julai mosi, wananchi wa Burundi waliadhimisha miaka 60 tangu nchi yao ilipojipatia uhuru wake kutoka kwa wakoloni wa Ubelgiji Jumapili ya Julai mosi, 1962. Mwaka moja kabla ya siku ya uhuru kulikuwa na uchaguzi wa kwanza chini ya usimamizi wa Umoja Mataifa na chama kilichoshinda katika uchaguzi huo UPRONA kilichoongozwa na mwanamfalme Mtutsi Louis Rwagasore, aliyemuoa mwanamke wa Kihutu na chama kiliunganisha pande zote mbili.

Hata hivyo, Jumamosi ya Oktoba 13, 1962 Rwagasore aliyefikiriwa kuwa alikuwa anajenga uelewano wa kuishi pamoja kati ya Watutsi na Wahutu, aliuawa. Kifo chake kilikatisha ndoto ya shirikisho la Tanganyika na Burundi alilokuwa nalo Mwalimu Julius Nyerere.

Tanganyika ilipata uhuru Desemba 9, 1961 na baadaye ikawa Jamhuri Desemba 1962. Baada ya Uhuru wa Tanganyika katika hotuba yake kwa mkutano wa mwaka wa chama cha Tanu mwaka 1962, Mwalimu Nyerere alionyesha wazi kufadhaishwa kwake kulikotokana na mauaji ya Rwagasore.

Soma zaidi Gazeti la Mwananchi leo Jumamosi Julai 2,2022

IMG_7930.jpg
 
Warundi ni ndugu zetu wa damu kabisa kuliko Wanyarwanda. I love these people. Hongereni sana Warundi kwa kuadhimisha miaka 60 ya uhuru wenu.

Mwenyezi Mungu aendelee hivyo hivyo kuwajalia moyo wa kuwaona Watanganyika kama ndugu zenu wa damu. Hakika nyinyi ni watu msio na makuu, majivuno na kujimwambafai kama Wanyarwanda.
 
Wangeungana nasi yale mauji aidha yasinge kuwa makubwa au Tanganyika kwa hekima yasinge tokea...
Pia kuna uwezekano mauaji yangekuwa makubwa zaidi kwa hao warundi kuchochea uhasama baina ya makabila mengine hasa yale yanayoishi eneo moja.

Kila jambo hutokea kwa sababu zake, pengine tumeepushwa na kubwa zaidi kwa kutoungana kwetu.
 
Warundi ni ndugu zetu wa damu kabisa kuliko Wanyarwanda. I love these people. Hongereni sana Warundi kwa kuadhimisha miaka 60 ya uhuru wenu.

Mwenyezi Mungu aendelee hivyo hivyo kuwajalia moyo wa kuwaona Watanganyika kama ndugu zenu wa damu. Hakika nyinyi ni watu msio na makuu, majivuno na kujimwambafai kama Wanyarwanda.
Warundi ni ndugu zetu wa damu kabisa kuliko Wanyarwanda. I love these people. Hongereni sana Warundi kwa kuadhimisha miaka 60 ya uhuru wenu.

Mwenyezi Mungu aendelee hivyo hivyo kuwajalia moyo wa kuwaona Watanganyika kama ndugu zenu wa damu. Hakika nyinyi ni watu msio na makuu, majivuno na kujimwambafai kama Wanyarwanda.
Warundi ni ndugu zetu wa damu kabisa kuliko Wanyarwanda. I love these people. Hongereni sana Warundi kwa kuadhimisha miaka 60 ya uhuru wenu.

Mwenyezi Mungu aendelee hivyo hivyo kuwajalia moyo wa kuwaona Watanganyika kama ndugu zenu wa damu. Hakika nyinyi ni watu msio na makuu, majivuno na kujimwambafai kama Wanyarwanda.
Warundi ni ndugu zetu wa damu kabisa kuliko Wanyarwanda. I love these people. Hongereni sana Warundi kwa kuadhimisha miaka 60 ya uhuru wenu.

Mwenyezi Mungu aendelee hivyo hivyo kuwajalia moyo wa kuwaona Watanganyika kama ndugu zenu wa damu. Hakika nyinyi ni watu msio na makuu, majivuno na kujimwambafai kama Wanyarwanda.
Mi mwenyewe ningefurahi sana kama nchi za Kongo na Burundi zigekuwa sehemu yetu
 
Warundi ni ndugu zetu wa damu kabisa kuliko Wanyarwanda. I love these people. Hongereni sana Warundi kwa kuadhimisha miaka 60 ya uhuru wenu.

Mwenyezi Mungu aendelee hivyo hivyo kuwajalia moyo wa kuwaona Watanganyika kama ndugu zenu wa damu. Hakika nyinyi ni watu msio na makuu, majivuno na kujimwambafai kama Wanyarwanda.
I'll nasiki Ni wauaji sna
 
Mi naonaga Burundi na Rwanda ni mikoa tu ya Tanzania, hivi nchi inakuwaje kadogo kama vingunguti? Ni nchi gani hiyo?
Unajua ukubwa wa nchi Singapore ni kmsq 728.6 tu (yaani Mia saba ishirini na usheee hapo, hawana hata kilomita za mraba buku? Na population Yao Ni watu mil 5.6 huku GDP Yao Ni $340bil.

Ni shiiiiiiiiiiiiida.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom