manning
JF-Expert Member
- Apr 1, 2013
- 5,044
- 11,690
Baraa hili ambalo tayari limeshapitia nchi kadhaa zinazoizunguka Tanzania baadhi ya watu wanasema sasa ni zamu ya Tanzania kukumbwa nalo.
Janga hili lilianzia miaka kadhaa huko nyuma kwa kukikumba chama cha UPC (Uganda people's congress) na kukisababishia kifo ambacho hakikutarajiwa. Baada ya kupumua kwa muda, baraa hili liliwavamia majirani wa Tanzania wanaoishi kuzini magharibi Zambia na huko likakiteketeza chama cha UNIP (United national independent party) Baada ya kusababisha mazara hayo huko Zambia na kusababisha baadhi ya viongozi wake kusota kwa muda mbele ya Nondo mpaka Mwl Nyerere akawaombea msamaha, baraa hilo lilihamia Kenya.
Hapo Kenya bila Huruma lilikifumuafumua chama cha KANU (Kenya African national Union) mpaka sasa wote mnajua mazishi yake yalivyofanyika.
Kwa sasa baadhi ya watabili wanasema Wazi kuwa ni Zamu ya Tanzania kukumbwa na zahama hiyo, na baadhi ( wengi wakiwa watanzania) wanatamka wazi kuwa mwaka 2015 baraa hilo haliepukiki Tanzania. Je utabili huu ni kweli utatimia baada ya Tanzania kuzungukwa tayari na baraa hili?
Janga hili lilianzia miaka kadhaa huko nyuma kwa kukikumba chama cha UPC (Uganda people's congress) na kukisababishia kifo ambacho hakikutarajiwa. Baada ya kupumua kwa muda, baraa hili liliwavamia majirani wa Tanzania wanaoishi kuzini magharibi Zambia na huko likakiteketeza chama cha UNIP (United national independent party) Baada ya kusababisha mazara hayo huko Zambia na kusababisha baadhi ya viongozi wake kusota kwa muda mbele ya Nondo mpaka Mwl Nyerere akawaombea msamaha, baraa hilo lilihamia Kenya.
Hapo Kenya bila Huruma lilikifumuafumua chama cha KANU (Kenya African national Union) mpaka sasa wote mnajua mazishi yake yalivyofanyika.
Kwa sasa baadhi ya watabili wanasema Wazi kuwa ni Zamu ya Tanzania kukumbwa na zahama hiyo, na baadhi ( wengi wakiwa watanzania) wanatamka wazi kuwa mwaka 2015 baraa hilo haliepukiki Tanzania. Je utabili huu ni kweli utatimia baada ya Tanzania kuzungukwa tayari na baraa hili?