Ni malaria gani ya namna hiyo ambayo hata Agha khan hawakuigundua? Mbona waandishi wa habari hawawahoji Agha khan ili waseme kwa nini vipimo vyao havikugundua Malaria ya Zito? Huyo daktari wa Muhimbili tu ndiye mtaalamu wa malaria kuliko madaktari wote wa Tanzania? Tukumbuke siasa za Tanzania kwa sasa ni chafu mno! Uwezekano wa madaktari kutumiwa kwa hujuma za kisiasa ni mkubwa pia! Kama ni kweli Agha khan walishindwa kugundua kuwa Zito alikuwa na malaria, basi ni bora hospitali ifungiwe au uongozi ujiuzulu! Tofauti na hapo, Tanzania bado tuna safari ndefu!