Ni kwanini watawala wetu wa CCM "wanaweweseka" Sana kuhusu ajali iliyotokea ya Precision Air?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,479
30,144
Kuliitishwa kikao cha dharula cha Baraza la mawaziri, kuongelea kitu kimoja pekee, ajali ya ndege ya Precision Air, iliyotokea zaidi ya wiki moja iliyopita!

Hata hivyo kilichonishangaza zaidi ni taarifa ya msemaji mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, baada ya kumalizika kwa kikao hicho, ambapo ametuomba watanzania tuwe watulivu, wakati huu ambapo Tume ya kuchunguza ajali hiyo inaendelea na uchunguzi wake!

Nimuulize Bwana Msigwa, hivi intelejinsia yao ndivyo inavyowaambia kuwa watanzania wanategemea kufanya vurugu, kuhusiana na ajali hiyo?🥺

Hivi hii ni mara ya kwanza, Taifa letu linapata ajali?

Mbona Kila mwezi, mabasi yetu yanaua mamia wa abiria huko barabarani, mbona hatujawahi sikia, hata mara moja, kikiitishwa kikao cha dharula cha Baraza la mawaziri, kujadili suala hilo?

Nchi hii kumewahi kutokea ajali nyingi Sana, majini na barabarani, zilizochukua uhai wa watanzania wenzetu kwa maelfu, lakini sijawahi kusikia Baraza la mawaziri likifanya kikao chake kwa njia ya dharula, kama ilivyotokea kwa ajali ya ndege ya Precision Air!

Najiuliza ni sababu zipi zinazowafanya watawala wetu wa CCM "waweseke" kiasi hiki kwa ajili ya ajali hii ya ndege ya Precision Air?

Kumewahi kutokea ajali nyingi tu na Tume mbalimbali zimeundwa na Serikali hii ya CCM, lakini matokeo yake hayajatolewa kwa Umma wa watanzania na badala yake ripoti hizo zimefichwa kwenye "makabati" ya watawala wetu wa CCM.

Kwa kuzitaja chache ya Tume hizo:-

1. Iliundwa Tume ya kuchunguza namna pesa "zilivyochotwa" huko BoT, baada ya kifo cha aliyekuwa Rais wetu, Hayati Magufuli, lakini hadi leo, taarifa hiyo haikutolewa kwa Umma wa watanzania na badala yake zikafichwa na watawala wetu.

2. Iliundwa pia Tume ya kuchunguza moto uliounguza soko la Kariakoo, lakini baada ya Tume hiyo kukamilisha Kazi yake na kukabidhi ripoti hiyo kwa watawala wetu, hatukusomewa yalibainika nini kwenye Tume hiyo.

3. Iliundwa pia Tume ya kuchunguza Mauaji ya mfanyibiashara wa madini huko Mtwara, Mussa Hamisi, ambapo inadaiwa aliuawa na Polisi na wakampora pesa zake za madini, zaidi ya shilingi milioni 70, hata hivyo matokeo ya Tume hiyo pia, hatukujulishwa watanzania.

Najiuliza hivi ni kwanini watawala wetu wameingia "kiwewe" kwa ajali hii ya ndege ya Precision Air?

Lakini jibu ninalolipata ni kuwa tofauti na Tume zilizopita, ambazo watawala wetu ndiyo waliokuwa wanaunda Tume hizo na baada ya Tume hizo kukamilisha uchunguzi wao, watawala wetu wamekuwa wakituficha, Ili tusijue nini kimebainika na Tume hizo.

Tokea ajali hiyo ya ndege ya Precision Air, iliyotokea zaidi ya wiki moja iliyopita, kumekuwa na shutuma nyingi kutoka kwa Umma wa watanzania, kuwa kulitokea uzembe wa Hali ya juu kwa vikundi vya uokoaji kutotimiza wajibu wao, hadi kusababisha vifo hivyo 19.

Kutokana na safari hii Tume ya uchunguzi kuwa ni huru, ambayo inawahusisha wataalamu waliotengeneza ndege hiyo ya Precision Air, kutoka Ufaransa, ndiko nadhani kumewatia "kiwewe" watawala wetu na hasa baada ya Tume hiyo kusema hadharani kuwa matokeo ya Tume hiyo yatatolewa baada ya wiki 2 tokea ajali hiyo ilipotokea na watawala wetu hawama "ubavu" wa kuizuia Tume hiyo isitoe taarifa yao kwa Umma
 
labda kwa sababu ni majaliwa jina la kijana ila kiufupi tanzania serikali hakuna na hipo ccm
 
Ajari hii imewaacha wengi mdomo wazi na wengi wamehoji bahati mbaya majibu hakuna, ajari inatokea 200m kutoka airport cha ajabu wanaofariki ni wengi, wananchi wanavuta ndege watu waliovalia magwanda ya jwtz wanapiga picha, walioshiriki kuokoa watu kwenye ajari ni wengi ila mmoja ndio anaonekana kufanya kazi kubwa, Kwa mujibu wa manusura rubani aliwatangazia hali ya hewa imebadirika cha ajabu hamna tafadhari zilizochukuliwa, ni mengi sana yanashangaza juu ya ajari hii ndiyo maana hata maelezo ya ya ya ya ya ya ya trap na trab wameshindwa kuyapika hivyo Msigwa anajitahidi kutuliza watu.
 
Ajari hii imewaacha wengi mdomo wazi na wengi wamehoji bahati mbaya majibu hakuna, ajari inatokea 200m kutoka airport cha ajabu wanaofariki ni wengi, wananchi wanavuta ndege watu waliovalia magwanda ya jwtz wanapiga picha, walioshiriki kuokoa watu kwenye ajari ni wengi ila mmoja ndio anaonekana kufanya kazi kubwa, Kwa mujibu wa manusura rubani aliwatangazia hali ya hewa imebadirika cha ajabu hamna tafadhari zilizochukuliwa, ni mengi sana yanashangaza juu ya ajari hii ndiyo maana hata maelezo ya ya ya ya ya ya ya trap na trab wameshindwa kuyapika hivyo Msigwa anajitahidi kutuliza watu.
Ni kweli kama alivyosema Katibu wa CCM wa uenezi, Bwana Shaka, kuwa kwa tukio hili, tumeushangaza Ulimwengu!😁
 
Ajari hii imewaacha wengi mdomo wazi na wengi wamehoji bahati mbaya majibu hakuna, ajari inatokea 200m kutoka airport cha ajabu wanaofariki ni wengi, wananchi wanavuta ndege watu waliovalia magwanda ya jwtz wanapiga picha, walioshiriki kuokoa watu kwenye ajari ni wengi ila mmoja ndio anaonekana kufanya kazi kubwa, Kwa mujibu wa manusura rubani aliwatangazia hali ya hewa imebadirika cha ajabu hamna tafadhari zilizochukuliwa, ni mengi sana yanashangaza juu ya ajari hii ndiyo maana hata maelezo ya ya ya ya ya ya ya trap na trab wameshindwa kuyapika hivyo Msigwa anajitahidi kutuliza watu.
Kinachonishangaza zaidi, ni kwanini utamaduni wa kuwajibika umetoweka Katika siku hizi hapa Tanzania?

Miaka ile ya 70, aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani, Mzee Alli Hassan Mwinyi, alijiuzuru uwaziri wake kutokana na Mauaji yaliyotokea huko Shinyanga, ingawa yeye binafsi hakuhusika moja kwa moja.

Ninashangaa hadi leo PM wetu, Kassim Majaliwa bado ameng'ang'ania ofisini kwake, licha ya kashfa hiyo iliolikumba Taifa letu kutokana na vifo hivyo vya watanzania wenzetu kutokana na ajali hiyo ya ndege
 
Hawa watu wanajishuku,huenda ni kafara wametoa ili waendelee kubaki madarakani
Ile Tume iliyoundwa na wataalamu wa ilikotengenezwa ndege nchini Ufaransa, wametuahidi kuwa ripoti yao, itakuwa tayari wiki ijayo.

Huenda ndiyo sababu, watawala wetu, wameingia "kihoro" chote hiki, kwa kuwa walizoea kuziweka "kabatini" ripoti zao🥺
 
No shida ya kiwewe chote , Wala sio ajali ya ndege mkuu, shida hapa ni serikali kutafuta agenda ili kuipaisha angalau saulisha mijadala mengine KWa watanzania Ili wapumue kidogo
KWa sasa nchi ni ya moto Kama vile tumetoka / tupo vitamin na hata wao pamoja wako pale hawajui washike lipi waache lipi KILA sehem pa hovyo kuliko wakati wowote ule, that's wanalazimika vipa umuhimu vitu vidogo uku wakifuata upepo,
Nchi ipo katika matatizo makubwa mno mfano
Mfumuko wa bei wa kutisha, shida ya maji, umeme,
Wizi mkubwa Sana wa fedha za umma ,
Mzunguko mdogo wa pesa n.k
 
Mbona huko barabarani, mabasi yetu yanaua mamia ya abiria kila mwezi, mbona hatujawahi sikia kikao cha dharula kikiitishwa, kuongelea ajali hizo?🥺
 
Kinachonishangaza zaidi, ni kwanini utamaduni wa kuwajibika umetoweka Katika siku hizi hapa Tanzania?

Miaka ile ya 90, aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani, Mzee Alli Hassan Mwinyi, alijiuzuru uwaziri wake kutokana na Mauaji yalivyotokea huko Shinyanga, ingwa yeye binafsi hskuhusika moja kwa moja.

Ninashangaa hadi leo PM wetu, Kassim Majaliwa bado ameng'ang'ania ofisini kwake, licha ya kashfa hiyo iliuolikumba Taifa letu kutokana na vifo hivyo vya watanzania wenzetu kutokana na ajali hiyo ya ndege
Mkuu, Acha kulisha watu matango pori na story zako za kusimuliwa.

Miaka ya 90 Mwinyi tayari alikuwa ni Rais. Hivyo hilo la kujiuzuru lilikuwa kabla ya 84 alipochaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar.

Halafu kudai kuwapo kwa utaratibu wa kujiuzuru huko nyuma ni upotoshaji. Mtu pekee aliyewahi kujiuzuru kwa kuwajibika ni Mzee Mwinyi, probably na Lowasa kwa Kashifa yake ya Richmond.

Kwa kuconclude ni kwamba huo utamaduni wa kujiuzuru hajawahi kuwepo Tanzania.
 
Kuliitishwa kikao cha dharula cha Baraza la mawaziri, kuongelea kitu kimoja pekee, ajali ya ndege ya Precision Air, iliyotokea zaidi ya wiki moja iliyopita!

Hata hivyo kilichonishangaza zaidi ni taarifa ya msemaji mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, baada ya kumalizika kwa kikao hicho, ambapo ametuomba watanzania tuwe watulivu, wakati huu ambapo Tume ya kuchunguza ajali hiyo inaendelea na uchunguzi wake!

Nimuulize Bwana Msigwa, hivi intelejinsia yao ndivyo inavyowaambia kuwa watanzania wanategemea kufanya vurugu, kuhusiana na ajali hiyo?

Hivi hii ni mara ya kwanza, Taifa letu linapata ajali?

Mbona Kila mwezi, mabasi yetu yanaua mamia wa abiria huko barabarani, mbona hatujawahi sikia, hata mara moja, kikiitishwa kikao cha dharula cha Baraza la mawaziri, kujadili suala hilo?

Nchi hii kumewahi kutokea ajali nyingi Sana, majini na barabarani, zilizochukua uhai wa watanzania wenzetu kwa maelfu, lakini sijawahi kusikia Baraza la mawaziri likifanya kikao chake kwa njia ya dharula, kama ilivyotokea kwa ajali ya ndege ya Precision Air!

Najiuliza ni sababu zipi zinazowafanya watawala wetu wa CCM "waweseke" kiasi hiki kwa ajili ya ajali hii ya ndege ya Precision Air?

Kumewahi kutokea ajali nyingi tu na Tume mbalimbali zimeundwa na Serikali hii ya CCM, lakini matokeo yake hayajatolewa kwa Umma wa watanzania na badala yake ripoti hizo zimefichwa kwenye "makabati" ya watawala wetu wa CCM.

Kwa kuzitaja chache ya Tume hizo:-

1. Iliundwa Tume ya kuchunguza namna pesa "zilivyochotwa" huko BoT, baada ya kifo cha aliyekuwa Rais wetu, Hayati Magufuli, lakini hadi leo, taarifa hiyo haikutolewa kwa Umma wa watanzania na badala yake zikafichwa na watawala wetu.

2. Iliundwa pia Tume ya kuchunguza moto uliounguza soko la Kariakoo, lakini baada ya Tume hiyo kukamilisha Kazi yake na kukabidhi ripoti hiyo kwa watawala wetu, hatukusomewa yalibainika nini kwenye Tume hiyo.

3. Iliundwa pia Tume ya kuchunguza Mauaji ya mfanyibiashara wa madini huko Mtwara, Mussa Hamisi, ambapo inadaiwa aliuawa na Polisi na wakampora pesa zake za madini, zaidi ya shilingi milioni 70, hata hivyo matokeo ya Tume hiyo pia, hatukujulishwa watanzania.

Najiuliza hivi ni kwanini watawala wetu wameingia "kiwewe" kwa ajali hii ya ndege ya Precision Air?

Lakini jibu ninalolipata ni kuwa tofauti na Tume zilizopita, ambazo watawala wetu ndiyo waliokuwa wanaunda Tume hizo na baada ya Tume hizo kukamilisha uchunguzi wao, watawala wetu wamekuwa wakituficha, Ili tusijue nini kimebainika na Tume hizo.

Tokea ajali hiyo ya ndege ya Precision Air, iliyotokea zaidi ya wiki moja iliyopita, kumekuwa na shutuma nyingi kutoka kwa Umma wa watanzania, kuwa kulitokea uzembe wa Hali ya juu kwa vikundi vya uokoaji kutotimiza wajibu wao, hadi kusababisha vifo hivyo 19.

Kutokana na safari hii Tume ya uchunguzi kuwa ni huru, ambayo inawahusisha wataalamu waliotengeneza ndege hiyo ya Precision Air, kutoka Ufaransa, ndiko nadhani kumewatia "kiwewe" watawala wetu na hasa baada ya Tume hiyo kusema hadharani kuwa matokeo ya Tume hiyo yatatolewa baada ya wiki 2 tokea ajali hiyo ilipotokea.
Ccm ni mafii
 
Back
Top Bottom