Ni kwanini Wagonjwa wengi sana hata wale walio Mahututi Siku Moja tu kabla ya Vifo vyao huwa wanakuwa Wachangamfu mno?

Nilishashuhudia kaka yangu alikuwepo ICU ila kuna siku aliongea na kusema mi nimepona tufanye utaratibu tuondoke,

Nakumbuka tulimwambia ukiendelea hivi tutatoka siku si nyingi.

Na tuliondoka pale tukiwa na matumaini ya kaka angu kupona lakini nilivyo rudi kesho yake saa 12 tayari alikuwa kaiaga dunia aisee,

Maana hospital ile ulikuwa habaki mtu pale ndani wa kumuuguzi wanauguza wao wenyewe,

nakumbuka nilimuona mama yangu akiwa na uchungu ambao sijawahi muona akiwa katika hali ile kabla...
 
Wataalamu waje hapa. Maana kuna ndugu yangu alikuwa mgonjwa hata kula akawa wa kulazimishwa. Kuna siku alidai ana hamu ya ugali na maziwa. Alipoletewa alikula hadi tukapata tumaini, ila niliona wazee wakiwa na wasiwasi sana. Kesho yake alfajiri alifariki.
 
Nilisha shuhudia kaka yangu alikuwepo ICU ila kuna siku aliongea na kusema mi nimepona tufanye utaratibu tuondoke,

Nakumbuka tulimwambia ukiendelea hivi tutatoka siku si nyingi...
Same story, different people. Umeniandikia. umepita mule mule.
 
Baba yangu alikuwa hata kula mwenyewe hawezi. Tulikuwa tumalisha kipindi chote cha ugonjwa. Siku hyo akajilisha mwenyewe tena chap chap. Nikasema baba umepata nafuu kubwa asante Mungu.

Nikaenda kuoga na baada ya nusi saa nimerudi mweeeh nimemkuta kageuza macho. Ndio ikawa mwanzo wa safari yake ya kukaa coma for 25 days. Pumzika kwa Amani Baba.
 
Kifo huwa tunakikataa. Ikitokea mgonjwa akakikubali kifo basi anapata nafuu, anakula na kufurahi maana anaaga afe.

Vijana wengi wanakufa kwa kuhangaika (struggles) wakipinga kufa. Wazee wengi na wagonjwa wa muda mrefu hukubali kifo na hivyo kufa kwa amani sana.
 
Mi mwenyewe nina baba yangu mdogo huyo alikuwa anaugua home kipindi hicho nimerudi shule likizo, amekaa wiki ndani hata nje hawezi kutoka siku hiyo bna jamaa kwanza kumekucha tu akadai leo hapigii mswaki ndani ivo anataka kuota jua na kupiga mswaki nje basi tukamtoa na stool tena fresh anadema dema,

imefika mchana kala fresh bila kumlazimisha jioni kameza dawa na akakaa sitting room kucheki video tukasema mgonjwa kapona aisee inafika saa tano usiku ni msala Mwamba ndo alikuwa anatembea ivo dah hio incidence ya kungata shuka kwa uncle mpaka leo imegoma kufutika kwa head mana nilishuhudia point tu point mpaka ile time mnafunika shuka completely
 
Mi mwenyewe nina baba yangu mdogo huyo alikuwa anaugua home kipindi hicho nimerudi shule likizo, amekaa wiki ndani hata nje hawezi kutoka siku hiyo bna jamaa kwanza kumekucha tu akadai leo hapigii mswaki ndani ivo anataka kuota jua na kupiga mswaki nje basi tukamtoa na stool tena fresh anadema dema...
Dah mpaka nimeogopa
 
hakika ulichoungumza ni kweli Mshana Jr aje atupe dondoo kidogo nimekumbuka mbali sana, na tangu siku hiyo sijaiona thamani ya maisha tena brother aliugua kwa siku tatu yuko hoi siku ya nne akaamka tukazungumza mambo mengi na ishu za kazini, akasema aombe ruhusa tutafte usafiri turudi home anajiskia nafuu, walahi usiku wake hali ilibadilika ghafla na ndio ikawa mwisho wa safari yake hapa duniani😭😭

R.I.P
 
Walio mahututi, huweza kupatana kwa amani na muumba wao. Mara nyingi hujaliwa pia kujua mwisho wa safari yao umekaribia kufika. Kwa sababu hizo, huwa wanakubali matokeo ya kuachana na dunia hii.

Ndio maana utakuta wanachangamka sana, bashasha na vicheko tele. Ndio maana mtoto anapozaliwa huwa peke yake analia, huku wengine wakichekelea bundle of joy... kulhal anapokufa, yeye huchekelea wakati wengine wakilia.

One foot in Heaven
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom