Ni kwanini Wafanyakazi wengi wa TRA siku hizi hasa wale wa vitengo muhimu vya ukusanyaji mapato wamekuwa waoga na hawajiamini mitaani?

Mzukulu

JF-Expert Member
Feb 14, 2020
1,401
2,629
Kwa baadhi niliokutana nao ( ambao nakiri hapa ) wazi wazi kuwa ni Marafiki zangu wazuri na wakubwa tu ila tokea Awamu hii ya Tano iingie Madarakani wengi Wao wamekuwa ni Waoga Waoga Kimuonekano na hata Hawajiamini tena huku hata mkiwa mmekaa nao tu mahala muda mwingi wanakuwa ni Watu wa Kuangaza angaza huku na kule halafu hawamuamini Mtu yoyote.

Je, ni Mimi tu Mzukulu pekee ndiyo nimeliona hili kwa hawa Wafanyakazi wa TRA au labda nanyi Wandugu mmeshakumbana nalo huko Makwenu?
 
Hii ni awamu nyingine, kila awamu ina mfumo wake, kila jambo na wakati wake
 
Zama zimebadirika Ndugu, Zama Hizi Hata ukitumia Mshahara wako halali Bado NusaNusa Watataka Kukuchunguza
 
Kwa baadhi niliokutana nao ( ambao nakiri hapa ) wazi wazi kuwa ni Marafiki zangu wazuri na wakubwa tu ila tokea Awamu hii ya Tano iingie Madarakani wengi Wao wamekuwa ni Waoga Waoga Kimuonekano na hata Hawajiamini tena huku hata mkiwa mmekaa nao tu mahala muda mwingi wanakuwa ni Watu wa Kuangaza angaza huku na kule halafu hawamuamini Mtu yoyote.

Je, ni Mimi tu Mzukulu pekee ndiyo nimeliona hili kwa hawa Wafanyakazi wa TRA au labda nanyi Wandugu mmeshakumbana nalo huko Makwenu?
Weka majina ya hao marafiki zako wa TRA ambao wanaishi kwa wasi wasi hapa ili na sisi tuwajue. Sababu zipo nyingi.

Kwa ufupi nchi hii hakuna hata mmoja ambaye anaishi kwa kujiamini. Ukitaka kuthibitisha hilo angalia ulinzi wa JPM hadi helcopta juu na mawasiliano ya simu kila mahali anapopita mbona hili huulizi?
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom