MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,244
- 7,966
Wanajukwaa si lengo langu kumsema mtu, ama siandiki kwa kusukumwa na hisia flani flani. Tumelalamikia kwa muda mrefu utendaji wa mahakana ya kimataifa ya makosa ya jinai ya uhalifu wa kivita(ICC) bila kutizama nyenendo zetu.Tulishuhudia juzjuzi tu nchini marekani afisa mkuu wa ujasusi wa nchi hiyo aliachia ngazi baada ya kuandamwa na tuhuma za kozorota kwa mambo ya kiusala nchini humo,kadhalika na nchi zingine za Ulaya na Asia uwajibikaji kwao ni kitu muhim sana. Uchu wa madaraka umetujaa nyoyoni mwetu,viburi, sifa na ubinafsi usiokua na maana.Ivi kweli kama unajijua we unalalamikiwa na jamii unatafuta ushahidi gani uletewe ili ujiuzulu? Kama huwezi kwanini unaona aibu kuachia ngazi? Hata kama hutambui hata vitabu vya M.Mungu ambavyo ambavyo vinaelezea maisha ya manabii na mitume walivyoishi ktk tawala zao, basi itoshe hata kuonyesha heshima kwa familia yako wewe.Nataka kusema kwamba watuhumuwa wote wa ESCROW acc wasisubir muda wa ushahidi wajiuzulu mapema.