The Phylosopher
JF-Expert Member
- Mar 11, 2015
- 1,494
- 2,040
Kuna swali nimejaribu kujiuliza kuhusiana na siasa zetu za Tanzania, mara nyingi vyama vimechukua hatua tofauti tofauti kwa wanachama wao.
Lengo kuu la hatua hizo ni kudumisha nidhamu ya chama na kuhakikisha kuwa chama kinabaki kwenye misingi yake.
Hata hivyo kwa kumbukumbu nyingi nilizonazo ni viongozi wachache sana kutokea upinzani ambao baada ya kuadhibiwa na chama walijirekebisha na kurejea kua wanachama watiifu badala yake wengi wao wameachana kabisa na siasa za upinzani.
Hali hiyo ni tofauti kabisa kwa wana-CCM ambao wakipewa adhabu aghalabu huitumikia na kurejea kuwa wanachama watiifu.
Hapa ndipo najiuliza kwani tatizo ni nini hasa?
Ni adhabu za maonezi zitolewazo na viongozi wa upinzani?
Ni kuhadaiwa na uongozi wa CCM?
Ni woga wa kuendesha maisha nje ya mfumo dola?
Ni kukosa uthabiti na umadhubuti wa kisiasa?
Au siasa ni ulaji tu hivyo tuache kuwashabikia wanasiasa kiuhalisia?
Naombeni mnisaidie kuwaza.
Lengo kuu la hatua hizo ni kudumisha nidhamu ya chama na kuhakikisha kuwa chama kinabaki kwenye misingi yake.
Hata hivyo kwa kumbukumbu nyingi nilizonazo ni viongozi wachache sana kutokea upinzani ambao baada ya kuadhibiwa na chama walijirekebisha na kurejea kua wanachama watiifu badala yake wengi wao wameachana kabisa na siasa za upinzani.
Hali hiyo ni tofauti kabisa kwa wana-CCM ambao wakipewa adhabu aghalabu huitumikia na kurejea kuwa wanachama watiifu.
Hapa ndipo najiuliza kwani tatizo ni nini hasa?
Ni adhabu za maonezi zitolewazo na viongozi wa upinzani?
Ni kuhadaiwa na uongozi wa CCM?
Ni woga wa kuendesha maisha nje ya mfumo dola?
Ni kukosa uthabiti na umadhubuti wa kisiasa?
Au siasa ni ulaji tu hivyo tuache kuwashabikia wanasiasa kiuhalisia?
Naombeni mnisaidie kuwaza.