Uchaguzi 2020 Ni kwanini TAKUKURU haijamchukulia hatua Dkt. Mayrose Majige wa CHADEMA kwa kutangaza kugombea Urais kabla ya muda?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,479
30,144
Tume ya uchaguzi ya Tanzania (NEC) ndiyo pekee yenye mamlaka ya kutangaza muda wa kuanza kampeni kwa vyama vyote vya sasa, kwa nafasi zote za zinazogombewa katika uchaguzi mkuu, unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.

Tume hiyo ya uchaguzi bado haijatowa ratiba hiyo na hivyo kuonya kwa yeyote atakayefanya kampeni kabla ya muda, wa kutoka chama chochote cha siasa, ajue kuwa anavunja sheria na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Kutokana na hali hiyo TAKUKURU imepewa jukumu la kuwachukulia hatua watu wote watakaofanya kampeni kabla ya muda kutangazwa.

Tumejionea namna TAKUKURU walivyokuwa wakali kwa jambo hilo, walipomtia mbaroni, Ismail Aden Rage, aliyekuwa mbunge wa Tabora mjini, kwa tiketi ya CCM, ambaye inasemekana amekuwa katika kampeni, kabla Tume ya uchaguzi ya Taifa, haijapuliza kipenga, cha kuanza rasmi kampeni.

Hata hivyo wananchi tumeshuhudia, namna mwanachama wa Chadema, Dkt Mayrose Majige, akiutangazia Umma wa watanzania kuwa ana nia ya kugombea Urais, kwa tiketi ya CHADEMA , katika uchaguzi wa mwaka huu.

Swali ninalouliza je ni kwanini TAKUKURU hawamtii mbaroni Dkt Mayrose Majige kwa kuanza kampeni mapema kabla ya muda?

Vile vile ninafahamu pia kuwa kwa mujibu wa Katiba ya nchi yetu, ni lazima mgombea yeyote adhaminiwe na apitishwe na chama chake, ndipo kimtangaze kuwa ni mgombea.

Je chama cha Chadema, ni lini kimemtangaza Dkt. Mayrose Majige kuwa kimempitisha kuwa mgombea wao kwa nafasi hiyo ya Urais?

Ni kwanini TAKUKURU itumike kisiasa katika kutimiza majukumu yake kwa kutumia "double standards" kwa kuelekezwa na mabosi wao watawala wa awamu ya tano wa CCM, ni nani wanapaswa kumkamata na kumhoji na nani hapaswi kukamatwa na kuhojiwa?

Ni dhahiri kuwa hao jamaa wa TAKUKURU wamepewa "maelekezo maalum" na mabosi wao watawala wa CCM kuwa wasithubutu kumkamata mwanamama huyo Dkt Mayrose Majige, kwa kuwa amepewa maelekezo maalum na CCM, atangaze nia ya kugombea nafasi hiyo ya Urais, kwa nia ya kuivuruga CHADEMA !

Kwa kuwa haiingii akilini ni kwa vipi wao TAKUKURU wafanye "double standard" kwa kosa la aina moja la kuvunja sheria ya uchaguzi, iliyotungwa na serikali yao katika kushughulikia wale wanaoanza kampeni mapema, kwa kumng'ang'ania mgombea wa CCM, Ismail Aden Rage na kumwacha huyu mwanamama, aliyetangaza hadharani kuwa anagombea Urais kwa tiketi ya Chadema

Tunachojua sisi wananchi ni kuwa huyo mwanamama Dkt Mayrose Majige, ni "mtu wao" hao CCM na ametangaza nia ya kugombea Urais, kwa maelekezo yao na ndiyo sababu TAKUKURU inashikwa na "kigugumizi"_cha kumtia mbaroni na kumhoji ni kwanini ameanza kampeni kabla ya muda
 
Mbona wao CCM wamekuwa "very strict" kwa kukataa wagombea wao wasitangaze nia mapema na kuanza kampeni kabla ya muda, iweje kwa huyu mwanamama kwa kutangaza nia ya kugombea Urais kwa tiketi ya Chadema, uamuzi wake huo ushangiliwe kwa nguvu na wanachama wengi wa CCM??
 
Sheria ipi
Huyu mama ishu ni kuwekewa pingamizi kwa tume ya uchaguzi ila nilimuona kama hayuko serious anatafuta teuzi mbeleni
Sheria inaangalia userious ukikosea? Angefanya hivyo mbowe ungesemahivi?
 
Manyumbu hawawez kuchangia umu Uzi umekaa kimtego jibu lolote watalo jibu kitakua nzuri kwa serekal
Huyu mama ishu ni kuwekewa pingamizi kwa tume ya uchaguzi ila nilimuona kama hayuko serious anatafuta teuzi mbeleni
 
Huyu mama ishu ni kuwekewa pingamizi kwa tume ya uchaguzi ila nilimuona kama hayuko serious anatafuta teuzi mbeleni
USSR
Sema huyo mama anafata nyayo za mama Anna Mgwira, ili na yeye akumbukwe kwenye nafasi za uteuzi za u-DC au u-RC!

Hebu tu-imagine hicho kitendo ndiyo amekuwa amekitenda Freeman Mbowe, tungeona kila mwanaccm hivi sasa angekuwa amemshukia kama mwewe na kutoa tamko la kutaka Chadema ifutwe kwenye daftari la vyama vya siasa hapa nchini, kwa kosa la kuvunja sheria ya vyama vya siasa
 
Sheria ipi
Sheria inaangalia userious ukikosea? Angefanya hivyo mbowe ungesemahivi?
Hilo sio jinai ni kukiuka kanuni za uchaguzi na hapo anaweza kuwekewa pingamizi th kama atagombea umenielewa kilaza wewe
 
Fikiria Membe ni sababu zipi zilizofanya avuliwe uanachama wa CCM?

Ni kutokana na "hisia" zao tu kuwa wanamhisi kuwa ana mpango wa kugombea Urais akimpinga Rais Magufuli!

Sasa kama Membe ametimuliwa CCM, ni kwanini huyu mama, anashangiliwa sana na wanaccm kuliko wanachadema, kwa kutangaza nia yake ya mapema kabla ya muda rasmi uliowekwa na Tume ya uchaguzi, kama siyo pandikizi lao??
 
Mbona wao CCM wamekuwa "very strict" kwa kukataa wagombea wao wasitangaze nia mapema na kuanza kampeni kabla ya muda, iweje kwa huyu mwanamama kwa kutangaza nia ya kugombea Urais kwa tiketi ya Chadema, uamuzi wake huo ushangiliwe kwa nguvu na wanachama wengi wa CCM??
Unajitekenya na kucheka mwenyewe, wapi kumeandikwa kutangaza nia ya kugombea ni kupiga kampeni? mwana CCM yupi kazuiwa kutangaza nia ya kugombea? mbona mie nimetangaza kugombea Sumve na sijashughulikiwa? hayo ni mambo yenu ndani ya chama hayatuhusu lakini pia kumbuka ni haki yake ya kikatiba.
 
Steve nyerere alitangaza nia ya kugombea ubunge Iringa Mjini, shishi nae katangaza nia ya kugombea ubunge moja kati ya majimbo ya Nchi hii je wamefuatwa na Takukuru?
Pambaneni na hali zenu..
Mbona wao CCM wamekuwa "very strict" kwa kukataa wagombea wao wasitangaze nia mapema na kuanza kampeni kabla ya muda, iweje kwa huyu mwanamama kwa kutangaza nia ya kugombea Urais kwa tiketi ya Chadema, uamuzi wake huo ushangiliwe kwa nguvu na wanachama wengi wa CCM??
 
Steve nyerere alitangaza nia ya kugombea ubunge Iringa Mjini, shishi nae katangaza nia ya kugombea ubunge moja kati ya majimbo ya Nchi hii je wamefuatwa na Takukuru?
Pambaneni na hali zenu..
getrusa
Mbona TAKUKURU wamemkamata Ismail Aden Rage wa chama chenu cha CCM, kwa kuanza kampeni kabla ya wakati??

Mbona nyinyi CCM milimfukuza Membe uanachama wa chama chenu cha CCM,kwa madai kuwa ameanza kampeni mapema ya kugombea Urais, dhidi ya Rais Magufuli??

Iweje sasa mseme ni ruksa kwa mtu yeyote, wa chama chochote cha siasa, kutangaza nia ya kugombea nafasi yoyote kabla ya muda??

Ni wazi kuwa hao TAKUKURU wanafanya kazi kwa "maelekezo maalum" ya watawala wa CCM, nani wa kumkamata na kumuhoji na nani wa kumuacha!
 
Hata hivyo wananchi tumeshuhudia, namna mwanachama wa Chadema, Dkt Mayrose Majige, akiutangazia Umma wa watanzania kuwa ana nia ya kugombea Urais, kwa tiketi ya Chadema, katika uchaguzi wa mwaka huu.

Swali ninalouliza je ni kwanini TAKUKURU hawamtii mbaroni Dkt Mayrose Majige kwa kuanza kampeni mapema kabla ya muda?
Mkuu Mystery, Dr. Mayrose Majinge hajatangaza kugombea, hajjateuliwa na hajaanza kampeni yoyote, bali ametangaza tuu nia ya kugombea urais wa JMT kwa tiketi ya Chadema. Hakuna ubaya wowote mtu yoyote kutangaza nia ya kugombea.

Usichangaye kuanza kampeni mapema, kujipitisha pitisha majimboni na kutangaza nia, hakuna kosa lolote kikatiba, kisheria, kikanuni na kiutaratibu, kwa mtu kutangaza nia.
P
 
Mkuu Mystery, Dr. Mayrose Majinge hajatangaza kugombea, ametangaza nia ya kugombea, Hakuna ubaya wowote mtu yoyote kutangaza nia ya kugombea.

Usichangaye kuanza kampeni mapema, kujipitisha pitisha majimboni na kutangaza nia, hakuna kosa lolote kikatiba, kisheria, kikanuni na kiutaratibu, kwa mtu kutangaza nia.
P
Pascal Mayalla
Ngoja nikuulize swali moja jepesi, mathlani Mimi nitangaze nia ya kugombea Urais, bila kuanza kampeni, wala chama "changu" cha CCM, kupitisha jina langu, dhidi ya Rais Magufuli mwaka huu, ningeendelea kuachwa nikiwa "free" mitaani bila kuchukuliwa hatua yoyote?
 
Pascal Mayalla
Ngoja nikuulize swali moja jepesi, mathlani Mimi nitangaze nia ya kugombea Urais, bila kuanza kampeni, wala chama "changu" cha CCM, kupitisha jina langu, dhidi ya Rais Magufuli mwaka huu, nitaachwa kweli bila kuchukuliwa hatua yoyote?
Naendelea kusisitiza, hakuna ubaya wowote wala kosa lolote kisheria, kikatiba, kikanuni wala kiutaratibu kutangaza nia ya kugombea nafasi yoyote. Kutangaza nia ni kuonyesha intent.

Mimi namuunga mkono Dr. Mayrose Majinge kwa asilimia 100!.

Live from EA Radio Super Breakfast: Mtangaza Nia Urais wa JMT Kupitia Chadema, Dr. Mayrose Majinge Yuko Live, Mubashara - JamiiForums

Mwanamke ajitokeza kuwania Urais kupitia CHADEMA. Ni Msomi, Mwanamke wa Shoka, Ana uwezo na Jembe Kweli, ila... - JamiiForums

Na nilianza kumfahamu kitambo toka akiwa CCM. Soma CV yake hapa

Uenyekiti wa UWT: Ni Vita Kati ya Ukweli na Ubatili! - JamiiForums
P
 
Tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu, tutayashudia mambo mengi sana ya vituko!
 
Back
Top Bottom