Ni kwanini Magufuli hawezi kuua upinzani (CHADEMA na CUF) hizi hapa sababu

Chadema haiuliwi na Magufuli inauliwa Kwa kukosa kwake Msimamo kwenye Yale inayoamua yenyewe Kwa hiyari Yao!

Ukitaka kujifunza umuhimu wa Ideology ya Chama Na umuhimu wake watazame ANC kabla ya Uhuru
Watazame Islamic brotherhood kule Egypt

Watazame Hamas kule Palestine

Laki hapa Leo unasema hiki Wafuasi wako wanaamini Na kuanza kulimeza kesho unawatapisha na kuwalisha jambo jipya

Mifano michache

1) 2005-2010 Chadema walikuja Na sera ya Majimbo wakimaanisha tuwe Na Federation Goverment lakin tangu 2010 baada ya kutikiswa kidogo tu mtikisiko wa Kisiasa wanaogopa Tena kuhubiri Hii sera

2) Chadema hawa hawa walikuja Na list of shame Na Mmoja Wao akawa Lowassa lakin Wao ghafla wakaja Sio tu kumfutia tuhuma bali kumteua kuwa Mgombea Dola

3) Chadema hawa hawa walitangaza hawatashiriki chaguzi zozote mpaka ipatikane tume huru Na Katiba Mpya lakin Wao tena wakapiga u turn wakarejea kwenye chaguzi ndogo
4) Chadema hawa hawa kupitia Mbowe baada ya kusalitiwa Na Shibuda walitangaza hawatachuku Tena Mtu kutoka CCM Na kumfanya Mgombea lakin Wao Wenyewe ikawa Mtu akitoka CCM ndio anapewa kipaumbele Cha kugombea rejea ya Lowassa , Lawrence Masha, Ole Medeye, Makongoro n.k

Chama hasa Cha Upinzani kikitaka kuwa Chama Kwa maana ya itikadi lazima kiachane Na mambo ya Kubadili gia angani, Siasa Sio Biashara ambayo unaweza kwenda Dubai ukisema unaenda kuchukua mzigo wa Nguo lakin ukapigiwa Simu Na Mdau wako akakwambia kuna uhaba wa viatu Achana Na Nguo beba viatu urudi fasta tuwahi sikukuu ya Eid
Tupe sababu kwanini jiwe hataki mikutano ya siasa na wakati kikatiba inaruhusiwa
 
Kuna Baadhi ya vijana wa Lumumba ambao wanazunguka na kupiga vigelegele kuwa Mwenyekiti wao Dt John Magufuri anaiua chadema ( upinzani), mpaka imepelekea baadhi ya Madiwani na wabunge kuhofia Kama wanaweza wasirudi mwaka 2020, Hii imewafanya wasaka vyeo wengi kuweweseka na kuamua kujisalimisha ccm kwakuhofia nafasi zao au mstakabali wao wa kisiasa kabla chadema ifikapo mwaka 2020 kama avyosema Dr Magufuri alipokuwa singida mpaka ifikapo Mwaka 2020 atahakikisha ameuzika upinzani Upinzani (Chadema).

Hata baadhi ya wanachama na viongozi wenye mapenzi wema na chama chao chadema wanabaki na kujiuliza huyu Magufuri atatoka mwaka 2020 kweli wabunge na Madiwani wataongezeka kweli haya ndio maswali ambayo wanachadema wengi wamekuwa wanajiuza lakini wamekosa Majibu yake, Lakini leo nimeamua kuja na majibu ya baadhi ya maswali hayo.

Chadema (Upinzani) hauwezi kufa kwa sababu ya baadhi ya Viongozi wake na madiwani kuondoka chamani, badala yake hivi sasa chama hicho kiko kwenye hatua ya mwisho ya kujirasimisha ili kichukue na kiiongoze Serikali, hii inaonekana kwenye Urasimishaji wa Chama ( Party Institutionalization) ambapo kuna mambo matatu unatakiwa kuyazingatia ambayo ni Utatanisho (complexity), ulinganisho (Adaptation) na Uhuru pasipo kuingiliwa (autonomous).

Chama chochote ili kichukue Serikali kinatakiwa kuyapitia Mambo hayo Matatu kwa kupande wa Chadema kimeshapitia mambo makuu mawili Ulinganisho na Utatanisho sasa kipo kwenye hatua kinapigania uhuru pasipo kuingiliwa (Autonomous), Ambapo wanachama wengi na viongozi hukutana na changamoto mbali mbali kufungwa au kuuwawa kabisa, kwa ufupi ngoja nielezee hatua hizi kwa kirefu na kuzioanisha na Chadema Kama imeshazipitia na kubaki imara.

Nianze na Ulinganisho (Adaptation) hii ni hatua ambapo chama ubadilika ulingana na mazingira pamoja na Mahitaji, Kwa upande wa chadema kimekuwa kikibadilika ili kiendane na Mazingira yalioyopo mfano Mzuri mabadiliko ya Katiba Mwaka 2006 pamoja na Uboreshaji wa Katiba Mwaka 2016 ili kuitambua chaso (Chadema student Organization) na kuzipa mamlaka kanda, Mabadiliko hayo yameifanya chadema kuwa imara sana kwa mfano kuzipa mamlaka kanda imesaidia kupunguza mrundikano wa shughuli kwenye ofisi ya Katibu mkuu na kuifanya chadema kuwa taasisi yenye sifa zote za Urasimu (Bureaucracy) Kama alivyosema Max Werber kwenye Nadharia yake Rationalism.

Hatua nyinyine ni Utatanisho (Complexity) neno hili inatokana na neno utata au ugumu, chama kinapopitia kwenye ugumu na kubaki imara hakiwezi kufa kamwe, Hapa ndio kauli ya Dhahabu ili ing'are inatakiwa kupita kwenye moto mkali, chadema na CUF ni vyama pekee nchini vilivyopitia Magumu mengi na kuendelea kubaki imara kabisa mfano wa Magumu Chadema kiliyoupitia ni kuondoka Kwa aliokuwa naibu katibu mkuu wake Mbunge Machachari Bw Zitto Kabwe na Katibu mkuu wake Alikuwa Mgombea Urais Mwaka 2010 Dr Wilboard Slaa lakini chama bado hakikuteteleka kilibaki imara Kabisa.

Hatua nyingine ni Uhuru Pasipo kuingiliwa (autonomous) Hii ni hatua ngumu Sana kwa chama ni kipindi ambapo chama kilichopo Madarakani kinatumia njia yoyote ili kiendelee kubaki madarakani mpaka inafikia hatua ya chama tawala kukingilia kwenye baadhi Programme zake zisifanikiwe, Na mfano mzuri hapa tunauona chadema kuzuiwa kufanya Mikutano ya Hadhara na maandamano ambayo yapo kwa mujibu wa katiba huku chama tawala chenyewe kinafanya.

Viongozi wao kuwa na kesi mbali mbali wanachama wao kutishwa vyombo vya Dola wapinzani kuuwawa, hizi ni dalili za upinzani kuwa na nguvu kubwa mpaka kinaogopesha kuwepo na chama dola kwa hiyo chama kinachotaka kudondoka hutumia Nguvu kubwa kuendelea kupaki madarakani. upinzani usipokuwa makini utacheleshwa tu kuingia Madarakani lakini hutokufa, hapa ndio kauli ya Punda akitaka kufa huwa anamateke makali huthibitika hapa usipokuwa Mvumilivu kwenye hatua hii unaweza kujisalimisha kwao au kuacha siasa.

Ushauri wangu kwa chadema kwa sasa hivi kinatakiwa kijikite zaidi Urasimishaji wa Chama Ndani (internal Party Institutionalization) na Urasimishaji wa chama wa nje (External Party Institutionalization), ambapo kwenye Urasimishaji wa ndani wa chama (Internal Party institutionalization ndani yake kuna Mwanzo wa uundwaji (Origin), kiwe na Raslimali za kutosha (Resources) chama kuwa wamoja (Organization Cohesion.)

Kwa vile zingine zinaelewaka ngoja nizungumzie Mwanzo wa uundwaji (Origin), chama ambacho kimesambaa na kijipenyeza vizuri chini katika kipindi cha uundwaji, kinauhakika wa kushinda kuliko chama ambacho hakina matawi ya kutosha huko chini kwa hiyo basi ushauri wangu kwa chadema (Upinzani) kinatakiwa kihakikishe Programu ya chadema ni msingi imefanikiwa kwa Asilimia mia, kinapoingia kwenye uchaguzi wa serikali za Mitaa kihakikishe kinaweka wagombea sehemu zote na wagombea wote

Vile vile Chadema kinatakiwa kiongeze Urasimishaji wa nje ya chama hapa na maanisha kiwe na uhusiano mzuri na Taasisi zingine mfano vyama vya Walimu, Vyama vya Madktari Mashirika ambayo sio ya kiserikali na Makanisa pamoja na Pia kiwe na Uhusiano mzuri na vyama vingine vya siasa Kama vile CUF, ACT, NCCR Mageuzi na Vingine vingi ili kipate sapoti yao vyama ambavyo bado ni vichanga na vinawanasiasa wenye uwepo na ni wapinzani kweli washawishiwe wavivunje vyama vyao waingie CUF au Chadema Mfano ACT na NCCR Mageuzi na Vingine ili kujitengenezea wigo mpana wa kukishambulia chama Dola.

Hitimisho langu Migogoro ndani ya chama mfano Mgogoro wa Agustine Mrema na Mabele Marando NCCR Mageuzi na kukosa mvuto mbele ya Watu mfano UDP ya Cheyo ndio vitu pekee vinavyoweza kuua chama cha siasa na sio vyombo vya Dola, kwa maana hiyo ccm inapoteza mda na nguvu zao bure: Kwani chadema imepitia migogoro mikubwa lakini bado iko imara. Mwaka 2020 chadema inachukua Serikali dalili zinaonekana wanachadema na wapinzani wajiandae mpaka hapa Sifa zote njema zinamstahiki Allah, Mola wa walimwengu wote Asanteni Sana.


Ni Mimi Mhere Mwita,
Mwana wa Geita,
0742530600.
Hata makaburu walipomfunga Mandela na kuua wapinzani wao walidhani hakuna siku itatokea mweusi akachukua dola South Africa.
Siku zote mtu asiye na haki,hutumia nguvu kubwa sana kupora haki,ni sawa na jambazi tu.
 
Chadema haiuliwi na Magufuli inauliwa Kwa kukosa kwake Msimamo kwenye Yale inayoamua yenyewe Kwa hiyari Yao!

Ukitaka kujifunza umuhimu wa Ideology ya Chama Na umuhimu wake watazame ANC kabla ya Uhuru
Watazame Islamic brotherhood kule Egypt

Watazame Hamas kule Palestine

Laki hapa Leo unasema hiki Wafuasi wako wanaamini Na kuanza kulimeza kesho unawatapisha na kuwalisha jambo jipya

Mifano michache

1) 2005-2010 Chadema walikuja Na sera ya Majimbo wakimaanisha tuwe Na Federation Goverment lakin tangu 2010 baada ya kutikiswa kidogo tu mtikisiko wa Kisiasa wanaogopa Tena kuhubiri Hii sera

2) Chadema hawa hawa walikuja Na list of shame Na Mmoja Wao akawa Lowassa lakin Wao ghafla wakaja Sio tu kumfutia tuhuma bali kumteua kuwa Mgombea Dola

3) Chadema hawa hawa walitangaza hawatashiriki chaguzi zozote mpaka ipatikane tume huru Na Katiba Mpya lakin Wao tena wakapiga u turn wakarejea kwenye chaguzi ndogo
4) Chadema hawa hawa kupitia Mbowe baada ya kusalitiwa Na Shibuda walitangaza hawatachuku Tena Mtu kutoka CCM Na kumfanya Mgombea lakin Wao Wenyewe ikawa Mtu akitoka CCM ndio anapewa kipaumbele Cha kugombea rejea ya Lowassa , Lawrence Masha, Ole Medeye, Makongoro n.k

Chama hasa Cha Upinzani kikitaka kuwa Chama Kwa maana ya itikadi lazima kiachane Na mambo ya Kubadili gia angani, Siasa Sio Biashara ambayo unaweza kwenda Dubai ukisema unaenda kuchukua mzigo wa Nguo lakin ukapigiwa Simu Na Mdau wako akakwambia kuna uhaba wa viatu Achana Na Nguo beba viatu urudi fasta tuwahi sikukuu ya Eid
Huna unachojua wewe,magufuli na ccm.ndo miungu yenu,hata siku magufuli akija kwako akakuambia anamtaka mkeo akalale naye,utapiga makofi kufurahia na kisha unampa mkeo anaenda kujilia.
Maana kazi yenu ni kusifia kila uchafu anaofanya.
 
Tupe sababu kwanini jiwe hataki mikutano ya siasa na wakati kikatiba inaruhusiwa
Kwasababu Nyie Ni Dhaifu mkipigwa Marufuku kufanya Siasa mnatii hata kwenda Mahakamani ku challenge uhalali wa katazo Hilo mmeshindwa
 
Kwa Lugha rahisi Ulipaswa useme 'kwa hoja hii nakubaliana nawe Ila Kwa hoja zingine sikubaliani nawe'

kwani Wewe una 'pinal code Au Msahafu' wa kuamua Kwa hoja hii this is the point Na hii Sio point!

Mtazamo wako ubaki ni Msimamo wako Sio ndio prevailing facts utake wote wawe Na Mtazamo Kama wako

Chama chenye kila resource kinashindwa washawishi wananchi na kubaki kuwanunua wapinzani jua hicho ni chama mahututi (ccm)
 
Huna unachojua wewe,magufuli na ccm.ndo miungu yenu,hata siku magufuli akija kwako akakuambia anamtaka mkeo akalale naye,utapiga makofi kufurahia na kisha unampa mkeo anaenda kujilia.
Maana kazi yenu ni kusifia kila uchafu anaofanya.

Hata kusoma comment yako Sijui lakin umenijibu ili nisome
 
Back
Top Bottom