Ni kwanini kiswahili cha Mtwara kiko tofauti na kiswahili cha kawaida?

Kiswahili cha sehemu yoyote ile kipo tofauti na kiswahili cha kawaida.
ila cha hawa jamaa kimezidi kuwa tofauti jamani, utafikiri sio watanzania, hata unapo fanya mazungumzo nao kama hujajua uzungumzaji wao huwezi elewa kama ji kiswahili wanaongea
 
bwanuweweee, mi bado sielewi kwanini wapo hivi , yaani kama ndio unakutana na mtu wa mtwara kwa mara ya kwanza na hujajua namna ya uzungumzaji wao basi unaweza sema aio mtz kabisa,

ndio watanzania wa kila mkoa wameadhirika na namna yakuongea kiswahili , ila cha hawa sidhani kama nikiswahili ,
 
bwanuweweee, mi bado sielewi kwanini wapo hivi , yaani kama ndio unakutana na mtu wa mtwara kwa mara ya kwanza na hujajua namna ya uzungumzaji wao basi unaweza sema aio mtz kabisa,

ndio watanzania wa kila mkoa wameadhirika na namna yakuongea kiswahili , ila cha hawa sidhani kama nikiswahili ,
Kiswahili chao badoo nafanya tathmini
 
Mbona jibu ni rahisi tu ! That is because of location,origin,distance= dialect
 
hiyo ni kawaida mkuu. katika kila lugha kuna lahaja (dialects) pamoja na standard language(ambayo ndiyo wewe umeibatiza jina la lugha ya kawaida). Dialects ni utumizi wa lugha ambao unaonesha utofauti na utumizi wa lugha ya kawaida au standard language. sasa dialects zaweza kusababishwa na mambo tofauti likiwemo umbali wa kijografia, matabaka ya kiuchumi, pamoja na shughuli zetu za kila siku.

lakini pia lugha nyingi ambazo tunazitambua kama lugha za taifa au lugha rasmi mara nyingi si lugha za kwanza(mother tongue) kwa wengi wetu. hii inamaanisha kuwa wengi wetu tunaanza kujifunza kiswahili baada ya kuwa tayari tunaongea lugha za makabila yetu kama vile kisukuma, kinyamwezi au hata hicho kimakonde. Kinachokuja kutokea wakati tunajifunza lugha nyingine (kiswahili katika mada yetu) tunajikuta tunaingiza accents za lugha mama katika lugha zetu za pili, za tatu na kuendelea.

kwasababu hiyo basi, utofauti huo wa utumizi wa kiswahili haujioneshi kwa wamakonde peke yao. tunaweza uona kwa wachaga, wasukuma, wasambaa, wenzetu wazanzibar, watu kutoka Tanga n.k.

Hili halijitokezi kwenye kiswahili tu bali hata kwenye lugha zingine kama kiingereza. Kwa mfano, sisi wabantu hatuna silabi ambazo kiingereza zinaitwa clossed syllable, maneno ambayo hayaishii na ilabu bali yanaishia na konsonanti. Matokeo yake katika ujifunzaji wa kiingereza, wapo wanaoshindwa kuendana na baadhi ya clossed syllables kwenye kiingereza hivyo kujikuta maneno kama "GOING" huyatamka "GOINGI"
 
Lafudhi zinatofautiana kila mahala. Mifano:
WaTanga huwashangaa sana waDar au waMikoani wanapoongeza GA kwenye matamshi ya maneno.

Mfano:
Nakupenda-GA
Alimletea-GA

Au, waVisiwani na Tanga husema HICHI badala ya HIKI.

Mfano:
Kiti HICHI badala ya
Kiti HIKI.
 
Fanya uchunguzi, kila mkoa wana lafuzi yao kwa sisi ambao tumesafiri mikoa mbali mbali utasikia tu, mfano tunaotoka Arusha tukienda Dar imekuwa ni rahisi sana kutambulika wao wa dar wakija tunajua kabisa ni wa pwani hawa, ukitokea Moshi ah basi wanajua Mangi, kadhalika, akitokea Maswa au ukanda wa Mwanza unajua huyu msukuma ndivyo ilivyo kwa hiyo hakuna haja ya kuuliza kwanini ila akikaa miaka anaanza kupoteza ile lafuzi.
 
Heshima zenu wadau zangu,

Kwa sasa nipo mkoani Mtwara ila kinachonishangaza katika huu mkoa.

Ni aina ya lugha ya kiswahili kiko tofauti ninachokijuaa yaani wakati sisi tunapaita Mtwara wao wanaita Ntwara, mtu wao wanasema 'ntuu'.

Sikubali wao ni 'chikubali' au sielewi wao wanasema 'chielewi' hayo ni baadhi ya maneno ninavyowasikia wenyeji wangu wakiongea ila kubwa ni kwanimi kiswahili chao kipo tofauti na kile cha kawaida?.
Kwenye kila lugha kuna dialects. Ukienda Pemba kiswahili chao tofauti na cha bara, ukienda usukumani utasikia tunakwendhaga. Kwendhaga siyo standard swahili hivyo ujue hata wewe yawezekana kiswahili chako siyo kile cha darasani.
 
Ishu ya kuongea kiswahili tofauti si Mtwara tu, kule pia kwa kina mwanafyale, viatu si wanaita Fiatu, vitu wanaita fitu.
Ukienda kule kwa akina ummanyire Juma Nkambi nao ni shida,.
Rudi hapo kwa ndugu zangu WasuK, ukiweka vocha ya buku inaisha sekunde tu sababu ya matamshi mazito utadhani mwongeaji kabeba gunia,.
Mara huko ndio usiombe, wao hawana L ni R kwenda mbele.
Na kwingine kwingi tu. Sijui ni kabila gani ambalo limenyooka kiswahili.
Mpogoro amekuja na kambale wake Dsm kuuza, mkononi ana kisu,. Katangaza wee asubuhi hadi jioni hajapata mteja hata mmoja,. Kisa ni lafudhi. Baada ya kutangaza kambale kambale, yeye anasema kaambali, kaambali. Sasa watu wakiangalia anasema kaa mbali halafu mkononi ana kisu, nani aende. Watu wakawa wanapita mbali.
 
Baaah,bwana ww jee kwaniii??kutuonaje watu wa ntwaraa,?wenyewe tumizoeaa na tunaona kunoga iiyooooo moja iyoo haina jinaa...kwahiyo ufanye kupita tuu utuachee au ukitaka chamaki nchanga!??we chema tuu wapo ushindwe wewe tuu...bah!!!
 
Fanya uchunguzi, kila mkoa wana lafuzi yao kwa sisi ambao tumesafiri mikoa mbali mbali utasikia tu, mfano tunaotoka Arusha tukienda Dar imekuwa ni rahisi sana kutambulika wao wa dar wakija tunajua kabisa ni wa pwani hawa, ukitokea Moshi ah basi wanajua Mangi, kadhalika, akitokea Maswa au ukanda wa Mwanza unajua huyu msukuma ndivyo ilivyo kwa hiyo hakuna haja ya kuuliza kwanini ila akikaa miaka anaanza kupoteza ile lafuzi.
Jamaa inabidi alielewe hili,..pengine ndio Mara yake ya kwanza kutoka nje na mahali anapoishi ndio maana anaona tofauti,ila kila kona ya nchi hii ina lafudhi yake.
 
Tatizo lipo kwako mtoa Uzi, Hukutembea mikoa mbalimbali, Mwanza nao wana kiswahili chao, Arusha,Dar, Sumbawanga,Mbeya,Musssoma,Tanga, nk.,, Kiujumla tembea Uyaone Na ujifunze mengi, Singida pia Hali kadhalika. Hii imetokana na matabaka ya Makabila yalioko Nchini, Pia kumbuka tatizo Kubwa zaidi lililo Pelekea watu kuwa na viswahili visivyo fanana, kumechangiwa sana na Kutopatiwa Elim mapema, watz walidumu ktk Lugha zao za Asili, Hili tatizo pia serekali ya ccm inapaswa kulaumia sana Kw kuwanyima watz Elim tangu mapema, Hivyo taifa limekuwa na watu wasiejuwa kiswahili ,,

Labda Kiingereza ndio kingesawazisha, ingawaje nchi nyingine kama Nigeria kuna dalili ya kushindwa kusawazisha.
 
Kiukweli hakuna kitu kama hicho.. Kitu pekee ambacho Mtwara wanachanganya ni matumizi ya m na n basi.. lakisi kuseme CHIKUELEWI huo ni uzushi tena wa kipumbavu kabisa na kuwakebehi watu wa huko.. Tatizo lao liko sawa kabisa na wakurya Mkoa wa mara.. hawawezi kutofautisha kati ya R na L..
 
Back
Top Bottom