GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,089
- 107,609
Hivi ni kwanini kila kukicha tu Watanzania tunalalamika kuwa maisha ni magumu na wengi wetu kuitupia lawama Serikali / Watawala kuwa ndiyo sababu Kuu ya Umasikini tulionao wengi wetu lakini hapo hapo ama tunajisahaulisha kwa makusudi au hatupendi kusema ukweli kuwa moja ya sababu Kubwa ya wengi wetu kuwa masikini na hali hii ngumu ya maisha ni kupenda Kuzaa hovyo kama Sungura pasipo mpango?
Hivi kwa mfano unakuta Mtu anafanya Kazi ya Mshahara wa Tsh 240,000/ kwa mwezi halafu hapo hapo anakimbilia Kuoa na kuanza Kufyatua Watoto bila mpangilio na kufikia kuwa na Watoto 3 au 4 hali ambayo inapelekea kuanza kushindwa kuwahudumia na maisha yake kuzidi kuwa magumu. Je hapa Serikali / Watawala wanastahili lawama juu ya Umasikini wako uliojitakia?
Leo nitaomba mnipe majibu yenu Kuntu / Mujarab kabisa ni kwanini Watanzania wengi ukweli huu kwamba moja ya sababu Kubwa kabisa ya Umasikini / Maisha magumu tuliyonayo ni kwasababu ya kupenda Kuzaa zaa hovyo kama Sungura bila mpangilio na wengi wetu tukija na sababu za Kipuuzi / Kiupupu kabisa kuwa kila Mtoto anakuja na baraka zake?
Nawasilisha.
Hivi kwa mfano unakuta Mtu anafanya Kazi ya Mshahara wa Tsh 240,000/ kwa mwezi halafu hapo hapo anakimbilia Kuoa na kuanza Kufyatua Watoto bila mpangilio na kufikia kuwa na Watoto 3 au 4 hali ambayo inapelekea kuanza kushindwa kuwahudumia na maisha yake kuzidi kuwa magumu. Je hapa Serikali / Watawala wanastahili lawama juu ya Umasikini wako uliojitakia?
Leo nitaomba mnipe majibu yenu Kuntu / Mujarab kabisa ni kwanini Watanzania wengi ukweli huu kwamba moja ya sababu Kubwa kabisa ya Umasikini / Maisha magumu tuliyonayo ni kwasababu ya kupenda Kuzaa zaa hovyo kama Sungura bila mpangilio na wengi wetu tukija na sababu za Kipuuzi / Kiupupu kabisa kuwa kila Mtoto anakuja na baraka zake?
Nawasilisha.