Ni kwanini kila migogoro ikitokea Dangote Cement lazima Obasanjo atue nchini?

Lobbying ni mini maana yake boss,nitoe tongotongo
Lobbying kwa lugha rahisi ni kitendo cha mtu au kikundi cha watu kujaribu kushawishi serikali au mwanasiasa/wanasiasa kadhaa waweze kupitisha jambo/sera fulani kwa manufaa ya watu kadhaa.

Mfano: Dangote ana pesa na anataka kuwekeza Tanzania lakini hana ushawishi au hana uzowefu na sera na mifumo ya uwekezaji wa hapa Tanzania.

Lakini Dangote anafahamiana na Obasanjo ambae anaifahamu Tanzania na ana ushawishi kwakuwa alishakuwa rais wa Nigeria.

Hivyo Dangote anamtumia Obasanjo kufanya lobbying na serikali ya Tanzania ili kumtengenezea mazingira rahisi katika uwekezaji wake.

Nadhani utakuwa umepata mwanga mkuu.
 
Mzee Obasanjo hanaga shuguli maalumu..anazurura tu. Hata wewe ukiwa na harusi unaweza kumualika
Nafasi aliyoshika inamfanya kuwa PR mzuri kutengeneza mahusiano na kampuni na nchi mbalimbali, ndiyo maana makampuni kama Pepsi.Nike au Adidas wanawatumia Messi au Ronaldo
 
Wasalaam Wakuu,

Hivi ni kwanini kila kunapotokea changamoto/ mgogoro kwenye kiwanda cha Dangote Cement Mtwara basi ndani ya siku chache tu lazima Rais Mstaafu wa Nigeria Obasanjo atue nchini na kuzungumza na Mkuu wa Nchi?

Ilitokea hili mara mbili wakati wa Rais Hayati Magufuli, na hivi majuzi badala ya mgogoro wa kiwanda na madereva nasikia leo hii Obasanjo ameonana na kufanya mazungumzo na Rais Mama Samia.

Kuna nini nyuma ya pazia Kati ya Dangote Group na Obasanjo?
Unawezakuta ana share kwenye kampuni ,kwa Nigeria iko poa rais mstaafu kuwa mfanyabiashara.kama ilivyokua kwa Bush jr na barick
 
Kwa kumbukumbu zangu. Obasanjo ni mshirika mkuu na ambassador wa Dangote. Wakati Obasaji anagombea urais miaka hiyo. Dangote alitumia raslimali zake nyingi kumpigia kampeni. Kwa kufanya hivyo Dangite akapata tenda nyingi za serikali wakati wa Obasanjo akazidi kutajirika.
Obasanjo alipostaafu Dangote akamfanya ambassador wake kwa kuwa Obasanjo kwa heshima yake ni rahisi kuinana na viongozi.
 
Back
Top Bottom