Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,477
- 30,130
Kuna clip ambayo imeendelea kusambaa mtandaoni, ambayo bila shaka yoyote, sauti inayosikika humo ni ya Mbunge wa Ukonga na waziri mdogo wa TAMISEMI Mwita Waitara
Katika clip hiyo amesikika mbunge huyo akitamka kuwa kwenye vita ya uchumi, mnapoona kuna mtu anawakwamisha kwenye vita hiyo hamna budi KUMTANGULIZA mtu huyo!
Ni maneno ya hatari sana kwa usalama wa nchi yetu, kutamkwa na mwanasiasa, mwenye wadhifa mkubwa wa ubunge, ambapo anatoa hukumu kuwa mtu wa aina hiyo hana budi kuuawa!
Ni maneno ya hatari mno kutamkwa kwa kuwa tunavyojua ni chombo kimoja pekee kilichopewa dhamana ya kutoa hukumu hapa nchini, ambapo chombo hicho ni mahakama
Vile vile ni maneno ya hatari mno kwa kuwa hadi sasa ni zaidi ya mwaka mmoja na nusu, hakuna mtuhumiwa hata mmoja aliyekamatwa na kufanyiwa "interrogation" kuhusiana na tukio lile la kumiminiwa risasi zaidi ya 30 kwenye gari lake, kwa nia ya kumwua Tundu Lissu, ambapo hadi sasa anaendelea kuuguza majeraha katika hospitali nje ya nchi.
Ndipo hapo ninapojiuliza, je Jeshi la Polisi linasubiri nini kumkamata Mwita Waitara, kwa mahojiano ili limfikishe mahakamani kutokana na maneno yake ya UCHOCHEZI??
Kama Jeshi la Polisi halitamkamata Mwita Waitara, tutajua kuwa limepewa "maagizo" toka juu ili lisifanye hivyo!
Kwa kufanya hivyo ndipo Jeshi hilo linatengeneza visasi vya hali ya juu ndani ya Jamii ya watanzania, kwa kuwa itakuwa inafahamika wazi kuwa kuna baadhi ya watu ndani ya CCM, wanaweza kuongea vitu vya hatari sana kwa nchi hii, lakini vyombo vya ulinzi na usalama vya nchi haviwezi kuwakamata, kwa kuwa kundi hilo la watu ni UNTOUCHABLES!
Katika clip hiyo amesikika mbunge huyo akitamka kuwa kwenye vita ya uchumi, mnapoona kuna mtu anawakwamisha kwenye vita hiyo hamna budi KUMTANGULIZA mtu huyo!
Ni maneno ya hatari sana kwa usalama wa nchi yetu, kutamkwa na mwanasiasa, mwenye wadhifa mkubwa wa ubunge, ambapo anatoa hukumu kuwa mtu wa aina hiyo hana budi kuuawa!
Ni maneno ya hatari mno kutamkwa kwa kuwa tunavyojua ni chombo kimoja pekee kilichopewa dhamana ya kutoa hukumu hapa nchini, ambapo chombo hicho ni mahakama
Vile vile ni maneno ya hatari mno kwa kuwa hadi sasa ni zaidi ya mwaka mmoja na nusu, hakuna mtuhumiwa hata mmoja aliyekamatwa na kufanyiwa "interrogation" kuhusiana na tukio lile la kumiminiwa risasi zaidi ya 30 kwenye gari lake, kwa nia ya kumwua Tundu Lissu, ambapo hadi sasa anaendelea kuuguza majeraha katika hospitali nje ya nchi.
Ndipo hapo ninapojiuliza, je Jeshi la Polisi linasubiri nini kumkamata Mwita Waitara, kwa mahojiano ili limfikishe mahakamani kutokana na maneno yake ya UCHOCHEZI??
Kama Jeshi la Polisi halitamkamata Mwita Waitara, tutajua kuwa limepewa "maagizo" toka juu ili lisifanye hivyo!
Kwa kufanya hivyo ndipo Jeshi hilo linatengeneza visasi vya hali ya juu ndani ya Jamii ya watanzania, kwa kuwa itakuwa inafahamika wazi kuwa kuna baadhi ya watu ndani ya CCM, wanaweza kuongea vitu vya hatari sana kwa nchi hii, lakini vyombo vya ulinzi na usalama vya nchi haviwezi kuwakamata, kwa kuwa kundi hilo la watu ni UNTOUCHABLES!