Mngurimi
JF-Expert Member
- May 27, 2020
- 819
- 789
Kichwa cha habari tajwa hapo juu ni moja kati ya maswali pendwa sana ambayo wahitimu kutoka vyuo mbalimbali huulizwa. Miaka minne iliyopita baada ya kutoka chuo niliulizwa swali hili na baadhi ya ndugu wa karibu wasiowahi kufika chuo. Wengi walihoji kuhusu pesa niliyokuwa nikiipata na wakati huo wakinipa mfano wa watu waliofanikiwa kupitia pesa ya boom na kufanya vitu vikubwa.
Kwangu, swali kama hilo sikutaka kulijibu maana ningelijibu lingenifanya nionekane sina nidhamu. Ninashukuru kwa sasa maisha yanaenda japo sijawahi kutumia pesa ya boom kufanya vitu vikubwa tofauti na kufungua miradi midogomidogo na kuishia kudhulumiwa au kukosa waendeshaji walio wema. Mafanikio yangu leo yanatokana na juhudi zangu binafsi na wala sio zile pesa za chuo ambazo huzuzua vijana wengi.
SWALI: Ni kwa nini haukutumia pesa ya boom kujenga au kufanya miradi mikubwa ya kimaendeleo? Tatizo ni kula bata? Pesa ni ndogo kuliko uhitaji? Majukumu ni mengi kuliko ndoto zako?
Karibuni kwenye mjadala......
Kwangu, swali kama hilo sikutaka kulijibu maana ningelijibu lingenifanya nionekane sina nidhamu. Ninashukuru kwa sasa maisha yanaenda japo sijawahi kutumia pesa ya boom kufanya vitu vikubwa tofauti na kufungua miradi midogomidogo na kuishia kudhulumiwa au kukosa waendeshaji walio wema. Mafanikio yangu leo yanatokana na juhudi zangu binafsi na wala sio zile pesa za chuo ambazo huzuzua vijana wengi.
SWALI: Ni kwa nini haukutumia pesa ya boom kujenga au kufanya miradi mikubwa ya kimaendeleo? Tatizo ni kula bata? Pesa ni ndogo kuliko uhitaji? Majukumu ni mengi kuliko ndoto zako?
Karibuni kwenye mjadala......