Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,477
- 30,137
Habari kubwa nchini hivi sasa ni hizi ripoti za Amnesty International na Human Rights Watch kuionya Tanzania kuhusu mwenendo wake wa kila kukicha, tokea Rais Magufuli aingie madarakani mwaka 2015, kupeleka sheria Bungeni za kukandamiza vyombo vya habari, kuziminya kampuni zisizo kuwa za kiserikali na kuvipa wakati mgumu sana kufanya shughuli zake za kisiasa, vyama vya siasa vya upinzani.
Habari hizo zimepata "coverage" kubwa sana katika vyombo vya habari vya nje, kama vile BBC, VoA na Deutsche Welle, lakini nimeangalia vituo vyote vikubwa vya runinga hapa nchini, kama vile TBC na ITV, vyote hapa nchini havikutangaza kabisa hiyo habari.
Tumeshuhudia pia Waziri wa Sheria na Katiba akikiri kupokea ripoti hizo mbili za Amnesty International na Human Rights Watch na kuahidi kuwa wataijibu ripoti hizo kikamilifu.
Ndipo hapo ninapojiuliza hivi hizi habari hazikuwa na maslahi na nchi yetu, hadi wakuu wa vyombo vya luninga vyote vikubwa nchini kutotangaza habari hizo?
Au ndiyo tuseme kuwa wakuu wa vyombo hivyo vya habari "wametishwa" na watawala ili wasizitangaze habari hizo kubwa zenye maslahi mapana kwa Taifa letu, kuwa vituo hivyo vya luninga vitafungiwa vikitangaza habari hizo?
Tukumbuke kuwa hata enzi za Rais wa zamani wa Zimbabwe, marehemu Robert Mugabe, alitumia sana nguvu kubwa kuvidhibiti vyombo vya habari vya nchini kwake kutotoa habari zozote ambazo serikali hiyo haikutaka zitoke na matokeo yake ndiyo hayo tunayoyaona ya nchi hiyo kutengwa na kuwekewa vikwazo na jumuiya ya kimataifa, hali iliyowafanya wananchi wake waishi maisha magumu sana ya kulia na kusaga meno.
Je, watawala wetu nao wamejawa na kiburi cha madaraka hadi kututaka nchi hii nayo ipitie njia hiyo hiyo na "kuvitisha" vyombo vyetu vya habari visitangaze habari zozote hasi na kutaka vyombo vyote vya habari nchini viingie katika mapambio ya "kusifu na kuabudu" hayo mafanikio ya serikali hii ya utawala wa awamu ya tano?
Imenenwa na wahenga kuwa mficha ficha maradhi, mwisho kilio ndicho kitamuumbua!
Habari hizo zimepata "coverage" kubwa sana katika vyombo vya habari vya nje, kama vile BBC, VoA na Deutsche Welle, lakini nimeangalia vituo vyote vikubwa vya runinga hapa nchini, kama vile TBC na ITV, vyote hapa nchini havikutangaza kabisa hiyo habari.
Tumeshuhudia pia Waziri wa Sheria na Katiba akikiri kupokea ripoti hizo mbili za Amnesty International na Human Rights Watch na kuahidi kuwa wataijibu ripoti hizo kikamilifu.
Ndipo hapo ninapojiuliza hivi hizi habari hazikuwa na maslahi na nchi yetu, hadi wakuu wa vyombo vya luninga vyote vikubwa nchini kutotangaza habari hizo?
Au ndiyo tuseme kuwa wakuu wa vyombo hivyo vya habari "wametishwa" na watawala ili wasizitangaze habari hizo kubwa zenye maslahi mapana kwa Taifa letu, kuwa vituo hivyo vya luninga vitafungiwa vikitangaza habari hizo?
Tukumbuke kuwa hata enzi za Rais wa zamani wa Zimbabwe, marehemu Robert Mugabe, alitumia sana nguvu kubwa kuvidhibiti vyombo vya habari vya nchini kwake kutotoa habari zozote ambazo serikali hiyo haikutaka zitoke na matokeo yake ndiyo hayo tunayoyaona ya nchi hiyo kutengwa na kuwekewa vikwazo na jumuiya ya kimataifa, hali iliyowafanya wananchi wake waishi maisha magumu sana ya kulia na kusaga meno.
Je, watawala wetu nao wamejawa na kiburi cha madaraka hadi kututaka nchi hii nayo ipitie njia hiyo hiyo na "kuvitisha" vyombo vyetu vya habari visitangaze habari zozote hasi na kutaka vyombo vyote vya habari nchini viingie katika mapambio ya "kusifu na kuabudu" hayo mafanikio ya serikali hii ya utawala wa awamu ya tano?
Imenenwa na wahenga kuwa mficha ficha maradhi, mwisho kilio ndicho kitamuumbua!