Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,480
- 30,152
Kuna msemo maarufu wa Kiswahili unaosema kuwa kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza
Msemo huo una maana sana kwa sasa kwa jinsi siasa zetu zinavyofanyika, kwa kuwa CCM wanaamini kuwa wanawafanyia mazuri sana wananchi wa nchi hii ambayo hayajawahi fanyika huko siku za nyuma na kwa kuwa wao pia wanaamini kuwa wapinzani ni watu wa kupiga domo tu wananchi watakuwa weshajua kuwa hao ni wapiga domo tu, kwa maana hiyo hawatajishughulisha nao na badala yake watawapuuza.
Kwa maana nyingine CCM hawapaswi wajisumbue na wanachoongea wapinzani kwa kuwa wananchi watang'amua kuwa hao ni wapiga domo tu na wanachoongea ni cha uongo, wananchi watawapuuza na kuendelea kuwa na Imani na wao CCM
Lakini kinachofanyika ni tofauti sana na msemo huo kwa kuwa wao CCM ndiyo pekee ambao wanaruhusiwa kufanya siasa nchini na wapinzani wamezuiwa hadi mwaka 2020
Na wakithubutu kufanya siasa hiyo kwa kuwa Kikatiba wanaruhusiwa, basi Mwenyekiti wa CCM ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu hapa nchini, ataagiza majeshi "yake" ya Polisi yapige, yaue, na wawakamate viongozi hao wa upinzani na kuwafungulia mashitaka wapinzani kutokana na kukiuka "agizo" lake la kutofanya siasa hadi mwaka 2020!
Wakati hao Polisi wanajishughulisha mno na kuwadhibiti wapinzani wasifanye shughuli zao za kisiasa, wamekuwa wakiwaachia wenzao wa CCM wafanye shughuli zao za kisiasa kadri wanavyotaka!
Ndipo hapo ninapojiuliza hivi hawa CCM hawaujui huo msemo unaosema kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza?
Kwa kuwa mateso wanayopata viongozi wa upinzani, hususani wa Chadema hivi sasa ni TOO MUCH
Mungu ibariki Tanzania
Msemo huo una maana sana kwa sasa kwa jinsi siasa zetu zinavyofanyika, kwa kuwa CCM wanaamini kuwa wanawafanyia mazuri sana wananchi wa nchi hii ambayo hayajawahi fanyika huko siku za nyuma na kwa kuwa wao pia wanaamini kuwa wapinzani ni watu wa kupiga domo tu wananchi watakuwa weshajua kuwa hao ni wapiga domo tu, kwa maana hiyo hawatajishughulisha nao na badala yake watawapuuza.
Kwa maana nyingine CCM hawapaswi wajisumbue na wanachoongea wapinzani kwa kuwa wananchi watang'amua kuwa hao ni wapiga domo tu na wanachoongea ni cha uongo, wananchi watawapuuza na kuendelea kuwa na Imani na wao CCM
Lakini kinachofanyika ni tofauti sana na msemo huo kwa kuwa wao CCM ndiyo pekee ambao wanaruhusiwa kufanya siasa nchini na wapinzani wamezuiwa hadi mwaka 2020
Na wakithubutu kufanya siasa hiyo kwa kuwa Kikatiba wanaruhusiwa, basi Mwenyekiti wa CCM ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu hapa nchini, ataagiza majeshi "yake" ya Polisi yapige, yaue, na wawakamate viongozi hao wa upinzani na kuwafungulia mashitaka wapinzani kutokana na kukiuka "agizo" lake la kutofanya siasa hadi mwaka 2020!
Wakati hao Polisi wanajishughulisha mno na kuwadhibiti wapinzani wasifanye shughuli zao za kisiasa, wamekuwa wakiwaachia wenzao wa CCM wafanye shughuli zao za kisiasa kadri wanavyotaka!
Ndipo hapo ninapojiuliza hivi hawa CCM hawaujui huo msemo unaosema kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza?
Kwa kuwa mateso wanayopata viongozi wa upinzani, hususani wa Chadema hivi sasa ni TOO MUCH
Mungu ibariki Tanzania