Ni kwa namna gani naweza kupata kazi za Afya nchi za Ulaya?

Beberu

JF-Expert Member
Jan 26, 2017
3,797
7,437
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ndugu zangu wa Tanzania naomba kuuliza kwa wenye uzoefu juu ya kupata kazi za afya (uuguzi) katika nchi za ulaya

Mimi nina degree ya Uuguzi (bachelor of Nursing) sasa nataka kwenda kufanya kazi nje ya nchi hususani ulaya, marekani na canada

Naomba kuuliza kwa wenye uzoefu ni hatua gani za kupitia ili niweze pata na vitu gani ni vya muhimu

Natanguliza shukrani zangu za dhati kabisa

NB: Uzalendo naujua vizuri kabisa hivyo msinikumbushe
 
Mkuu hujatupa ndoano Tamisemi na Wizara ya Afya?

Huko majuu nadhani inahitaji koneksheni ndefu
 
Kama ni lengo lako hilo andaa PASSPORT kabisa..!
Pia fanya tafiti online kwenye nchi mbali mbali uweze kujua nafasi za kazi zinazopatikana huko..
Requirements zao ziko vipi kwa raia wa kigeni, na namna ya uapitkanaji wa visa ya kazi.

Pia usisahau kuangalia fursa na nhi tajiri za kiarabu kama UAE, Qatar, Na Saudi ...

Kazi nje mishahara mikubwa, na uki exchange kwa pesa za madafu... ndio kabisa
 
Safi comrade kuwa na mawazo hayo mkuu kila la kheri ila nakushauri pia angazia na hapa baran Afrika nchi kama Botswana huwa nasikia inapokea sana ma MDs na Nurses tokea tz
 
Kuna dada mmoja wa Kikenya nafikiri anaitwa Joyce yupo YouTube, mtembelee huyo kwenye channel yake ana taarifa nyingi kuhusu kupata kazi Canada.
 
Uwe na kibali cha kukuruhusu kufanya kazi huko, usome kozi zao wakupe vyeti vyao.
 
Nchi rahisi kwa wewe kwenda ni nchi za Scandivia. Tatizo ni lugha. Labda ukubali ku-apply chuo uwe kama unaenda kusoma tena halafu ukifika huko uone la kufanya. Ngoja nifanye research nikupe ushauri mzuri zaidi. Siyo leo lakini kwani niko bussy kidogo.
 
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ndugu zangu wa Tanzania naomba kuuliza kwa wenye uzoefu juu ya kupata kazi za afya (uuguzi) katika nchi za ulaya

Mimi nina degree ya Uuguzi (bachelor of Nursing) sasa nataka kwenda kufanya kazi nje ya nchi hususani ulaya, marekani na canada

Naomba kuuliza kwa wenye uzoefu ni hatua gani za kupitia ili niweze pata na vitu gani ni vya muhimu

Natanguliza shukrani zangu za dhati kabisa

NB: Uzalendo naujua vizuri kabisa hivyo msinikumbushe
Degree yako inatambuliwa kimataifa? Kuna shirika moja linafanya kazi ya uajenti kutafuta madakta na manesi specialist kwenda kufanya kazi Scandivia. Hulipi malipo yoyote na hata tiketi ya safari na course ya lugha ya nchi unayokwenda unapewa free. Tatizo moja kubwa ni kuwa unatakiwa uwe umefanya kazi nchi za EU angalau kwa muda wa mwaka.
 
Watu wenye akili zilizofanyiwa manipulation with electroshock na LSD kama wewe hamkosekani
Toa mchango wako kwa mtoa mada kama Mimi nilivyofnya itamsaidia sana mtoa mada kuliko Kuja hapa empty headed na kuanza ku attack waliotoa mawazo yao
 
Jaribu kuperuzi sana kwenye nchi zao
Kwa kuangalia hizo kazi utapata kila kitu wanachotaka na vigezo vyao

Kila la kheri mkuu
 
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ndugu zangu wa Tanzania naomba kuuliza kwa wenye uzoefu juu ya kupata kazi za afya (uuguzi) katika nchi za ulaya

Mimi nina degree ya Uuguzi (bachelor of Nursing) sasa nataka kwenda kufanya kazi nje ya nchi hususani ulaya, marekani na canada

Naomba kuuliza kwa wenye uzoefu ni hatua gani za kupitia ili niweze pata na vitu gani ni vya muhimu

Natanguliza shukrani zangu za dhati kabisa

NB: Uzalendo naujua vizuri kabisa hivyo msinikumbushe
Ulivyomalizia post yako umenichekesha mkuu...anyway Ile ww huna uzalendo ndo maana unatumia jina la beberu
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom