kibaravumba
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 6,635
- 7,005
Nimeona Irag limetokea tukio la kutisha.
Hata hivyo sio mara ya kwanza kusikia mitungi ya gesi ikilipuka.Hasa mitungi ya gesi ya kupikia majumbani.
Swali langu ni hili,je sababu ya kulipuka huwa ni nini?
Je, upo uwezekano wa kuchukua tahadhari au ndio hivyo ni kudra za mwenyezi Mungu tu?
Mbona sijawahi kuona elimu ya kuchukua tahadhari ikitolewa?
===
Watu 64 wamefariki Dunia na wengine 50 wamejeruhiwa baada moto Mtungi wa Oksijeni kulipuka katika wodi inayotibu wagonjwa wa Corona katika Hospitali ya Al-Hussein katika mji wa Nasiriya, kusini mwa Iraq.
Waziri Mkuu Mustafa Al-Kadhimi ameagiza kusimamishwa kazi kwa Meneja wa Hospitali hiyo na Viongozi wengine wa Hospitali na kuagiza wakamatwe kwa mahojiano zaidi.
Aidha Spika wa Bunge la Iraq Mohamed al-Halbousi ameandika ujumbe kwenye ukurasa wake wa Twitter akisema kuwa tukio hilo la moto katika hospitali hiyo ni uthibitisho tosha wa kushindwa kuwajibika katika majukumu ya kulinda maisha ya waIraqi, na ni wakati wa kukomesha janga hili".
Hata hivyo sio mara ya kwanza kusikia mitungi ya gesi ikilipuka.Hasa mitungi ya gesi ya kupikia majumbani.
Swali langu ni hili,je sababu ya kulipuka huwa ni nini?
Je, upo uwezekano wa kuchukua tahadhari au ndio hivyo ni kudra za mwenyezi Mungu tu?
Mbona sijawahi kuona elimu ya kuchukua tahadhari ikitolewa?
===
Watu 64 wamefariki Dunia na wengine 50 wamejeruhiwa baada moto Mtungi wa Oksijeni kulipuka katika wodi inayotibu wagonjwa wa Corona katika Hospitali ya Al-Hussein katika mji wa Nasiriya, kusini mwa Iraq.
Waziri Mkuu Mustafa Al-Kadhimi ameagiza kusimamishwa kazi kwa Meneja wa Hospitali hiyo na Viongozi wengine wa Hospitali na kuagiza wakamatwe kwa mahojiano zaidi.
Aidha Spika wa Bunge la Iraq Mohamed al-Halbousi ameandika ujumbe kwenye ukurasa wake wa Twitter akisema kuwa tukio hilo la moto katika hospitali hiyo ni uthibitisho tosha wa kushindwa kuwajibika katika majukumu ya kulinda maisha ya waIraqi, na ni wakati wa kukomesha janga hili".