Ni kipi hasa kilisababisha 'osagyefo' dr.kwame nkurumah kupinduliwa madarakani??

mkush

JF-Expert Member
Aug 19, 2011
214
161
Salaam wana jamvi wote!! Ninaomba mwenye data za uhakika juu ya nini hasa kilisababisha mwana wa afrika kwame nkurumah kupinduliwa hapo 1966,maana kuna uvumi kuwa alipinduliwa mara baada tu ya kuruhusu jengo la freemason lililokuwepo mjini accra kuvunjwa huku mwenzie nyerere akiliacha liendelee kuwepo mjini dar es salaam.je nadharia hiyo ina ukweli wowote na imani hizo??(kumbuka ushawishi wake ulikuwa juu sana afrika ukiachilia mbali intellectual arrogant aliyokuwa nao)
naomba wana jamvi mtililike juu ya hili
 
alipinduliwa na cia kwakuwa marekani ilikuwa na hofu juu ya harakati za kwame za kuliunganisha bara la africa na kukata mirija ya unyonyaji.hofu hiyo ya marekani ikapelekea kutuma majasusi wao wa cia kwenda kuratibu na hatimaye kumpindua masia dr. kwame
 
Nkwame Nkrumah, serikali yake ilikua ya rushwa, alitegemea jeshi la kuazima kutoka russia, pia hakua makini upande wa jeshi lake la watu wa ghana, salary kwa jeshi ilikua kidogo wakati yeye na watu wake wakifanya anasa kwa pesa ya serikali, ndo raisi ambaye ameingia kwenye historia ya kuongoza nchi nyingine tofauti na Ghana, baada ya kuondolewa madarakani 1966 alienda Gunea ya ikweta kuongoza nchi hyo kwa pamoja na raisi wa nchi hyo seke toure hadi alipofariki 1977
 
Kwame alikuwa kama Nyerere aliwekeza sana kukomboa na kuliunganisha Bara la Africa kuliko kutatua matatizo ya wananchi wake, sie Tz tulimstahi na kumvumili Mwl, Ghana hawakuvumilia ndio sababu wametuzidi kila kitu kasoro Ujinga,Maradhi na Umaskini. Alipinduliwa akiwa nje ya nchi kwny safari zake za ukombozi
 
Nkwame Nkrumah, serikali yake ilikua ya rushwa, alitegemea jeshi la kuazima kutoka russia, pia hakua makini upande wa jeshi lake la watu wa ghana, salary kwa jeshi ilikua kidogo wakati yeye na watu wake wakifanya anasa kwa pesa ya serikali, ndo raisi ambaye ameingia kwenye historia ya kuongoza nchi nyingine tofauti na Ghana, baada ya kuondolewa madarakani 1966 alienda Gunea ya ikweta kuongoza nchi hyo kwa pamoja na raisi wa nchi hyo seke toure hadi alipofariki 1977
Cheki kwenye google habari sahihi zaidi. Equatorial Guinea, zamani ikiitwa Rio Muni imepakana na Cameroon kaskazini na Gabon kusini na mashariki. Haikupata kuongozwa na Sekou Toure. Sekou Toure alikuwa wa Guinea. Ile inayopakana na Sierra Leone, Guinea Bissau, nk.
 
Sababu ya kupinduliwa kwake inaweza ikatolewa na pande mbalimbali zilivyoona mambo wakati huo. Tunamkumbuka Nkrumah alikuwa ambitious sana juu ya maendeleo ya nchi yake. Akosombo Dam ulikuwa mradi ambao ulianza kujengwa wakati wa Osagyefo na uliambatana na miradi mingi ya miundombinu nyingine na viwanda. Kuna hadithi kwamba aliomba ufadhili magharibi, na hawakumkubalia. Akapata ufadhili kutoka mashariki. Jambo hili lilileta ukaribu wa Ghana na nchi za kikomunisti wakati wa vita baridi. Hili ndilo, kwa maoni yangu, lilipelekea majasusi wa magharibi kufanya njama za kumwondoa. Ikumbukwe pia huyu bwana aliibukia kuwa mwanafalsafa wa masuala ya ujamaa na ukoloni mamboleo.
 
Salaam wana jamvi wote!! Ninaomba mwenye data za uhakika juu ya nini hasa kilisababisha mwana wa afrika kwame nkurumah kupinduliwa hapo 1966,maana kuna uvumi kuwa alipinduliwa mara baada tu ya kuruhusu jengo la freemason lililokuwepo mjini accra kuvunjwa huku mwenzie nyerere akiliacha liendelee kuwepo mjini dar es salaam.je nadharia hiyo ina ukweli wowote na imani hizo??(kumbuka ushawishi wake ulikuwa juu sana afrika ukiachilia mbali intellectual arrogant aliyokuwa nao)
naomba wana jamvi mtililike juu ya hili
Soma novel ya The Beatyful Ones are not yet Born by Ayi Kwei Armah utapata majibu ya kwa nini alipinduliwa
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom